Now mil 50 UTT, napambana ifike mil 65 mwaka huu

Now mil 50 UTT, napambana ifike mil 65 mwaka huu

Baada ya kuufuatilia huu uzi kwa ukaribu. Nimejilipua, nilikua na kaakiba bank kama 20M hakazai chochote, nimekatoa nimekaweka pale UTT kwenye mfuko wa Ukwasi, ngoja tuone itakuaje.
safi sana mkuu,
nimeshangaa watu wanaona riba ya 10% et ndogo...... yani uwekeze kwenye risk free investment kwa faida ya 10% alafu uone ndogo?

wanasahau hio hela ukifanyia biashara inaweza kupotea ndani ya siku 2 na usiwe na uwezo wa kuiokoa.....

anyway, elimu ya masoko ya fedha tanzania bado sana!
 
Ndiyo.
Mfano umeanza kudeposit 1M, kila mwezi inaongezeka 1% yake.
Mwezi ufatao… ukawa na 1,001,000\= wanaweka 1% yake. Vivyo hivyo
hii nzuri sana aiseee........
sisi wenye matumizi mabaya ya visenti vijisent vikikaa benk huko utt kunatufaa
 
Sawa Mkuu ..Safi Sababu umeishasema Hautaki Risk za Biashara. Ila 50M Kwa profit ya 450 monthly, Kwa Mjasiliamali halisi asee is not Good Move!! Endelea kufikiri vema! Hizi ni Investiment Wanazofanya wastaafu baada ya kUchukua Mafao.....
Which is less than 16k per day 🙁
 
safi sana mkuu,
nimeshangaa watu wanaona riba ya 10% et ndogo...... yani uwekeze kwenye risk free investment kwa faida ya 10% alafu uone ndogo?

wanasahau hio hela ukifanyia biashara inaweza kupotea ndani ya siku 2 na usiwe na uwezo wa kuiokoa.....

anyway, elimu ya masoko ya fedha tanzania bado sana!
Naam, nimeona mambo yasiwe mengi, sikua najua hii kitu kabisa au pengine sikuwahi kufuatilia. Hata kama faida ndogo basi angalau itunze thamani ya pesa yako.
 
Kwa wengi ambao wanahofia juu ya masomo ya mitaji na uwekezaji hawana makosa.Wengi wa vijana iwe wasomi au sio wasomi,bado hawana elimu juu ya masomo ya mitaji na uwekezaji.
Hii kitu ilikuwa na umuhimu wa kuwekwa kwenye mitaala ya shule japo kwa kugusia tu.
Kama ingefanyika hivyo basi hata maneno kama Hisa,Hati fungani na Mirabaha isingekuwa misamiati migumu kwa watanzania.
Sijui kwanini haviwekwi. Yaani kwa hapa kwetu Tanzania ni kawaida sana kukutana na msomi wa chuo kikuu na pengine yupo kazini miaka kadhaa lakini hajui nini maana ya hisa, bond, na zinafaida gani na nani anaweza kuwekeza huko

Matangazo na elimu za kubeti zina nafasi kubwa sana ya kuifikia jamii kuliko mambo ya msingi kama haya
 
Mkuu dhamira yako hasa ni nini?

Ushasema wewe huwezi kuweka feza zako huko na ukaeleweka sasa mbona kama unatengeneza chain ndefu ambayo haina maana yoyote?

Kwahiyo pia akitokea mtu akakushauri ukaweke Feza zako Bank katika Fixed Account, napo utataka uanze kujua ni manager gani alianzisha Fixed ACC, walikaaa kikao lini, wangapi wakakubali na wangapi wakakataa na walitumia vifungu gani vya katiba Yao?

Yani BOT kuweka mfumo wa kusaidia Wanachi katika uwekezekaji wa mitaji ni hadi Bunge likae,ujue kama lilianzia wizarani au kwa mtu binafsi umalizie na vifungu vya Sheria

Unauliza Mambo mengi ilimradi tu wewe uonekane wa tofauti sana, uonekane una Akili sana kuliko wanaoweka pesa zao, uonekane Mjanja sana, uonekane unajua sana sheria

Vile Unahoji kuhusu Bank kuu ya Tanzania as if ni Saccos/vikoba/Vikundi vya kina Mama mtaani kwenu, ushasema hutaki we acha wafanye wenye uhitaji usilete ujuaji mwingi ilhali hauna maana yoyote

Au uliwahi kuskia mtu katapeliwa huko kwenye UTT ili utujuze ilikuwaje mkuu?
Utt watu wanaweka mabilioni we unataka kujua board of directors...

Sisi wabongo tunataka tuambiwe weka milioni upate milioni nyingine ndani ya mwezi ! Hakuna kitu km hicho, ndo maana akina kalaynda wanatupiga.
Ila kuweka milioni faida elf 50 mtu anaona ni ndogo
 
Habari,

Lengo sio kujitamba Bali ni kupeana chachu ya kuendelea kupambana. Leo nimefikisha 50ml lengo langu mwaka huu ni 65ml kutokana na saving zangu.

Sihitaji high return business bora nipate low return with minimal risk. Coz biashara imewahi nichakaza nikachanganyikiwa now sitaki kurudia makosa yaliopita. Kwangu UTT ni Bora zaidi! Nimewekeza Umoja, Jikimu, na Bond
Chukua hela wekeza kwenye miradi Yako uzalishe Zaid acha uvivu ww!
 
Back
Top Bottom