Hahahahaahha.... I Kanti You!! Mimi mvivu wa kucheza toka utotoni nitakuwa nawashangalia wewe na kaka B hapo mkiingia Kati....
Wewe dotcom hujui hio michezo,nyimboHahahaaaa!!
Huu uzi umenikumbusha mbali sana.
Ha ha ha ha hapo una paka mate mkononi ......ile ya kuimba mko mduara (kama una wako mshike kiuno chini kwa chini ehee chini kwa chini)
Hahahaaa hahaha du sio kwa kichapo kile maana nilihisi naishiwa damu asingekuwa bibi kusema nmetosha ningekufa wallahAaahahahahahhahahahahahaaa aahahahahahhaahahhaahhahahahaa eehehehehehehehehheheheeeee yaani weweee umenifanya nicheke kwanguvu hapa nilipo loooh
Nimevuta taswira jinsi ulivokuwa unaimba huo wimbo kwanguvu bila wasiwasi unashangaa unavutwa ndani paaah paaah kichapo loooh.
Pole mwaya looh nimecheka hadi machozi looh.
Hivi huwa unafikiri mimi mtoto mwenzio?Wewe dotcom hujui hio michezo,nyimbo
Mtu mmoja ana kidendele,
Keshokutwa tutamnyoa nywele.
Moja chama chetu cha umoja
Mbili macho kama pilipili
Tatu, Tatu mwizi wa mapera
Nne:mwanne acha uhuni
Tano, kwa mchuzi wa manjano
Sita,baharini kuna vita
Saba,sabasaba imefika
Nane,zunguruka tuonane
Tisa,kwa Mzungu kunatisha
Kumi, kwa magumi na mateke
Hehehehehehehehee haki ya nanihii
Huu ilikuwa unamuwekea mtu kitu chochote mfano ganda la nyanya kichwani bila yeye kujua halafu unaanza kuimba .......
Mtu wangu ana kideengeelee
Kesho kutwa nitamnyoa nyweleee
Hahahahahahhaaa basi ukisikia hivyo unaanza kujipukuta kama umewekewa kitu mwilini au kwenye nguo looh.
Halafu hiyo ID yako nakumbuka zamani enzi zile maikalus bado yapo mjini, kulikuwa na daladala moja linaitwa Chakochangu.
Malhaba kumekucha kwa bongo mpya ya viwonder.Shikamoo bi mkubwa
bubu hasemi ,,miMama wa kambo, mbo
Mbona wanitesa sa
Sasa naondoka ka
Kaa peke yako ko
Koti la babu bu
Bubu asemi mi
Mimi nasema ma
Mwengine aendelee..
Hizi nyimbo hata origin haijulikan..!
Hahahahahaaa!!! Hapa, nipo kwenye kikao. Nimecheka kimya kimya baada ya kuona huu wimbo.Ana Ana Ana do,
Kachanika basto,
ispiringi matingo,
kajamba, ushuzi unanuka, tena sana, sana kabisa.
Nadhani huu wimbo ulikuwa wa kizungu ukaswahilishwa, kama kuna mtu anaujua asili yake anaweza kutuhabarisha.
Aisee..! Hii mechanism yake sikuielewa kabisaa..! Yaani vinatokea kabisa vidoa vyeupe hasa kidole cha kati..!Vipi yange yange walishawahi kukupa kucha nyeupe? Wakipita juu tulikuwa tubaimba
Yange yange nipe kucha nyeupeee....
Cha ajabu kweli kwenye kucha kunatokea vidoa vyeupe!