Now mil 50 UTT, napambana ifike mil 65 mwaka huu

Now mil 50 UTT, napambana ifike mil 65 mwaka huu

Nakubaliana na wewe 100%. Kila mtu ana choice yake na anafanya reseach kwa namna yake. Hii UTT nilikuwa naisikia tu ila mwezi uliopita nikaona niingie kwenye website yao (ambayo nayo sikuipenda sana). Nimesoma soma sehemu ya ''about us'' lakini sikuweza kujua ni nani wamiliki/mmiliki; na hisa za ownership (kama zipo) zikoje. Nikadhani labda ni hiki kiingereza changu kibovu, hivyo ngoja niulizie.
Nenda kwenye ofisi zao, utapata elimu nzuri sana na utawaelewa.
 
Kuna tofauti kubwa baina ya uwekezaji na Uhifadhi (investment vs saving).Katika benji,ile akaunti yako ya kawaida ni inaitwa saving account.
Faida ya saving account ni kwamba ukiwa na hitaji la haraka la fedha ni una uwezo wa kuitoa kupitia Simu,wakala au ATM.
Hasara yake ni kwamba unakatwa gharama ya kukuhifadhia na gharama ya kufanya miamala ya matumizi.

Kuwekeza hufanywa kwa kuweka fedha kwenye taasisi ambazo zimesajiliwa na kusimamiwa na Mamlaka ya mitaji Tanzania, C.M.S.A
Unawekeza fedha kwa kuikopesha serikali na makampuni kupitia hati fungani,na kuwekeza kwenye mfuko wa pamoja kama huo wa UTT , NIC na WATUMISHI.
Lakini pia kuna uwekezaji kwa kushiriki ununuzi wa Hisa.
Got you. Mimi UTT niko Liquid fund, nilikuwaga pia na Bond. Ila Bond 10days kusubiria pesa vikanishinda, nikazitoa zote nikabaki na Liquid.
Inasaidia, kuna uhitaji mwingine wa pesa unakuwaga sio wa lazima sana, ila km pesa iko bank kuifikia ni chap sanaa.
Ila UTT kuna kauvivu flani kuifata ‘ kanasaidia
 
Kwa kifupi UTT ni kampuni ya serikali mkuu,,kazi yake ni kumsaidia mwananchi kushiriki kwenye masoko mbalimbali ya mitaji. Kwa hyo wewe unaweza pia kushiriki moja kwa moja kwenye masoko ya mitaji bila kupitia UTT. kwa hyo UTT ni kama middle man anaye kusaidia kwenda kuwekeza kwenye masoko ya mitaji bila wewe kushiriki moja kwa moja.

Kuna faida nyingi za kushiriki kwenye masoko ya mitaji na hisa kupitia UTT badala ya wewe kwenda moja kwa moja.

1. Kwanza ni kampuni ya serikali,imeanzishwa kuwasaidia wananchi.

2. Ina wataalamu walio bobea katika masuala ya uwekezaji wa masoko na mitaji.

3.wao wanakusanya pesa kutoka kwa watu wengi,na hivyo kupelekea kupata riba kubwa wakienda kuwekeza kwenye masoko ya mitaji na hisa.. tofaut na ungeenda wewe moja kwa moja kwenye hayo masoko.


Faida ni nyingi kwa ufupi.
Asante sana. Ni kampuni ya serikali. Bunge lilihusishwa wakati wa uanzishwaji au ni wizara tu au ni nani hasa? Kwa vifungu gani vya sheria? Board of directors na watendaji wake wakuu wanachaguliwa/kuteuliwa na nani?
 
Asante sana. Ni kampuni ya serikali. Bunge lilihusishwa wakati wa uanzishwaji au ni wizara tu au ni nani hasa? Kwa vifungu gani vya sheria? Board of directors na watendaji wake wakuu wanachaguliwa/kuteuliwa na nani?
Mkuu dhamira yako hasa ni nini?

Ushasema wewe huwezi kuweka feza zako huko na ukaeleweka sasa mbona kama unatengeneza chain ndefu ambayo haina maana yoyote?

Kwahiyo pia akitokea mtu akakushauri ukaweke Feza zako Bank katika Fixed Account, napo utataka uanze kujua ni manager gani alianzisha Fixed ACC, walikaaa kikao lini, wangapi wakakubali na wangapi wakakataa na walitumia vifungu gani vya katiba Yao?

Yani BOT kuweka mfumo wa kusaidia Wanachi katika uwekezekaji wa mitaji ni hadi Bunge likae,ujue kama lilianzia wizarani au kwa mtu binafsi umalizie na vifungu vya Sheria

Unauliza Mambo mengi ilimradi tu wewe uonekane wa tofauti sana, uonekane una Akili sana kuliko wanaoweka pesa zao, uonekane Mjanja sana, uonekane unajua sana sheria

Vile Unahoji kuhusu Bank kuu ya Tanzania as if ni Saccos/vikoba/Vikundi vya kina Mama mtaani kwenu, ushasema hutaki we acha wafanye wenye uhitaji usilete ujuaji mwingi ilhali hauna maana yoyote

Au uliwahi kuskia mtu katapeliwa huko kwenye UTT ili utujuze ilikuwaje mkuu?
 
Mkuu dhamira yako hasa ni nini?

Ushasema wewe huwezi kuweka feza zako huko na ukaeleweka sasa mbona kama unatengeneza chain ndefu ambayo haina maana yoyote?

