Pre GE2025 Nzega, Tabora: Mtaani kwetu kuna watu wanapita Kila kaya wanagawa mitungi ya gesi, Sharti lao uwape namba yako ya NIDA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kila lenye mwanzo halikosi mwisho tusubiri
 
Sio rushwa sema ni muwekezaji mpya wa Gesi anagawa mitungi ili wapate wateja wa Gesi Wengi makoto utakutana nayo katika gesi
 
Hapo sawa kama wanakataana wao kwa wao sawa
Ushahidi wa hili ni ule uhuni uliofanyika majuzi kule Dodoma,ile ni hofu ya kukataliwa kama ungefuatwa utamaduni waliojiwekea wenyewe,sasa kuepuka hilo ndiyo wakafanya shambulizi la kushitukiza,lakini wanaccm hawajaridhika na kilichofanyika,hivyo hilo halijaisha mpaka liishe. Hadi anawakodi mashekhe wamletee majini siyo mchezo.
 
Sio rushwa sema ni muwekezaji mpya wa Gesi anagawa mitungi ili wapate wateja wa Gesi Wengi makoto utakutana nayo katika gesi
Na namba za nida za kazi gan boss
 
We leteni na uku bwana, najua ata nikiwapa wapinzani wataiba tuu, leteni mitungi yangu
 
Ndio kama wanania njema kweli wafanye 15 badala ya 25 wanayotuuzia... Halafu waende kwenye petrol/diesel wafanye 2000 badala ya 2900 uone maisha kama hayabadiliki na bei za nauli zinashuka
Hayo uliyosema ndiyo ya maana wakazingatia watathaminika ,
 
Endeleeni kukopa mitungi ya gas kwa 500K kwa miaka miwili. Usiseme ulikuwa hujui wakati umekubali mpaka ukatoa namba ya NIDA.
 
We leteni na uku bwana, najua ata nikiwapa wapinzani wataiba tuu, leteni mitungi yangu
Unabariki uchafu wao boss na ndio huo unaotuathiri kwenye maisha yetu ya Kila siku
 
Kwahio namba ya NIDA ya mtu ndio Upigaji Kura wake ?!!! Kama vipi waje kwangu niwape Namba za Nida kama Zote; ila wasinipe Mitungi ya Gesi bali wawaambie watunge Sera wabadilishe / wahakikishe Umeme unazidi kupungua Bei...
 
Wewe na wao ni wale wale unachokitetea unakijua
 
acha uzushi wa kipuuzi, namba ya NIDA ina biashara gani mpaka inunuliwe? Kukosa maarifa ni janga
 
Chukua mtungi kura n siri, kwani MBOWE amefanywaje na pesa zake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…