Nyongo ya mamba ni sumu kali inayouwa kwa haraka zaidi

Nyongo ya mamba ni sumu kali inayouwa kwa haraka zaidi

Nyongo ya mamba siyo sumu. Ni uvumi potofu tu. Majaribio mengi yameshafanywa na wanasayansi na wote wamesema siyo sumu! Mwaka 2015 nchini Msumbiji walikufariki watu 75 kwenye sherehe baada ya kunywa pombe ya kienyeji. Uvumi ukavumishwa eti wamepewa sumu ya mamba. Wanasayansi wakafanya utafiti na kukuta ni aina ya bacteria waliosababisha hivyo vifo kwa sumu yao na siyo sumu ya mamba.
Acha kubisha usicho kijua Mzee baba,hii ni uhalisia kabisa inatokea kila siku maeneo husika fika siku moja use shuhuda kwa wabishi wenzako.
 
Nyongo ya Mamba siyo sumu, ni uzushi na uongo uliozoeleka miongoni mwa jamii za kishirikina, sio kweli hata kidogo kwamba Nyongo iwe sumu.

Sasa wewe niambie kazi ya hiyo nyongo ya mamba mwilini mwa mamba ni ipi???

Nyongo ipo kwa binadamu, kwa kuku, mbuzi nk, kazi yake ni kumeng'enya mafuta ndani ya utumbo mwembamba, ndani ya utumbo mwemba ndimo usagaji wa chakula hufanyika.

Mamba hula vyakula vyenye protein na mafuta hivyo nyongo inamsaidia kuyeyusha mafuta yatokanayo na vyakula anavyokula.

Nyongo (bile) ni digestive juice.

Watu wengi wenye imani kwamba nyongo ya mamba ni sumu hao utakuta wamekulia katika imani za kishirikina na uchawi.

Kama nyongo hiyo ingekuwa ni sumu mbona yeye mwenyewe mamba si angekufa kabla ya kuua watu wengine au hata nyama yake isingekuwa inaliwa au hata kinyesi chake kingekuwa ni hatari na sumu kubwa.

Tumieni akili kuliko kupinga kijinga kwa kufuata mkumbo tu.

Angalia ndani ya Google uone watu waliofanya hizo tafiti.

Crocodile bile lethal poison??
Ushawahi itumia?au unafuata upepo unapovuma?
 
Acha kubisha usicho kijua Mzee baba,hii ni uhalisia kabisa inatokea kila siku maeneo husika fika siku moja use shuhuda kwa wabishi wenzako.
Naongelea utafiti wa kisayansi na si ubishi au uzushi potofu unaoeneze wewe. Naongelea wataalam waliofanya research kwa kuwalisha panya na nyani nyongo ya mamba na haikuwa na matokeo yoyote mabaya. Naongelea scientific facts na siyo mapokeo ya simulizi za mababu kama unavyofanya wewe! Naongelea mambo yaliyofanywa maabara na siyo bla blah za mtaani kama wewe!
 
Ushawahi itumia?au unafuata upepo unapovuma?


Na wewe nikuulize swali hilohilo, je umeshaonja nyongo ya mamba kuthibitisha kwamba ni sumu??.

Matumizi ya Nyongo ya mamba kama kiungo (additive) katika miti-sumu ili kufanya sumu hizo ziwe kali na kuua kwa haraka ni Elimu au sayansi inayopatikana katika maeneo yetu ya Afrika mashariki na kati, kusini na magharibi, ni elimu inayotumiwa hasa na Waganga na wachawi katika kutengeneza hizo sumu ili kudhuru watu. Ni elimu inayohusikana na mambo ya kichawi.
 
Na wewe nikuulize swali hilohilo, je umeshaonja nyongo ya mamba kuthibitisha kwamba ni sumu??.

Matumizi ya Nyongo ya mamba kama kiungo (additive) katika miti-sumu ili kufanya sumu hizo ziwe kali na kuua kwa haraka ni Elimu au sayansi inayopatikana katika maeneo yetu ya Afrika mashariki na kati, kusini na magharibi, ni elimu inayotumiwa hasa na Waganga na wachawi katika kutengeneza hizo sumu ili kudhuru watu. Ni elimu inayohusikana na mambo ya kichawi.
Nishashudia watu wameathirika kwa kutumia ikichanganywa na dawa za kienyeji au kichawi.
 
Nahitaji hii sumu naipataje? Mwenye kujua jinsi naweza kuipata naomba msaada?
 
Sisi ambao sio wa wabishi na ambao tunapenda kujifunza tunashukuru kwa taarifa.
 
Tunaenda kuwashika ziwani au mto ruaha ile nyongo tunatoa ile sumu kwa ajili ya mishale yetu ya kuwindia tunachanganya namiti pori fulani mizizi yake basi hata tembo ukimpiga mshale ule au nyati mita 5 tu mbele hapo hapo ganzi anadondoka
Kumbe wewe ni Jangili
 
Nyongo ya Mamba ni sumu kali mno

Hata ikitokea mamba amekufa mtoni, serikali ikifahamu inaweza kuwazuia watumiaji wa maji ya mto huo wasitumie maji kwa siku nzima

Watu wa Maliasili na wanajeshi huwa wanachinja mamba wakubwa waliozeeka na kuchukua nyongo na magamba TU, nyama wanaweza kuwaachia wananchi mle mpaka muache.

Kwa aliyekula nyama au mafuta ya mamba anajua ni jinsi gani inavyoleta KIU, unaweza kunywa maji Lita 5 kwa siku na bado kiu isiishe.

Babu yangu alikuwa na mkuki na nyongo ya mamba kidogo kwenye kikopo cha Kiwi, lakini alikuwa anaficha darini.
 
Acha kupotosha na kuwatisha watu bhana toka nakua kwetu mwambao wa ziwa kuelekea Kagunga sijawahi kusikia mtu kauawa au kufa kwa kuwekewa sumu ya mamba kwenye kahawa.Nasikia sumu ya nyongo ya mamba ni hatari ila huo utaratibu ndio mgeni kwangu maana toka Kalalangabo,mtanga na ngelwe yake,Kazinga,mwamgongo,Bugamba,Zashe kagunga mpaka kuelekea huko nchi jirani sijasikia historia hii labda huko kusini.

Cha msingi ni kujihadhari kabla ya hatari hakuna sumu tamu na wala hakuna muuaji asiyekujua.

"Proudly, brought to u by Bachelor Sugu"
Kweli, hayo maeneo hakuna Mambo hayo. Hata mtoa maada anasema, eti Kigoma mjini, mwanga, Ujiji? Mzushi tu. Huku Kuna ustaarabu bwana.
 
Back
Top Bottom