Now mil 50 UTT, napambana ifike mil 65 mwaka huu

Uwekezaji na mitaji siyo lazima ufundishwe shule na sidhani kama kuna nchi wanasomesha wanafunzi wote kwenye hili jambo. Hii ni kama specialization. Watanzania kila kitu tunataka kifundishwe shuleni wakati shule tunakwenda kupata basic knowledge ya kuweza ku-grasp mambo mengine kwa kutumia maarifa tuliyopata. Kwa mfano kipindi cha korona, msomi yeyote alitakiwa atumie maarifa yake kujua kuwa kujifukiza hakuwezi kuua virus wa korona hata kama hakusoma field ya afya. Kwangu mimi tunaohoji kuhusu hii UTT, tuko sahihi 100%. Kabla hujafanya investiment popote pale, ni lazima ufanye research ya kutosha na siyo tu mtu anakupa ushuhuda eti ''niliweka fedha na nimeshapata faida''.
 
Pesa unazoweka NSSF, ni uwekezaji au sio?
Uwekezaji una vyanzo mbali mbali depends na morali ya mtu.
Mwingine anaona hawezi tunza kwenye Acc ya kawaida ya CRDB ambapo kila mwezi watakuwa wanamkata maintanance fee.
Heri aweke UTT aokote hata hiyo faida ya 1% monthly.
Mwingine anajitunzia kwenye kibubu ndani, mwingine anatunza kwenywe M pesa nk
 
Ukiona kitu kinapigiwa sana promo kuwa makini sana
Naona mkuu ungechukua hata dakika 45 kila siku katika kujifunza juu ya masoko ya uwekezaji na mitaji.
Kwenye huo upande ,siye ngozi nyeusi ndiyo bado hatujaamka kwenye huo upande, ila Waarabu na wahindi hapa nchini wanakula sana mema ya nchi katika hili.
Hakikisha baada ya miezi miwili unajua maana ya terms kama:Bond,Dividend, equity,Bills,Shares na Index.
Ujue tofauti ya Index fund,mutual na external traded fund...
By the way mi ni mwanataaluma wa Ujenzi,ila nilitenga mda kujifunza juu ya financial markets.
 
Nakubaliana na wewe 100%. Kila mtu ana choice yake na anafanya reseach kwa namna yake. Hii UTT nilikuwa naisikia tu ila mwezi uliopita nikaona niingie kwenye website yao (ambayo nayo sikuipenda sana). Nimesoma soma sehemu ya ''about us'' lakini sikuweza kujua ni nani wamiliki/mmiliki; na hisa za ownership (kama zipo) zikoje. Nikadhani labda ni hiki kiingereza changu kibovu, hivyo ngoja niulizie.
 
Huyo jamaa ni mpingaji,utamkuta kwenye kila uzi wa UTT anapinga..hayupo tayari kutaka kujielimisha wala kuelekezwa.
 
Kuna tofauti kubwa baina ya uwekezaji na Uhifadhi (investment vs saving).Katika benji,ile akaunti yako ya kawaida ni inaitwa saving account.
Faida ya saving account ni kwamba ukiwa na hitaji la haraka la fedha ni una uwezo wa kuitoa kupitia Simu,wakala au ATM.
Hasara yake ni kwamba unakatwa gharama ya kukuhifadhia na gharama ya kufanya miamala ya matumizi.

Kuwekeza hufanywa kwa kuweka fedha kwenye taasisi ambazo zimesajiliwa na kusimamiwa na Mamlaka ya mitaji Tanzania, C.M.S.A
Unawekeza fedha kwa kuikopesha serikali na makampuni kupitia hati fungani,na kuwekeza kwenye mfuko wa pamoja kama huo wa UTT , NIC na WATUMISHI.
Lakini pia kuna uwekezaji kwa kushiriki ununuzi wa Hisa.
 
Sahihi kabisa
 
Kwa kifupi UTT ni kampuni ya serikali mkuu,,kazi yake ni kumsaidia mwananchi kushiriki kwenye masoko mbalimbali ya mitaji. Kwa hyo wewe unaweza pia kushiriki moja kwa moja kwenye masoko ya mitaji bila kupitia UTT. kwa hyo UTT ni kama middle man anaye kusaidia kwenda kuwekeza kwenye masoko ya mitaji bila wewe kushiriki moja kwa moja.

Kuna faida nyingi za kushiriki kwenye masoko ya mitaji na hisa kupitia UTT badala ya wewe kwenda moja kwa moja.

1. Kwanza ni kampuni ya serikali,imeanzishwa kuwasaidia wananchi.

2. Ina wataalamu walio bobea katika masuala ya uwekezaji wa masoko na mitaji.

3.wao wanakusanya pesa kutoka kwa watu wengi,na hivyo kupelekea kupata riba kubwa wakienda kuwekeza kwenye masoko ya mitaji na hisa.. tofaut na ungeenda wewe moja kwa moja kwenye hayo masoko.


Faida ni nyingi kwa ufupi.
 
Watanzania hasa siye vijana, tujijengee desturi ya kujifunza vitu vipya, siyo kisa ni Daktari basi hautaki kujua kuhusu sheria hata kwa juu juu.
Kuna vitabu,kurasa za mitandao na videos.Hasa kwenye elimu ya usimamizi wa fedha yaani huko ndiyo wakenya na wanaijeria wanatupiga bao kila siku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…