Nyuma ya mafanikio ya mwanaume kuna mwanamke lakini pia wanasahau kuigeuza hii kauli

Nyuma ya mafanikio ya mwanaume kuna mwanamke lakini pia wanasahau kuigeuza hii kauli

Hziyech22

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2019
Posts
15,351
Reaction score
21,362
Habari wanajf

Nina ndugu yangu wa kike aliolewa na jamaa mmoja hivi kutoka kabila la lile la wapenda sifa na wote wameingia kwenye ndoa wakiwa wote Wana hela lakini mwanaume ndio ana hela zaidi, kiukweli ndoa yao ilidumu ingawa kwenye ndoa hapakosi changamoto lakini ndugu yangu wa kike alisimama kidete kulinda ndoa na kiukweli waliofanikiwa Sana kimaisha zaidi.

Baada ya kupita muda mrefu ndugu yangu alifariki so akamuacha Mume wake alone.Baada ya kupita muda falani Jamaa ikabidi aoe mwanamke mpya na jamaa kweli akafanikiwa kuoa Mwanamke mzuri Sana kuliko hata mwanamke wake aliyofariki, huyo dada alikuwa full package ana sura yenye mvuto wa aina yake, kifuani yupo bomba bila kusahau shape yake ni so amazing ukimuangalia hivi lazima udenda ukutoke wakaishi kama miaka miwili hivi kwenye ndoa jamaa uchumi wake ukaanza kudrop Sana na mwanamke akamkibia ikiwa kavuna vitu vingi kwa jamaa, watoto wake aliyopata kwa mke wake aliyofariki aliwapeleka shule za Serikali kutoka shule za international ambapo alikuwa anawalipia 5M kwa mwezi wote watoto watatu, magari yake yote matatu Moja lilibebwa na huyo mke wake huyu mchungaji ambalo jamaa alimnunulia kama zawadi nakumuandikisha kwa jina lake magari yaliyobaki ikabidi auze baada ya maisha kuyumba

Jamaa alikuwa hajawahi kupanda daladala,bajaji wala bodaboda kwenye maisha yake yote ikabidi hizi ndio ziwe usafiri wake, Jamaa alikuwa ananunua vitu kwenye supermarket na kula kwenye migahawa mikubwa au hotelini baada ya anguko lake ukawa anakula kwenye migahawa ya kawaida ila jeuri yake ya pesa ikaisha kabisa.

Huyu mke wake alimnyonya ile mbaya nilibahatika kuona nae kiukweli utazani siyo kama yeye vile kakonda ile mbaya dah! Asikuambie kitu wanawake Wana nguvu Sana maana jamaa CV yake imeshiba ile mbaya ana elimu kubwa ana Masters na kasoma kwenye chuo kikubwa Sana Cha nje cambridge kazidiwa ujanja na mwanamke aliyeishia diploma kipindi anachopitia ni kigumu sana unajua kuna kuanguka lakini huyu Unaweza kusema kaporomoka nimekuwa nikijiuliza kwa uchumi aliyonayo imekuaje kaporomoka kwa kiasi hicho? Tunaweza tukamlaumu lakini atujui situation ilikuaje? Kwa uzuri wa yule mwanamke Unaweza ukaishia tu kukaa kimya.

Baada ya kukimbiwa na huyo mke wake ikaja kugundulika kumbe huyo manzi alikuwa nae ana watoto wa3 bila jamaa kujua na huyo manzi sasa hivi nasikia ana hela Sana kupitia kuchuma kwa mgongo wa jamaa.

NB: Ushauri wangu kwenu Wanaume ikiwemo na mimi uwe una hela au hauna weka hii akili mwako "sio kila mwanamke ni wa kila mwanaume" sisi Wanaume tuna ushamba fulani hiv mwanaume akiwa hana pesa anakuwa na discipline akiwa na pesa anakosa hii kitu nakuamini anaweza kumpata mwanamke yoyote na wengi wao wanaangalia sura, tako hii inakuhusu mzabzab maisha ni zaidi ya kuwa na hivyo Cha msingi tuwe Makini na aina ya mwanamke tunayeingia nae kwenye maisha
 
Huwa mnalogwa au ni nini kwa nini mwanaume unakua huna msimamo?
 
Kuna wanaume gundu pia
Sio gundu kama nilivyosema " sio kila mwanamke wa kila mwanaume" pia Hiyo Hiyo kauli inageuka " sio kila mwanaume wa kila mwanamke" huyo atakuwa ni mwanaume sio sahihi sio kwamba ana gundu
 
Unaweza kumlaumu lakini ningekuonesha mwanamke mwenyewe unaweza usihoji Hilo suala la yeye kuwa na msimamo
Tuma picha kaka, kwanzia hapo kifuani mpaka umbo na mbwembwe zingine sura si muhimu tutaweka imagination, tuone kama kweli baharia aliingia majaribuni
 
Tuma picha kaka, kwanzia hapo kifuani mpaka umbo na mbwembwe zingine sura si muhimu tutaweka imagination, tuone kama kweli baharia aliingia majaribuni
Shida ni Moja ninaweza kukuwekea alafu ikatumika vibaya ndio wasiwasi wangu upo hapa
 
Ila kukosa pesa ni fedheha sana mno jamani kwa sisi wanaume ndoa inaweza kuvunjika mda wowote
 
Back
Top Bottom