Acha kubisha usicho kijua Mzee baba,hii ni uhalisia kabisa inatokea kila siku maeneo husika fika siku moja use shuhuda kwa wabishi wenzako.Nyongo ya mamba siyo sumu. Ni uvumi potofu tu. Majaribio mengi yameshafanywa na wanasayansi na wote wamesema siyo sumu! Mwaka 2015 nchini Msumbiji walikufariki watu 75 kwenye sherehe baada ya kunywa pombe ya kienyeji. Uvumi ukavumishwa eti wamepewa sumu ya mamba. Wanasayansi wakafanya utafiti na kukuta ni aina ya bacteria waliosababisha hivyo vifo kwa sumu yao na siyo sumu ya mamba.
Mafundi mitambo wetu wataweka sawa.Mbona hizo picha A&B ni kende na dushelele?
Ini gani lenye sura ya mgawanyiko wa namna hiyo?
Halafu sasa kuna electric wire zimeunganishwa, imekaaje hii, ni model?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ushawahi itumia?au unafuata upepo unapovuma?Nyongo ya Mamba siyo sumu, ni uzushi na uongo uliozoeleka miongoni mwa jamii za kishirikina, sio kweli hata kidogo kwamba Nyongo iwe sumu.
Sasa wewe niambie kazi ya hiyo nyongo ya mamba mwilini mwa mamba ni ipi???
Nyongo ipo kwa binadamu, kwa kuku, mbuzi nk, kazi yake ni kumeng'enya mafuta ndani ya utumbo mwembamba, ndani ya utumbo mwemba ndimo usagaji wa chakula hufanyika.
Mamba hula vyakula vyenye protein na mafuta hivyo nyongo inamsaidia kuyeyusha mafuta yatokanayo na vyakula anavyokula.
Nyongo (bile) ni digestive juice.
Watu wengi wenye imani kwamba nyongo ya mamba ni sumu hao utakuta wamekulia katika imani za kishirikina na uchawi.
Kama nyongo hiyo ingekuwa ni sumu mbona yeye mwenyewe mamba si angekufa kabla ya kuua watu wengine au hata nyama yake isingekuwa inaliwa au hata kinyesi chake kingekuwa ni hatari na sumu kubwa.
Tumieni akili kuliko kupinga kijinga kwa kufuata mkumbo tu.
Angalia ndani ya Google uone watu waliofanya hizo tafiti.
Crocodile bile lethal poison??
Naongelea utafiti wa kisayansi na si ubishi au uzushi potofu unaoeneze wewe. Naongelea wataalam waliofanya research kwa kuwalisha panya na nyani nyongo ya mamba na haikuwa na matokeo yoyote mabaya. Naongelea scientific facts na siyo mapokeo ya simulizi za mababu kama unavyofanya wewe! Naongelea mambo yaliyofanywa maabara na siyo bla blah za mtaani kama wewe!Acha kubisha usicho kijua Mzee baba,hii ni uhalisia kabisa inatokea kila siku maeneo husika fika siku moja use shuhuda kwa wabishi wenzako.
Ushawahi itumia?au unafuata upepo unapovuma?
Nishashudia watu wameathirika kwa kutumia ikichanganywa na dawa za kienyeji au kichawi.Na wewe nikuulize swali hilohilo, je umeshaonja nyongo ya mamba kuthibitisha kwamba ni sumu??.
Matumizi ya Nyongo ya mamba kama kiungo (additive) katika miti-sumu ili kufanya sumu hizo ziwe kali na kuua kwa haraka ni Elimu au sayansi inayopatikana katika maeneo yetu ya Afrika mashariki na kati, kusini na magharibi, ni elimu inayotumiwa hasa na Waganga na wachawi katika kutengeneza hizo sumu ili kudhuru watu. Ni elimu inayohusikana na mambo ya kichawi.
Asee usibishe! Kakonko nimewahi kaa pale kwa siku 10. Ni Kimji kidogo lakini kina Wehu wengiHapana labda kwa sumu ndiyo inaongoza wehu wengi sidhani lakini wapo,matukio ambayo Ni common ukichaa na kujinyonga yapo huko ila muongoza gwaride Ni Sumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Tumeishi sote kakonko pia.Asee usibishe! Kakonko nimewahi kaa pale kwa siku 10. Ni Kimji kidogo lakini kina Wehu wengi
Kumbe wewe ni JangiliTunaenda kuwashika ziwani au mto ruaha ile nyongo tunatoa ile sumu kwa ajili ya mishale yetu ya kuwindia tunachanganya namiti pori fulani mizizi yake basi hata tembo ukimpiga mshale ule au nyati mita 5 tu mbele hapo hapo ganzi anadondoka
Anataka aionje ili athibitishe kama ni kweliUnaitaka ili uifanyie kazi gani?
Kuna mapaka yanasumbua kila nikiyalisha sumu ya panya hayafiUnaitaka ili uifanyie kazi gani?
Nani kakudanganya kuwa ni nyongo ya mamba ni sumu?Kuna mapaka yanasumbua kila nikiyalisha sumu ya panya hayafi
Kweli, hayo maeneo hakuna Mambo hayo. Hata mtoa maada anasema, eti Kigoma mjini, mwanga, Ujiji? Mzushi tu. Huku Kuna ustaarabu bwana.Acha kupotosha na kuwatisha watu bhana toka nakua kwetu mwambao wa ziwa kuelekea Kagunga sijawahi kusikia mtu kauawa au kufa kwa kuwekewa sumu ya mamba kwenye kahawa.Nasikia sumu ya nyongo ya mamba ni hatari ila huo utaratibu ndio mgeni kwangu maana toka Kalalangabo,mtanga na ngelwe yake,Kazinga,mwamgongo,Bugamba,Zashe kagunga mpaka kuelekea huko nchi jirani sijasikia historia hii labda huko kusini.
Cha msingi ni kujihadhari kabla ya hatari hakuna sumu tamu na wala hakuna muuaji asiyekujua.
"Proudly, brought to u by Bachelor Sugu"