Nyimbo za Bongo Fleva kupigwa Airport ni uamuzi wa busara?

Je? Hizo ni bongo fleva? [emoji45] [emoji45] [emoji45]

Sent from my CPH2251 using JamiiForums mobile app
 
Kwanini usiseme nyimbo za matusi zisipigwe na sio Bongo Fleva ? Unajuaje kama watapiga za Matusi au kwanini wasiwashauri wadau wawe na radio version ambayo haina matusi...

Hivi unajua hata nyimbo za ughaibuni zinaimba nini au sababu ni lugha....; au nikuwekee chache....

In short kupangia watu cha kusikiliza its so yesteryear.., kama ni kukuza utalii basi zipigwe zenye maudhui ya utalii au wasanii wabadilishe wawe na utalii versions....

Nyimbo kama za Remmy Ongala nitarudi Mwanza au hata za Pepe Kalle nimepoteza kipenzi changu au ile marashi ya Karafuu Zanzibar its all it's all about no matter nani kaimba.....
 
NAKAZIA.
KWANZA MUZIKI wetu ni UPI? AMAPIANO AU NIGERIAN? NAOMBA KUJUZWA MUZIKI ASILI YETU NI UPI NA WANAMUZIKI WAPI NDIO WANAIMBA.

Sent from my CPH2251 using JamiiForums mobile app
Si kuna kamati iliundwa na kupewa zaidi ya milioni 300 itafute mdundo wa Taifa na baadae vazi la Taifa?
Waulize iko wapi?
Hii nchi unaweza ukaamua kula hata bilioni mchana kweupe mbele ya kamera na hakuna wa kukuuliza.
 
Mkuu watu wanakariri upuuzi tu lakini kiukweli Kuna nyimbo nyingi sana
Hizo nyimbo nyingi zimewahi kupigwa wapi?
Maskini na wanyonge hawajawahi kuzisikia hizo nyimbo, hawana kwenye flash wala haizpigwi redioni.
wewe unazisikiaga wapi ama una mawazo yako kichwani tu ndio unafikiri kila mtu anawaza hivyo?
Umewahi kuhudhuria sherehe za mwenge, uhuru, sehemu waknakuja viongozi wa kitaifa, ma dj si wanapigaga nyimbo hizo hizo za matusi?
Mikesha ya mwenge nchi nzima wanapigaga nyimbo gani?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my CPH2251 using JamiiForums mobile app
 
Muziki ni sehem ya kuulinda na kuusambaza utamaduni wa nchi kupitia sanaa hiyo..tatizo linakuja je,tumeweka nguvu kwenye kuulinda utamaduni wetu kupitia sanaa ya Muziki???ukiangalia wanaMuziki wanaovuma hapa Tz wengi wao hawafanyi muziki wa asili na utamaduni wetu,wanaiga kutoka mataifa mengine,hizo nyimbo zitakazopigwa hapo lengo ni nini?au wanaleta siasa kwenye mambo ya msingi?
 
Mdogo wangu MWANA FA, pitia hu ujumbe, Utamaduni wetu ndio hao akina Zuchu na Diamond ku-zalisha wanawake zaodi ya 5 na kwaacha:
Kujichora tatoo na kutumia madawa ya kulevya, alafu kamishna wa madawa anawabembeleza eti anawajua ataanza kuwafuatilia, nikajichekea mie eti awafuatilie wakati ndio wapiga kampeni wakuu wa CCM?
 
Muziki unatumika kuanzia kizazi kilichopita,kilichoko na kinachoingia kuanzia sasa na kama ulivyosema nyimbo nyingi n sample za nyingine hazina asili ya hapa.

Hivyo nyimbo zitakazotumika ni zile zilizobeba uasilia wetu na zipo nyingi sanaaa.kuanzia za wacheza ngoma,wazeee wa kughani sauti(mpoto) taarabu,zilizopendwa.

Hakuna hisia kali kama hii kwa mgeni pata picha umeshuka london alafu unadikia country music zinapigwa unaanza kufil uko uingereza kabla hata haujakutana na chochote kile na mziki una tengeneza kumbukumbuku.

Kwa mgeni ambaye anapenda music ataanza kuulizia habari za wimbo unaopigwa na wasanii wanaopatikana Tz.
 
Waweke zele nyimbo za,inama nkupak mafuta itereze taratibu

Itapendeza

Ova
 
Upo uwanja wa ndege, nyimbo hizo za ngono zinapigwa, mgrni anavutiwa na mdundo, hajui Kiswahili anakuuliza kinachoimbwa!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Hapo kazi kwa mchaguaji DJ..
 
Sasa nyie mna mkosi gani?
Kila mahali mnataka mziki tu kuanzia kwenye sherehe, vilio, kwenye mabasi, na sasa airports
Mwafrika ana shida mahali sio bure
Huyu jamaa arudi kwenye miziki yake na matusi
Jitu Zima linawaza kukata kiuno nani ana shida ya mziki airport kama sio upumbavu wa akili zao hizo
Nakereka sana kuona mziki unapigwa kwenye sehemu zisizokuwa mahali pake
Kaona kuitangaza Tz ni mziki
Kina Miriam Makeba nyimbo zao ziliuzika mpaka ulaya miaka ya 70 kwani ilipigwa airport?
Mtu anakuja nchini anaondoka anasikitika kwa kuulizwa hongo bila kosa
Unafikiri atajali huo mziki
 
Kwa uchungu na ukweli umenena.
 
Siasa za Bongo.
Akili kubwa inaongoza akili ndogo.
Bongo nyosoπŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”.
Utaambiwa,tumepiga hatua katika tasinia.πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kwanza watu wengine hawapendi mikelele ya mziki, kwa hiyo mwenyewe kaona kafanya kazi kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…