Nyumba ya Dudley Mbowe kupigwa mnada kwa kushindwa kulipa Sh milioni 62.7 za waandishi

Nyumba ya Dudley Mbowe kupigwa mnada kwa kushindwa kulipa Sh milioni 62.7 za waandishi

Kama mikupuo ilikua mitatu na mkupuo wa mwisho ni tarehe 30 February maana yake bado muda haujaisha, Dudley alipewa zote kwa mkupuo tarehe 30 February.
Februari tokea lini ikawa na tarehe 30?Hivi shule mlijifunza ujinga.Na bado kuna wavimba macho wanaunga mkono.
 
Mmmh

Hamna kitu kitachopigwa mnada hapo, dalali Esther Massawe, mdaiwa Dudley Mbowe.... Haya tusubirie
 
GGSebRBWMAAt5l4.jpg
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi imetoa amri na kumteua dalali wa kukamata nyumba ya mtoto wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Dudley Mbowe na kuipiga mnada kwa kushindwa kulipa Sh milioni 62.7 za waandishi wa habari. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Uamuzi huo wa mahakama umetolewa leo tarehe 14 Februari 2024 mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Mary Mrio baada ya kupitia hoja za washinda tuzo katika Tume la Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Julai 2023.

Shauri hilo namba 28461 la mwaka 2023, wadai Maregesi Paul na wenzake tisa dhidi ya Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe.

Akiwasilisha hoja mahakamani, Maregesi alidai Mkurugenzi Dudley baada ya wadai kushinda shauri alikubali kulipa lakini baadaye hakutekeleza makubaliano.

"Amekaidi kutulipa tumeona njia sahihi tumekubaliana tukamate nyumba yake namba 9 iliyopo Mtaa wa Feza , Mikocheni B barabara ya Chipaka,"alidai Maregesi.

Akitoa uamuzi huo Naibu Msajili Mrio, alisema mahakama inatoa amri ya kukamata nyumba namba tisa, iliyopo Mtaa wa Feza, Mikocheni B.

"Mahakama inatoa amri ya kukamata nyumba na imemteua Dalali wa Mahakama, Jesca Massawe kutoka Kampuni ya Udalali ya MM Auctioneer &Debt Collectors,"alisema.

Baada ya uamuzi huo, mahakama iliahirisha shauri na kulipanga tarehe 4 Machi mwaka huu kwa ajili ya kupata taarifa ya utekelezaji wa amri hiyo

Walalamikaji hao walipata tuzo tarehe 17 Julai mwaka 2023 mbele ya Mwenyekiti wa CMA, Bonasia Mollel.

Madai ya awali yalikuwa jumla ya Sh milioni 114 baada ya kukaa mezani kwenye majadiliano kwa pamoja kiwango hicho cha fedha kilishuka na kufikia Sh milioni 62.7.

Dudley alikubali kulipa fedha hizo kwa awamu tatu, tarehe 30 Oktoba, tarehe 30 Desemba mwaka 2023 na awamu ya mwisho ilikuwa tarehe 30 Februari mwaka huu lakini hakulipa.

Chanzo: Mwanahalisi
 
Watoto wa Mbowe sio raia, ni Raia wa Marekani na Uingereza kwa nini wanaruhusiwa kumiliki ardhi Tanzania? Hiyo nyumba itaifishwe
Maskini kuwachukia matajili haiwafanyi maskini kuwa matajili!acheni chili za kipumbavu
 
mbowe.png

Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi imeamuru kukamatwa na kupigwa mnada nyumba ya mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe iliyoko Mikocheni, ili kulipa deni la Sh62.7 milioni anazodaiwa na waliokuwa waandishi na wahariri wa gazeti hilo.

Sambamba na amri hiyo iliyotolewa na Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Mary Mrio, pia imemteua dalali wa kutekeleza amri hiyo, Jesca Massawe kutoka kampuni ya udalali ya MM Auctioneer & Debt Collectors.

Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo kufuatia maombi yaliyowasilishwa na waandishi hao, Maregesi Paul na wenzake tisa ili kutekeleza tuzo yao waliyopewa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), katika shauri la mgogoro wa kikazi walilolifungua dhidi ya mwajiri wao huyo.

Akizungumza na Mwananchi, Paul amesema wakati amri hiyo inatolewa, Dudley ambaye ni mtoto wa Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chadema, hakuwepo mahakamani licha ya kwamba alikuwa ameahidi kuwa angefika na fedha za kuwalipa.
 
Mbowe hajafanya poa. Kwenye ruzuku ya 2.7b alishindwa kuchomoa 62m na kulipa waandishi? Huyu ni kiongozi mbinafsi anayejijali peke yake na familia yake. Halafu kumbe Tanzania Daima ni mali yake binafsi na sio CHADEMA? Hakika huyu ni mjasiriamali na nyumbu ni mtaji wake.
 
Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi imeamuru kukamatwa na kupigwa mnada nyumba ya mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe iliyoko Mikocheni, ili kulipa deni la Sh62.7 milioni anazodaiwa na waliokuwa waandishi na wahariri wa gazeti hilo.

Sambamba na amri hiyo iliyotolewa na Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Mary Mrio, pia imemteua dalali wa kutekeleza amri hiyo, Jesca Massawe kutoka kampuni ya udalali ya MM Auctioneer & Debt Collectors.

Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo kufuatia maombi yaliyowasilishwa na waandishi hao, Maregesi Paul na wenzake tisa ili kutekeleza tuzo yao waliyopewa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), katika shauri la mgogoro wa kikazi walilolifungua dhidi ya mwajiri wao huyo.

Akizungumza na Mwananchi, Paul amesema wakati amri hiyo inatolewa, Dudley ambaye ni mtoto wa Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chadema, hakuwepo mahakamani licha ya kwamba alikuwa ameahidi kuwa angefika na fedha za kuwalipa.
ugali moto
mchuzi moto
 
Mbowe hajafanya poa. Kwenye ruzuku ya 2.7b alishindwa kuchomoa 62m na kulipa waandishi? Huyu ni kiongozi mbinafsi anyejijali peke yake na familia yake. Halafu kumbe Tanzania Daima ni mali yake binafsi na sio CHADEMA? Hakika huyu ni mjasiriamali na nyumbu ni mtaji wake.

Akifanya hivyo mnakuja kumnanga tena anatumia ruzuku kwa manufaa yake, binadamu hamueleweki
 
Mbowe hajafanya poa. Kwenye ruzuku ya 2.7b alishindwa kuchomoa 62m na kulipa waandishi? Huyu ni kiongozi mbinafsi anyejijali peke yake na familia yake. Halafu kumbe Tanzania Daima ni mali yake binafsi na sio CHADEMA? Hakika huyu ni mjasiriamali na nyumbu ni mtaji wake.
Wanafanya maigizo ili kuonesha kuwa Mbowe haibi ruzuku. Mlalamikiwa hakwendà mahakamani makusudi. Hao wadai watalipwa kimyakimya.
 
Back
Top Bottom