Tetesi: Nyumba ya mjane wa Balozi John Rupia Katibu Mkuu Kiongozi (mstaafu) yadaiwa kupigwa mnada

Tetesi: Nyumba ya mjane wa Balozi John Rupia Katibu Mkuu Kiongozi (mstaafu) yadaiwa kupigwa mnada

Hata kichwani ukiwa zero brain, kama baba amefanya the right investment kwenye properties, shares, stocks and bonds, watoto wanakula tuu dividends na kuishi maisha mazuri for the rest of their lives.

Hata hiyo nyumba inayouzwa, inauzwa tuu kwasababu something went wrong somewhere, it was earmarked for a huge investment kwasababu nyumba za kuishi wanazo plenty tena prime areas lakini Balozi alikubali kuishi hapo kwenye a humble house for a reason!, nalijua jumba lao la masaki, ni usipime!.

Hii taarifa ni marketing tricks kuufanya mnada wa hiyo nyumba kugeuka an article of ostentation hivyo to fetch a very high price!. Mtu kama the King Maker anaweza kutia team ili kununua nyumba ya Rupia, kama ule mnada wa mahekalu ya Lugumi yaliyo minus Dr. Shika!, mwisho wa siku ni Lugumi kazinunua mwenyewe nyumba zake na sasa anaendelea kuishi mwenyewe!.
P

King maker atakuwa hajaiona kweli hii, ngoja nimtumie what's up, alafu sijui atasoma labda kesho maana gas business inachanganya sana, King maker akiona hii lazima anunue au yule jamaa Fida Hussein mwenye properties zote hizo nyingi masaki, plus Zahra & Raha Towers mjini pale, Fida akiona hii anachukua mara moja.
 
Mkuu peno hasegawa, asante kwa taarifa hii.

Nyumba yoyote inapopigwa mnada maana yake ni imetumika kama collateral for loan.

Kama nyumba hiyo ni matrimonial home, haikubaliki as a collateral mpaka both spouses wasaini.

Mke kama ulisaini nyumba itumike as collateral, mume akachukulia mkopo, baadae mume akafa bila kuulipa huo mkopo, kifo cha mume hakifuti lile deni la ule mkopo, hivyo mkopo lazima ulipwe!. Ukishindwa kulipa, ujane sio an excuse kuizuia bank to recover its debts.

Huu ni mfano mzuri wa kuwafundisha Watanzania kuweka bima, kuna mpaka bima za mikopo, ukifa kabla hujamaliza kulipa mkopo, bima ina take over na kukulipia!.

Rupia ni among the top ten giant families zenye lots of properties jijini Dar es Salaam!. Yale maghorofa yote matatu pale Uhuru Roundabout ni ya baba yao Mzee John Rupia, ambapo wakati wa utaifishaji hayo hayakuguswa!.

Hivyo hilo la hii nyumba ni dogo tuu!.
Pole Mama Anna, hili ni dogo tuu kama upepo na litapita tuu!.
P
HV lini Ezekiel Kamwaga utakuwa na akili unakuja kuwatetea watu walijimilikisha kupita Kia's eti mjane anaishi mle ndani ,siyo sawa hili Kama wamekopa walipe tu hkn jins vinginevyo itauzwa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hata kama angekuwa mjane wa balozi, ndiyo akope hela za benki asilipe halafu atazamwe tu,?

Bado mjane wa rais fulani namsubiria ajichanganye.

Dawa ya deni ni kulipa. Mleta mada vipi wewe!??

Kwahiyo ulitaka Hawa wajane wa viongozi wasilipe madeni??
Tumshangaee huyo kamwags

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
KIFO CHA BALOZI PAUL RUPIA: DAR ES SALAAM TUMEFIWA

Sidhani kama kuna mtu ana ujasiri wa kunyanyua kalamu yake pale Abdallah Tambaza atakapoandika historia yoyote inayuhusu Dar es Salaam iwe matukio au iwe taazia.

Naitazama taazia ya Balozi Paul Rupia baada ya kumaliza kuisoma na kuna kitu kinachogonga kichwani kwangu kama vile kuniuliza, ''Hivi kweli huna lolote la kusema kuhusu Balozi Paul Rupia?''

