Nyumba ipi naweza kuikamilisha kwa 7M nikahamia kati ya hizi?

Nyumba ipi naweza kuikamilisha kwa 7M nikahamia kati ya hizi?

Habari wakuu?
Nimerudi tene kijana wenu niliechoshwa na sarakasi za wenyew nyumba na wapangaji wenzangu,
By the way naomba kujuzwa kati ya hizo RAMANI 2 nilizo'attach apa ni ipi naweza kuikamilisha kwa 7M nikahamia, ama siziwezi zote???
Thanks 🙏View attachment 2489657View attachment 2489661
Nyumba ya kwanza hujengwa kwa hatua, mil saba inaweza kukukufanya uhamie kwenye gofu , then utaendeleza ukiwa uko ndani
Kusema mil 7 ukamilishe kila kitu kwa ramani ulizotoa hapo ni uongo,
Dirisha tu la alluminium linakamilika kwa 300,000 hapo naona unayo matatu upande mmoja
 
Kwa hiyo bajeti na hilo lengo la kuhamia nakushauri ujenge ile ramani ya kwanza ila usijenge yote, ikate nusu kama inavyoonekeana kwenye picha niliyoambatanisha alafu unaacha matoleo utaendeleza kulingana na upatikanaji wa pesa kisha utamalizia na nyumba itakamilika
Shukran sana mkuu
 
Nyumba ya kwanza hujengwa kwa hatua, mil saba inaweza kukukufanya uhamie kwenye gofu , then utaendeleza ukiwa uko ndani
Kusema mil 7 ukamilishe kila kitu kwa ramani ulizotoa hapo ni uongo,
Dirisha tu la alluminium linakamilika kwa 300,000 hapo naona unayo matatu upande mmoja
Shukran mkuu, me lengo langu nipate jengo nipige plasta, niweke floor ya kawaida tu, niweke grill, Umeme na ikiwezekana nifunge gypsum board basi, je NITAWEZA???
 
Kwa hiyo bajeti na hilo lengo la kuhamia nakushauri ujenge ile ramani ya kwanza ila usijenge yote, ikate nusu kama inavyoonekeana kwenye picha niliyoambatanisha alafu unaacha matoleo utaendeleza kulingana na upatikanaji wa pesa kisha utamalizia na nyumba itakamilika
Huu ndio ushauri murua ukishupaza shinga utajutia
 
Haitoshi mkuu
Inategemea na eneo ulilopo
Ukibana saaana
Kwa haraka haraka kusimamisha boma
Msingi utakula mil. 2
Tofali ni kama 1800pcs=mil. 1.8
Cement mifuko 70pcs= mil. 1.4
Mbao na bati mil. 3
Na hapo bado sana make kuna
Slab
Brandaling za gypsum
Gypsum board
Plasta
Wearing ya maji na umeme
Vigae
Na vitu vingne vingi inategemea decoration zako unazotaka
 
Shukran mkuu, me lengo langu nipate jengo nipige plasta, niweke floor ya kawaida tu, niweke grill, Umeme na ikiwezekana nifunge gypsum board basi, je NITAWEZA???
hiyo pesa haiwezi tosha makorokoro yote hayo!
Kama lengo ni kukimbia kadhia za wenye nyumba jenga boma tu ikiwezekana hata room moja , grills ,umeme, floor plasta .nk utafanya ukiwa ndani kwako, kuna watu wanahamia hata choo hajachimba na maisha yanaendelea
 
Habari wakuu?
Nimerudi tene kijana wenu niliechoshwa na sarakasi za wenyew nyumba na wapangaji wenzangu,
By the way naomba kujuzwa kati ya hizo RAMANI 2 nilizo'attach apa ni ipi naweza kuikamilisha kwa 7M nikahamia, ama siziwezi zote???
Thanks 🙏View attachment 2489657View attachment 2489661
Una milioni saba na bado unafikiria ramani zenye choo na jiko??
 
Back
Top Bottom