Kwahiyo pia akitokea mtu akakushauri ukaweke Feza zako Bank katika Fixed Account, napo utataka uanze kujua ni manager gani alianzisha Fixed ACC, walikaaa kikao lini, wangapi wakakubali na wangapi wakakataa na walitumia vifungu gani vya katiba Yao?

Yani BOT kuweka mfumo wa kusaidia Wanachi katika uwekezekaji wa mitaji ni hadi Bunge likae,ujue kama lilianzia wizarani au kwa mtu binafsi umalizie na vifungu vya Sheria

Unauliza Mambo mengi ilimradi tu wewe uonekane wa tofauti sana, uonekane una Akili sana kuliko wanaoweka pesa zao, uonekane Mjanja sana, uonekane unajua sana sheria

Vile Unahoji kuhusu Bank kuu ya Tanzania as if ni Saccos/vikoba/Vikundi vya kina Mama mtaani kwenu, ushasema hutaki we acha wafanye wenye uhitaji usilete ujuaji mwingi ilhali hauna maana yoyote

Au uliwahi kuskia mtu katapeliwa huko kwenye UTT ili utujuze ilikuwaje mkuu?
Ahaaa. Sasa mkuu hapa umeweka mpira makwapani kiana. Mimi nataka kujua ili niondoa wasiwasi wangu. People change their minds, don't they?"
 
Ahaaa. Sasa mkuu hapa umeweka mpira makwapani kiana. Mimi nataka kujua ili niondoa wasiwasi wangu. People change their minds, don't they?"
UTT ni mutual fund (tumia Google kujua maana ya mutual fund) ambayo imeanzishwa maalum kwa ajili ya watanzania baada ya serikali (Mkapa) kuona watanzania hawana access na mifuk o mikubwa ya mitaji/uwekezaji.
Ipo chini ya Wizara ya fedha, imesajiliwa B.O.T na Mamlaka ya soko la mitaji C.M.S.A.

Wanabodi wake wengi ni wataalam wa fedha,uchumi na sheria.
Huku hakuna janja janja kwani ndipo moja ya taasisi kubwa inayoikopesha fedha serikali. Uendeshaji wake ni wa umakini coz inaisaidia serikali kupata credit rating nzuri kimataifa na ambayo huipa serikali unafuu wa kupata mikopo nje na uwekezaji.
 
UTT ni mutual fund (tumia Google kujua maana ya mutual fund) ambayo imeanzishwa maalum kwa ajili ya watanzania baada ya serikali (Mkapa) kuona watanzania hawana access na mifuk o mikubwa ya mitaji/uwekezaji.
Ipo chini ya Wizara ya fedha, imesajiliwa B.O.T na Mamlaka ya soko la mitaji C.M.S.A.

Wanabodi wake wengi ni wataalam wa fedha,uchumi na sheria.
Huku hakuna janja janja kwani ndipo moja ya taasisi kubwa inayoikopesha fedha serikali. Uendeshaji wake ni wa umakini coz inaisaidia serikali kupata credit rating nzuri kimataifa na ambayo huipa serikali unafuu wa kupata mikopo nje na uwekezaji.
Asante mkuu. Mutual fund najua maana yake. Angalau wewe umekuja na maelezo. Unajua watanzania wengi tuna utamaduni wa ''kutii bila shuruti'' na ukionekana kama unahoji basi wewe ni kibaraka na mpingaji. Mimi ni mtanzania na nimekulia Tanzania ambayo ''project'' nyingi zinazoanzishwa huwa zinakuwa hazina mwisho mzuri hivyo nina haki kabisa ya kuhoji.
 
SI kama hivi... Au we huoni kama ni promo hii
Bro,sio kupigiwa debe. Just tunawaeleza watu juu ya namna tofauti za low risk investment.
Ndiyo mana katika moja ya maoni yangu ,nimeshauri watu wajisomee juu ya financial markets.
Hata nawe unaweza ukafanya hivyo,mana Kuna course za online za bure nyingi tu Coursera, YouTube.,pitia platform kubwa kama Bloomberg ujifunze.
Ila yote ya yote ni hiyari ya mtu, ila jifunze uongeze maarifa siyo kubaki hivyo.
 
Asante mkuu. Mutual fund najua maana yake. Angalau wewe umekuja na maelezo. Unajua watanzania wengi tuna utamaduni wa ''kutii bila shuruti'' na ukionekana kama unahoji basi wewe ni kibaraka na mpingaji. Mimi ni mtanzania na nimekulia Tanzania ambayo ''project'' nyingi zinazoanzishwa huwa zinakuwa hazina mwisho mzuri hivyo nina haki kabisa ya kuhoji.
Nakuelewa mkuu,kwangu ilichukua zaidi ya miezi 6 kufuatilia juu ya Masuala ya Uchumi.
Fursa ni nyingi ila bado serikali haijaweza kuweka haya mambo vyuoni. Mwisho wa siku wahindi ndiyo wanaomiliki Uchumi wetu.
 
Nakuelewa mkuu,kwangu ilichukua zaidi ya miezi 6 kufuatilia juu ya Masuala ya Uchumi.
Fursa ni nyingi ila bado serikali haijaweza kuweka haya mambo vyuoni. Mwisho wa siku wahindi ndiyo wanaomiliki Uchumi wetu.
Ni fursa nzuri,ila nashangaa serikali haijaweka wazi kama ulivyo sema kwa kutoa elimu..mwisho wa siku wanafaidi wachache.
 
Back
Top Bottom