Najijibu mwenyewe, ''Vipi nitakosa la kusema kuhusu Balozi Rupia ilhali nimemfahamu kwa miaka mingi na kwa mbali ni jamaa yangu kwa nasaba ingawa ya mbali kwangu binafsi?''

Haya nitakayosema hapa huenda yakawashtua na kuwashangaza wengi.
Ishatokea hivi mara nyingi.

Udugu wetu na ukoo wa Rupia unatoka mbali sana kutoka kwa bibi yetu mkuu Bi Christina mama ya bibi yetu Bi. Deborah Mgone (1890 - 1995).

Bibi zetu hawa ndiyo waliotuunganisha na ukoo wa Rupia.
Sisi leo ni kizazi cha nne kutoka kwa bibi yetu mkuu Bi. Christina.

Hapa unazungumzia historia inakaribia miaka 200.

Kama walivyo akina Rupia kuwa wana nyumba Misheni Kota nasi pia tuna nyumba mbili Misheni Kota hadi leo.

Nyumba nyingine tatu ziko Mtaa wa Swahili moja, Sikukuu zilikuwa mbili sasa imebaki moja.

Moja bibi aliuza.
Hii ilikuwa jirani sana na Saigon Club.

Nyumba hizi tumezaliwa tumezikuta.
Hatujui lini zilijengwa.

Naamini hizi nyumba sasa zina umri zaidi ya miaka 100.

Nyumba hizi zinatukumbusha utoto wetu na kututafsiria mengi katika maisha yetu.

Bi. Christina na Bi. Deborah niliowataja hapo juu hawa wote mimi nimewaona kwa macho yangu na wameondoka duniani mimi nina fahamu zangu kamili.

Na katika dada zetu alikuwapo Christiana kapewa jina la bibi yetu mkuu maarufu tukimwita ''K'' (apumzike kwa amani).

''K'' alikuwa mkubwa kidogo kwangu na alinipokea St. Joseph's Convent School 1967 na yeye alipokewa hapo na kaka yetu Charles Mgone 1965 au 1966.

Ndani ya historia hii vipi nikose la kusema kuhusu Balozi Paul Rupia na ukoo wa Rupia wenyewe na historia ya wazee wetu waliokuwapo wakati sisi tunazaliwa na kaka zetu tuliowakuta mfano wa marehemu Albano, Balozi Rupia na Steven maarufu kwa jina la Mpuya?

Hawa walikuwa watu maarufu bila ya hata kujikwaza.

Nimehudhuria shughuli nyingi na Albano akiwepo lakini huwezi kusikia sauti yake.

Yeye siku zote alikuwa mtu wa kusikiliza.
Mzee Albano alikuwa mtu wa maneno machache mno.

Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes nilikutana na barua iliyoandikwa na Makata Mwinyimtwana anamwandikia Ally Sykes kuhusu mwanae Makata ambae alikuwa anakwenda kusoma Liberia pamoja na Paul Rupia kwa scholarship ya TANU.

Barua hii nasikitika sana leo kuwa sikuitia maanani asilani.
Nimeisoma nikapita.

Ninachokumbuka ni kuwa Mzee Makata Mwinyimtwana alikuwa anatafuta ushauri kutoka kwa Ally Sykes kuhusu hali ya baadae ya vijana hawa waliokuwa wanakwenda nje kupata elimu ya juu.

Katika msafara huu wa kwenda Liberia alikuwako Ngombale Mwiru.

Huyu Makata Mwinyimtwana kama alivyokuwa John Rupia alikuwa Mwafrika tajiri sana Tanga.

Inafahamika na wengi kuwa Balozi Rupia hakuwa anapenda kueleza si historia yake wala ya baba yake.

Naamini kabisa kama angenyanyua kalamu kuandika kumbukumbu zake hakuna wasiwasi kuwa historia ya baba yake ingefahamika na mengi ambayo leo yanababaisha watu yangekuwa hadhir.

