Nyumba nyingi hutumia mlango wa jikoni kuingia ndani badala ya mlango wa sebuleni, ni uchawi au ni nini?

Nyumba nyingi hutumia mlango wa jikoni kuingia ndani badala ya mlango wa sebuleni, ni uchawi au ni nini?

Vijijini iko sana iyo,
Mama zetu hawakupenda tupite pite ovyo seblen kuchafua.

Seblen Ni kwa ajili ya wageni
 
Inategemea jinsi nyumba ilivyo jiposition. Nyumba nyingi upande wa jikoni ndio kuna space na shughuli nyingi hufanyikia huko ikiwemo za kiusafi. Kwa sababu ya shughuli nyingi kufanyika huko ndio maana mlango huo unakuwa wazi muda wote. Ndio maana anapokuja mgeni wa aina yeyote inabidi umfungulie mlango wa mbele. Kama hukufunguliwa mlango wa mbele basi mwenyeji wako alikuchukulia kama mwenyeji
Kama mgeni amekuja na anasikia kabisa kuna watu wanaongea huko nyuma hawezi jisumbua kugonga mlango wa mbele badala yake atazungukia jikoni.

Hii nyumba ninayoishi funguo za mlango wa mbele zimepoteaga kitambo sana.
 
Mazoea mabaya ata kugegedana wengi wanatumia mlango wa uani
 
Kwa hapa mjini mara nyingi, ni issue ya kiusalama zaidi, maana nyimba nyingi sebule huwa mbele kabisa kama ukiingia getini, kwakuwa nyumba nyingi shughuli za kila siku hufanyika nyuma ya nyumba kama kupika, kuosha vyombo, kufua nk halihuoelekea upande wa mbele kuwa kumefungwa muda mwingi.

Kutokana na maisha tunayoishi mara nyingi binti wa kazi ndiyo anashinda nyumbani, hivyo inakuwa ngimu kufungua mlango wa mbele mara kwa mara ukizingati mlango wa mbele huwa na sekurity kubwa zaidi ku access kwani utahitaji kufungua mlango wa grill then mlango wa kawaida, hilo zoezi ni gumu sana, hivyo hata members wa familia wakirudi huona ni rahisi kupitia mlango wa nyuma ambao huwa wazi muda mwingi kuliko wa mbele.
 
comments za kimaskini mm kwangu naingia kwa kupanda lift up....jiko liko mbali na sebule kbsaa iz ni hadith mpya kwangu
 
Urithi wa kikoloni. Watu weusi hasa watumishi wa ndani kwa wazungu huko ulaya hawakuruhusiwa kupitia mlango mkubwa bali wa jikoni. Mkubwa ulikuwa ni wa wazungu pekee. Inaanzia hapo
Siyo wazungu wote walipitia mlango wa mbele. Kama umesoma vitabu vya zamani, utakuta manager wa shamba ni mzungu naye alipitia nyuma. Niwale wenye hadhi ya mwenye nyumba na zaidi ndo walifunguliwa mlango Butler.
Nasisi unakuta watu wameshazoea. Mlango wa mbele ni kwa wakwe na watu wenye hadhi kama mapadre au watu wa aina hiyo.
Tukubaliane kutokubaliana.
 
Kuna nyumba nyingi sana nilizowahi kutembelea, unakuta unakaribishwa ndani kwa kupitia mlango wa jikoni, na ule wa sebuleni unakuta haujawahi kutumika tangu nyumba ijengwe.

Hii husababishwa na nini, chanzo au lengo la tabia hii, ni nini?
Ni akili yako tu ndogo , maana nyumba nyingi za ughaibuni unaingilia jikoni pia, sitting room inatizama garden kwa nyuma. Anyway, Miafrika ndivyo ilivyo....
 
Kuna nyumba nyingi sana nilizowahi kutembelea, unakuta unakaribishwa ndani kwa kupitia mlango wa jikoni, na ule wa sebuleni unakuta haujawahi kutumika tangu nyumba ijengwe.

Hii husababishwa na nini, chanzo au lengo la tabia hii, ni nini?
Hahahahaha mazoeaa tuuuu,ht kwangu tunatumia mlango wa jikoni saanaaa,ila sababu ya kutotumia wa mbele ni unatizamana na geti kubwa la nje sasa ukiwa unafunguliwa mara kwa mara ni rahisi mtu kuingiaa kule mbele bila mtu wa uku uwani kujuaa na mara zote wanaobaki home wanakua wanafanya shughuli za home nyumaa/uwani
 
Kuna nyumba nyingi sana nilizowahi kutembelea, unakuta unakaribishwa ndani kwa kupitia mlango wa jikoni, na ule wa sebuleni unakuta haujawahi kutumika tangu nyumba ijengwe.

Hii husababishwa na nini, chanzo au lengo la tabia hii, ni nini?
Kuzuia uchafu wa viatu kuingia sebuleni. Na kuna nchi wanaigeuza nyumba . Ukiingia getini ni,nyuma ya nyumba, kwahiyo watu wanaingilia garage
 
Hii staili binafsi siipendi kabisa,mimi naamini jikoni ni sehemu nyeti mno,sababu huko ndiko chakula kinapoandaliwa na chakula ni usafi na unyeti lakini ni moja kati ya siri za familia kama yalivyo mambo ya chumbani,binafsi kwangu huwa sipendi mtu asiyehusika na familia kusogea jikoni kwahyo kwangu unatumika mlango wa mbele kwa shughuri za wageni na jikoni panabaki na falagha na utulivu wake sio watu wakatizekatize huko,kwanza kama mna housegirl au mama mwenye nyumba ambae si msafi sana hao wageni unaowapitisha jikoni wakiona wanaweza kukataa kula chakula chako.
 
Hii staili binafsi siipendi kabisa,mimi naamini jikoni ni sehemu nyeti mno,sababu huko ndiko chakula kinapoandaliwa na chakula ni usafi na unyeti lakini ni moja kati ya siri za familia kama yalivyo mambo ya chumbani,binafsi kwangu huwa sipendi mtu asiyehusika na familia kusogea jikoni kwahyo kwangu unatumika mlango wa mbele kwa shughuri za wageni na jikoni panabaki na falagha na utulivu wake sio watu wakatizekatize huko,kwanza kama mna housegirl au mama mwenye nyumba ambae si msafi sana hao wageni unaowapitisha jikoni wakiona wanaweza kukataa kula chakula chako.
Naunga mkono hoja yako[emoji122][emoji122]
 
Mkuu kwel hata mimi natumia mlango wa jikoni sijui shida ni nini lakin kuna wakat nakasirika kuzunguka kufuata kitu ndan wakati ningepita chap kwa haraka mlango wa mbele
Shughuli nyingi hufanyika nyuma ya nyumba, eg bustani, ufugaji nk. Hodi nyingi huwakuta wenyeji wako nyuma ya nyumba, mlango wa mbele ukiwa umefungwwa kwa usalama. Binafsi funguo za mpango wa mbele hazitumiki na kitasa kime-jam!
 
Back
Top Bottom