Nusuru ndoa yangu

Nusuru ndoa yangu

Inawezekana
1. Umeoa fukara na sasa kapata uhuru wa kifedha.

2. Umeoa mjinga na sasa kapata pesa ndio wauona ujinga wake.

3. Ulikuwa unamnyanyasa wakati hana pesa, na sasa kapata pesa ni muda wa kulipiza kisasi.

Hitimisho, katika yote hayo juu umeoa mwanamke asiyekuheshimu/asiyekutii...
Kuna bro alioa demu,demu akawa na kazi ya utumishi,bro akapanda cheo,kufika sehemu mafuso yakanunuliwa,na demu akawa na uhakika wa jumba la kifahari na mafuso ya mchanga yanaleta laki tatu kwa siku,yule manzi si kamuwangia jamaa hainuki kwenye wheel chair mwaka wa kumi sasa na mbususu hawezi kula anakula kwa macho tuu.mwanamke amegeuka meneja wa familia. bro anabaki kuita tuu jina,na mwangalizi ni ndugu wa mwanaume,Hawa watu weka mbali na watoto
 
Hahahaaaa pointi tatu muhimu tunapata hapa, endelea kuvumilia ulishajichanganya mwenyewe

1000011282.jpg
 
Akikutangaza kuwa hutoi matumizi unakufa? Mpuuze tu. Dawa kiburi mpe jeuri. Tafuta vijana wa kazi ongea nao chemba, waibe duka zima, wasiache hata dekio. Akifungua tena, wanapita nalo again. Yani ni tukio juu ya tukio.
Ka ana bwana anaempa mtaji wachoke wao. Inaumiza sana kuwa na mwenza unaempambania kwa maendeleo ya familia alafu akuletee fistula ya moyo.
 
Mkuu pole sana na chukua hii kama itakusaidia.

Kama kweli yupo kwako Kwa ajiri ya family hyo mkeo nakushauri vizia na uuze Kila kitu kwenye kibanda hicho halafu kaa kimyaa.

Iwapo utaona kuanzisha Tena basi jua wazi yupo mwingine zaidi Yako anayeheshimiwa na kupewa heshima yote.

La mwisho na LA muhimu sana

MWANAMKE SIO MAMA YAKO. KWANINI UTESEKE? make it this sentence in English language
 
Nakubaliana naww
Akikutangaza kuwa hutoi matumizi unakufa? Mpuuze tu. Dawa kiburi mpe jeuri. Tafuta vijana wa kazi ongea nao chemba, waibe duka zima, wasiache hata dekio. Akifungua tena, wanapita nalo again. Yani ni tukio juu ya tukio.
Ka ana bwana anaempa mtaji wachoke wao. Inaumiza sana kuwa na mwenza unaempambania kwa maendeleo ya familia alafu akuletee fistula ya moyo.
 
Maduka yanafilisika hasa ukiwa na tabia ya kutoa mahitaji ya nyumbani.

Ukitaka biashara isiyumbe kila mwisho wa mwezi mwongezee mzigo dukani.

Sema na umemchoka tu, yaani hizi nguo za kike za elfu 25 na perfume ndo vivunje ndoa.

Hebu tuliza akili angalia familia yako.
 
Yajayo yanafurahisha .
USHAURI MZURI TU.
1. Usimuitie mtu mwambie kwa upole akija juu basi mwachie majukumu yote kuanzia ada,mavazi ya watoto,mishahara ya wafanyakazi chochote kile kinachohusu pesa unamwambia mwambie mama akupe. Akija kuomba msahada mjibu mtaji wangu umeisha.

Usile nyumbani , tena kula kwingine maana upo kwenye ugomvi,. Soo huna raha. Penda kutafuta makao mapya uishi kwa amani hata kama nikuhama kimkoa. Pokea simu yake ila usimpigie labda umpigie pale unataka kuwajulia hali watoto . Hata kama hawali tafuta njia ya watoto wapate chakula ila usimtumie yeye. Hata kama ni chipsi ni sawa.