Naikumbuka Misheni Kota ya 1960s na kilichokuwa kinanipeleka ni kuwa hii ilikuwa miaka ya ''Soul Music'' - James Brown, Aretha Franklin, Ottis Redding, Wilson Pickett, Sam and Dave halikadhalika Erick Burdon and The Animals, Mick Jagger and The Rolling Stones, The Beatles nk.

Muziki wa Wamarekani Weusi na Misheni Kota kulikuwa na vijana wapigaji muziki huu katika bendi maarufu za vijana Sparks na The Rifters - akina Sauti Plantan, Lameck Nicodemus Ubwe na wadogo zake Jacob na Esau.

Nikishinda Misheni Kota siku za likizo - ''jam sessions.''

Nikifika hadi nyumbani kwa Mzee Rupia kwa hili au lile na naikumbuka sana ile mikungu iliyokuwa pale nje.

Lakini sikuwa naijua historia ya nyumba ile kuwa ndipo mkutano wa kuunda African Association ulipofanyika mwaka wa 1929 na wakati ule nyumba ile ilikuwa ya Cecil Matola John Rupia akaja kuinunua baadae.

Haya nilikuja kuyajua baada ya kumsoma Daisy Sykes katika kitabu alichohariri John Iliffe.

Nilipokuwa mazikoni tena niko na Abdallah Tambaza nimemuona Ayoub Sykes na dada zake Guru na Miski, Said Mpango na dada yetu Bi. Baya kutoka Msasani wamekuja mazikoni wamebaba maua wamekuja kumzika kaka yao mkubwa Balozi Rupia.

Babu yao Kleist Sykes alikuwa rafiki mkubwa wa John Rupia ndani na nje ya siasa za African Association na barza yao kubwa ilikuwa nyumbani kwa Keist Mtaa wa Stanley na Sikukuu jirani na nyumba ya bibi yangu Bi. Deborah na jirani ya nyumba ya Mzee Maleta na Mzee Kubbe.

Sasa miaka 73 imepita baada ya kifo cha Kleist na kuvunjika kwa ile barza.
Wajukuu ni sisi na tumeihifadhi historia hii ndani ya vifua vyetu.

Paul Rupia kwangu alikuwa ni kaka mkubwa wala sina maingiliano yoyote na yeye.

Wala sikuwa najua kuwa kuna ujamaa baina yetu.
Haya nilikuja kuyafahamu baadae sana.

Mimi na wenzangu Paul Rupia alikuwa ni kaka tu kama walivyokuwa kaka zetu wengine wa Misheni Kota kama Kurwa na Doto Plantan, Malombe, Denis Nicodemus Ubwe kwa kuwataja wachache, wakati ule anasoma Chuo Kikuu Cha Nairobi.

Dar es Salaam tumefiwa.
Balozi Paul Rupia ni sehemu ya historia ya Dar es Salaam.

Tumefiwa na mtu ambae kaona yote kwa macho yake na kaishi maisha ya nyakati zile na kwa hakika alikuwa hazina kwetu lau kama alikuwa kimya katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ingawa baba yake alikuwa mmoja kati ya waasisi wa TANU na wafadhili wakubwa Balozi hakupenda kueleza haya.

Balozi Rupia yeye kwa ile tabia na hulka yake ya unyofu hakupenda kueleza historia ya Rupia katika kupigania uhuru wa Tanganyika na kuwa baba yake alikuwa mmoja wa nguzo kuu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kaka yetu Balozi Rupia huyu hakutukataza kuandika historia hii yetu kwa faida ya vizazi vijazo ingawa yeye mwenyewe maisha yake yote alikuwa kimya.

Balozi Paul Rupia katuachia funzo.

Kaka yetu Paul Rupia ni hadithi nzuri ya kuhadithiwa, chembelecho Rais Ali Hassan Mwinyi.

PICHA:
Picha hizo hapo chini nimempiga Balozi Paul Rupia akiwa na mkewe Bi Rose Desta na kaka yangu Charles Mgone akiwa na mkewe Bi. Joyce Bakuname siku ya harusi ya mwanetu Harold.

