Nondo azungumzia kutekwa kwake. Nina hofu sana na maisha yangu

Nondo azungumzia kutekwa kwake. Nina hofu sana na maisha yangu

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Matukio ya utekaji bado tishio nchini Tanzania kwa tukio la hivi karibuni, la kutekwa kwa Mwenyekiti wa Ngome ya vijana ya chama cha upinzani nchini Tanzania, ACT Wazalendo, Abdul Nondo ambapo kwa sasa akiwa amelazwa katika hospitali ya Agha Khan, jijini Dar es Salaam, baada ya kutekwa na kupatikana akiwa amejeruhiwa vibaya.

Nondo ameleza hali ilivyokuwa

Ilikuwa tarehe 30 novemba nilikuwa nimetokea Kigoma nikafika Dar es Salaam kwenye saa kumi alfajiri kwahiyo wakati na shughulikia usafiri ni kiwa tayari nimetoka kwenye geti la Magufuli Bus stendi, ndiyo wakatokea vijana kama sita wakanivamia wakaniambia tulia ambapo awali nilikuwa ninahisi ni vibaka.

Lakini nikaona jambo linakuwa siriazi zaidi, nikaona kuna gari limesongezwa Toyota hadtoku na milango ikiwa imefunguliwa ni nalazimishwa kungia kwenye gari. Kwahiyo mimi nilikuwa napiga kelele kupambana kuhakikisha kwamba siingii kwenye gari. Kwahiyo nikawa naomba msaada hata kwa watu wa pembeni pale nawaambia naombeni mnisaidie mimi naitwa Nondo njooni mnisaidie hakuna mtu aliyejitokeza, maana kulikuwa na bajaji pale kulikuwa na bodaboda lakini kulikuwa na watu walikuwa wanakwenye kupanda mabasi ili kusafiri kwahiyo walinizidi nguvu.

Hili tukio lilikuwa la ghafla sikuwa kabisa na fikra wala na wazo kwamba kuna mtu ananifuatilia. Watu walionikamata hawakujitambulisha wao ni wakina nani hata walipofanikiwa kuniingiza kwenye gari nilichofanikiwa kukisikia ni kwamba wakilaumia kwamba pingu zipo wapi? Baada ya kukosa pingu wakanifunga kamba kwa nguvu sana na mikono yangu walipeleka kwa nyuma ya mgongo na usoni wakanifunga kitambaa kwahiyo sikufanikiwa kuwatambua. Gari likaondoka kwa mwendo hadi likaingia sehemu likapaki wakanishusha wakanifungua kamba na wakanifunga pingu sasa na vilele wakiendelea kunifunga kitambaa machoni .

Wakanisogeza pembeni kidogo kama kuna kibalaza fulani hivi wakaanza kunipiga sana kwa kutumia magongo kwenye unyayo kwenye mabega, kwenye mapaja, kwenye magoti . Lakini pia baadae tena wakanifunga wakanininginza juu walinipitisha chuma mguu kwa mguu halafu pingu wakaiweka kwa chini huku wakiendelea kunipiga na neno kubwa waliokuwa wananiambia kwamba wewe si cha mdomo unaongea sana sasa hivi tutakuuwa mshezi wewe , yani walikuwa wananitukana matusi makubwa.

Baadae wakawasha gari na lilitemba umbali mrefu kidogo wakaenda sehemu wakalibadilisha gari na safari ikanza tena limetembea gari kwa umbali mrefu sana likafika sehemu likasimama nikatolewa jamaa akaniambia toka! Kutambea umbali kidogo kutoka usawa wa gari kwa mguu wakati natembea nikawa nahisi kama nakanya kokoto hivi na baada ya kutembea umbali kidogo hivi nikahisi mazingira kama ya bahari na mawimbi. Nikajuwa hawa watu wanaenda kunitupa baharini kwa sababu wamnifunga kamba na wamenifunga na macho wanaenda kunitupa baharini kwenye kina na kwahiyo nitakosa msaada na nitakufa.