Kwa mwaka tu atarudisha akili ubongoni. Atatulia tuli . Kupigana na mtu hata kama ni mwanaume nikukosa maarifa

Good day
 
Maduka yanafilisika hasa ukiwa na tabia ya kutoa mahitaji ya nyumbani.

Ukitaka biashara isiyumbe kila mwisho wa mwezi mwongezee mzigo dukani.

Sema na umemchoka tu, yaani hizi nguo za kike za elfu 25 na perfume ndo vivunje ndoa.

Hebu tuliza akili angalia familia yako.
Acha kutetea ujinga
 
Chukua funguo ukachongeshe za bandia tafuta vjana wa kazi wakaibe duka zima uza hivyo vyote, msikilizie akirudisha mraji jua unasaidiwa, kama anasema mtaji wako ulishaisha jua kua kuna mtaji mwingine ulishawekwa
 
Kama ile frem ya dukani uliiikodi ww kwenye mkataba fanya jambo tafuta kijna wa kuuza duka, tafuta frm mpya sehemu nyingine lipia bila mkeo kujua,

Mtafututie mkeo safali japo ya siku 3 akiwa amesafili amisha duka , akirudi duka limeamishwa na kule anauza kijana mwingine , mwambie atulie nyumbani,


Mwanamme unatakiwa kuwa na kauli ndani ya nyumba,
 
MUNGU hakuwa na mpango wa ndoa za kizazi hiki period, na bado mtaisoma namba..
 
Mimi ni muajiriwa katika sekta ya umma mke wangu sio mwajiriwa yaani ni mama wa nyumbani. Tuko kwenye ndoa ya kikristo kwa miaka 14 na tumejaaliwa watoto.

Ili kupunguza ukali wa maisha na kuondoa utegemezi kwa mambo madogo madogo, niliamua kufungua kibanda cha duka na kumkabidhi mke wangu ili kisaidie kwa baadhi ya mahitaji muhimu ya nyumbani huku Mimi nikitumia sehemu ya mshahara kuwekeza kwenye maeneo mengine ya maendeleo.

Ni mwaka mmoja na miezi kadhaa imepita tangu nimfungulie mke wangu biashara lakini jambo la kusikitisha ni kuwa sioni tena faida ya kibanda kile maana mke wangu anabadilisha aina za nguo na marashi huku nikimuuliza anadai kuwa ananiheshimisha kwa watu. Pia ananitangaza kwa ndg na jamaa zake kuwa sitoi matumizi yeye ndiye anayetoa matumizi.

Tumekaa vikao kadha wa kadha tukihusisha ndg zetu lakini haonekani kubadilika na kikao cha mwisho alitamka kuwa mtaji wangu umeishahivyo uliomo ni wa kwake.

Hali hii imesababisha migogoro ya mara kwa mara na sioni tena raha ya ndoa.

Pia hali hii imenijengea tabia ya kumchukia mke wangu mara kwa mara ninashikwa na hasira hata bila sababu ya msingi japo kiukweli Sina nia ya kuvunja ndoa yangu bali ninahitaji mke abadili tabia.

Ninaomba ushauri ili kunusuru ndoa yangu.

Ahsanteni.
Mwachie na usijihusishe na chochote kwenye hilo duka. Endelea kufungua miradi mingine kaa huko ukipiga kazi. Usisahau kuwa kwenye maisha kuna wewe mwenyewe bila ya mtu mwingine. Jijali brother
 
Mkuu kwanza pole kwa changamoto, kwa uzoefu wangu mdogo wa kwenye masuhala ya ndoa hapo shemeji yetu kuna mtu anampa kiburi ndio mana kwa sasa hakuheshimu tena kwa sababu huko nyuma alikuwa anakuheshimu sana hapo busara inaitajika sana
 
Back
Top Bottom