Picha hiyo ya chini wa kwanza kulia ni shangazi yetu Bi. Flora Mgone.
308750308_1265103534237022_2390742274289806053_n.jpg

308511406_1265095497571159_6240557770778962666_n.jpg
Nilikuwa nakusubiri Sasa unekuja Asante mzee wacha nisome sasa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hizi ni 1st class families, hawahitaji kufanya biashara zozote, au kumiliki viwanda, just prime properties, shares, stocks and bonds.
P
First class family zipi hazifanyi biadhara,kenyatta mpk leo wana maviwanda
Hizi familia zenu zinaishi kwa kubweteka kisa majina ya baba zao
Wao wanatafuna tu walichotafuta wazazi wao badala kuongeza
Umeona familia nyingi za vigogo zklivyo porongoka...
Hebu jifunzeni kuhusu " generation wealth "kama wenzenu wadosi ,waarabu
Rosamund aziz ni bolionea lkn watoto,ndg zake wanatafuta ubilionea wao ,hawana time na pesa za mzee wao
First class families zako nyingi unakuta ziko kwenye migogoro ya Mali kifamilia tu
Kila mtu angekuwa anatafuta ungekuta mambo kama hayo yasingetokea,hakuna mtu anayeweza kuachia nyumba obay kiboya boya
Ukiona hivyo ujue hali si shwari kifedha,aise paskali msalimie B.MApalala

Ova
 
Hata kichwani ukiwa zero brain, kama baba amefanya the right investment kwenye properties, shares, stocks and bonds, watoto wanakula tuu dividends na kuishi maisha mazuri for the rest of their lives.

Hata hiyo nyumba inayouzwa, inauzwa tuu kwasababu something went wrong somewhere, it was earmarked for a huge investment kwasababu nyumba za kuishi wanazo plenty tena prime areas lakini Balozi alikubali kuishi hapo kwenye a humble house for a reason!, nalijua jumba lao la masaki, ni usipime!.
P
Hata hiyo nyumba wainywa tu

Iliuzwa nyumba ya mkono masaki

Nayo ilikuwa usipime,na iliuzwa

Ova
 
Sasa nani alimwambia akakope kwa kutumia hiyo nyumba na pesa za mkopo kapeleka wapi? Tuanze hapo kwanza

Watu wafanye makosa halafu waanze kutafuta huruma

Apambane hana watoto, hana ndugu pesa alikula na nani?
Halafu kwani yeye atakuwa mjane wa kwanza kupigiwa mnada nyumba yake na benki? Kwann ionekane kwa huyu mama ndiyo very special? Hawa viongozi tunawadekeza sana, ndiyo maana wanajiona wako juu ya sheria.
 
King maker akiona hii lazima anunue au yule jamaa Fida Hussein mwenye properties zote hizo nyingi masaki, plus Zahra & Raha Towers mjini pale, Fida akiona hii anachukua mara moja.
Umesahau kunitaja na mm Sexless mwenye baa na madangulo kila kona ya jiji. Nina ukwasi wa kufa mtu
 
Mkuu peno hasegawa, asante kwa taarifa hii.

Nyumba yoyote inapopigwa mnada maana yake ni imetumika kama collateral for loan.

Kama nyumba hiyo ni matrimonial home, haikubaliki as a collateral mpaka both spouses wasaini.

Mke kama ulisaini nyumba itumike as collateral, mume akachukulia mkopo, baadae mume akafa bila kuulipa huo mkopo, kifo cha mume hakifuti lile deni la ule mkopo, hivyo mkopo lazima ulipwe!. Ukishindwa kulipa, ujane sio an excuse kuizuia bank to recover its debts.

Huu ni mfano mzuri wa kuwafundisha Watanzania kuweka bima, kuna mpaka bima za mikopo, ukifa kabla hujamaliza kulipa mkopo, bima ina take over na kukulipia!.

Rupia ni among the top ten giant families zenye lots of properties jijini Dar es Salaam!. Yale maghorofa yote matatu pale Uhuru Roundabout ni ya baba yao Mzee John Rupia, ambapo wakati wa utaifishaji hayo hayakuguswa!.

Hivyo hilo la hii nyumba ni dogo tuu!.
Pole Mama Anna, hili ni dogo tuu kama upepo na litapita tuu!.
P
Babao alikuwa na watoto wangapi ukiondoa John Rupia?
 
Back
Top Bottom