Kwahiyo alivyonipeleka mpaka hapo akaniambia nikae chini nami nikaa akananiambia nisegeuke ukegeuka nakugonga risasi na mimi sikugeuka akachukua kama kisu akikata kamba aliokuwa amenifunga kwenye mikono na akanifungua kitambaa alichokuwa amenifunga kwenye macho kwahiyo akaniambia nikitokea hapa niende nyumbani moja kwa moja usipite sehemu yoyote na wala tusisike unahadhitia popote na wala tusisike sauti yako kwenye chombo cha Habari chochote kama tumeweza kukukamata na sasa hivi umekuwa mzima tunaweza hapahapa kukuuwa.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Nilikuwa naweza kutembea mwenyewe lakini kwa kazi sana nikatembea hadi nikatokea barabani na ilikuwa ni ufukwe wa coco nikaomba msaada kwa baadhi ya watu wakasindwa kunisaidia lakini nikakutana na bodoboda na yeye akaenda kuwaita na wenzie wakaja wakanihoji pale kutengeneza uaminifu. Bodoboda mmoja akakubali kunibeba akaniuliza nakupeleka home nikamwambia hapana nikamwambia anipeleke kwenye ofisi yetu ya chama pale magomeni kwaajili ya msaaada zaidi kwa sababu sikuwa na simu maana simu walichukua kwahiyo nikapokelewa na mlizi kwahiyo mlinzi akafanya mawasiliano na viongozi wa chama.

 
Matukio ya utekaji bado tishio nchini Tanzania kwa tukio la hivi karibuni, la kutekwa kwa Mwenyekiti wa Ngome ya vijana ya chama cha upinzani nchini Tanzania, ACT Wazalendo, Abdul Nondo ambapo kwa sasa akiwa amelazwa katika hospitali ya Agha Khan, jijini Dar es Salaam, baada ya kutekwa na kupatikana akiwa amejeruhiwa vibaya.

Ilikuwa tarehe 30 novemba nilikuwa nimetokea Kigoma nikafika Dar es Salaam kwenye saa kumi alfajiri kwahiyo wakati na shughulikia usafiri ni kiwa tayari nimetoka kwenye geti la Magufuli Bus stendi, ndiyo wakatokea vijana kama sita wakanivamia wakaniambia tulia ambapo awali nilikuwa ninahisi ni vibaka.

Lakini nikaona jambo linakuwa siriazi zaidi, nikaona kuna gari limesongezwa Toyota hadtoku na milango ikiwa imefunguliwa ni nalazimishwa kungia kwenye gari. Kwahiyo mimi likuwa napiga kelele kupambana kuhakikisha kwamba siingii kwenye gari.
Kwa hizi siasa za bongo, anajiamini vipi kupanda gari kutoka kigoma hadi Dsm? halafu hana hata mlinzi mmoja

Wakati huo huo yeye ni mkosoaji wa serikali

Kama anakosoa serikali katika hali ya umaskini wa hivyo bora aache siasa na uanaharakati, atakufa mapema sana tena kifo cha kikatili
 
Kwa hizi siasa za bongo, anajiamini vipi kupanda gari kutoka kigoma hadi Dsm? halafu hana hata mlinzi mmoja

Wakati huo huo yeye ni mkosoaji wa serikali

Kama anakosoa serikali katika hali ya umaskini wa hivyo bora aache siasa na uanaharakati, atakufa mapema sana tena kifo cha kikatili
Mbeya.

Chadema ina walinzi waliopitia mafunzo ya ukomando na walikamatwa viongozi na mmoja hajatolewa hadi leo na wanadai muda anachukuliwa alikua anapigwa.

Na makomando wapo hapo
 
Kwa hizi siasa za bongo, anajiamini vipi kupanda gari kutoka kigoma hadi Dsm? halafu hana hata mlinzi mmoja

Wakati huo huo yeye ni mkosoaji wa serikali

Kama anakosoa serikali katika hali ya umaskini wa hivyo bora aache siasa na uanaharakati, atakufa mapema sana tena kifo cha kikatili
Ukiwa na walinzi ndo hawakupati??Mbowe na wale makomandoo si kila siku wanambeba..watafanya nini?? Lema juzijuzi si katekwa kwenye ndege au hujui??
 
If you live by the sword, you die by the sword.

Mie wala siwasikiti wanasiasa waliokuwa wana-promote ujinga wa Magufuli eti alikuwa mtekaji.

Uongo sikuzote una madhara, huyu poyoyo kwangu hata angekutwa kakatwa vipande kwangu sawa.

Shida ni watu kama bonge wa pwani ambae ana maisha yake mengine kwanini atekwe au hata mzee Kibao ambae alikuwa low life.

Lakini mtu kama Nondo aliekuwa anashadadia Magufuli muuaji, atekwe tu na kundi lolote; he is useless anyway.
 
Mbeya.

Chadema ina walinzi waliopitia mafunzo ya ukomando na walikamatwa viongozi na mmoja hajatolewa hadi leo na wanadai muda anachukuliwa alikua anapigwa.

Na makomando wapo hapo
Actualy si wanachadema wote wanalindwa, only viongoz wa juu, the rest hawana ulinzi
 
If you live by the sword, you die by the sword.

Mie wala siwasikiti wanasiasa waliokuwa wana-promote ujinga wa Magufuli eti alikuwa mtekaji.

Uongo sikuzote una madhara, huyu poyoyo kwangu hata angekutwa kakatwa vipande kwangu sawa.

Shida ni watu kama bonge wa pwani ambae ana maisha yake mengine kwanini atekwe au hata mzee Kibao ambae alikuwa low life.

Lakini mtu kama Nondo aliekuwa anashadadia Magufuli muuaji, atekwe tu na kundi lolote; he is useless anyway.
Tecnicaly yeye ndio ameasisi haya. Sisem directly alinyonga mtu hapana. Before JK, mkapa, haya mambo yaliouwa ni very rare. Hata ikitokea ilikwua ni serious issue kwa serikali.

Alipokuja bwana mkubwa, ikapitishwa sheria iliyo waruhusu wale jamaa kukuamata, lakini sheria hiyo hiyo hakiunyosha watapeleka wapi watuhumiwa, maana hata polisi hawapeleki.
Such kind of activities zilianza kupewa nguvu, at a time zilikuwa zina repotiwa, then next phase no reports kabisa.

And thats how chama tawala, wanatumia hiyo loophole, jpm aliwaonyesha they dont have ku depend on plain politics, kuna other means za kubakia madarakani

No offence jpm alilita maendeleo, it was good. But kuna otherside he was not good
 
Kwa hizi siasa za bongo, anajiamini vipi kupanda gari kutoka kigoma hadi Dsm? halafu hana hata mlinzi mmoja

Wakati huo huo yeye ni mkosoaji wa serikali

Kama anakosoa serikali katika hali ya umaskini wa hivyo bora aache siasa na uanaharakati, atakufa mapema sana tena kifo cha kikatili
Yaani hata Abdul Nondo nae awe anatembea na bodyguard!
Duh
P
 
Tecnicaly yeye ndio ameasisi haya. Sisem directly alinyonga mtu hapana. Before JK, mkapa, haya mambo yaliouwa ni very rare. Hata ikitokea ilikwua ni serious issue kwa serikali.

Alipokuja bwana mkubwa, ikapitishwa sheria iliyo waruhusu wale jamaa kukuamata, lakini sheria hiyo hiyo hakiunyosha watapeleka wapi watuhumiwa, maana hata polisi hawapeleki.
Such kind of activities zilianza kupewa nguvu, at a time zilikuwa zina repotiwa, then next phase no reports kabisa.

And thats how chama tawala, wanatumia hiyo loophole, jpm aliwaonyesha they dont have ku depend on plain politics, kuna other means za kubakia madarakani

No offence jpm alilita maendeleo, it was good. But kuna otherside he was not good
Hadithi tu, Magufuli alikuwa mcha mungu

God rest his soul in eternal peace
 
Wanaotoaga Vipigo vya kwenye Unyayo, Magotini, mabegani ni wale wale hakuna asiyewajua coz style Yao ya kupiga Vibaka ndo Hiyo Hiyo.
 
Si hadith, is a fact, hakuwa saint, alikuwa na mazuri yake na mabaya yake pia
Kwenye mazuri tutamsifia, but kwenye tutasema tu. It simple as that
He wasn’t a Saint, but overall he was a good man at heart and good intentions kwa nchi yake.

Kwetu kumekucha 👋
 
Mbeya.

Chadema ina walinzi waliopitia mafunzo ya ukomando na walikamatwa viongozi na mmoja hajatolewa hadi leo na wanadai muda anachukuliwa alikua anapigwa.

Na makomando wapo hapo
Komandoo gani bila silaha za moto? Unadhibitiwa fasta na hata wakamataji wanapenda wanakuwa wanajua status Yako na hivyo wanachukua watu wenye medani hizo hizo.
 
Back
Top Bottom