Ofisa wa TRC aliyefukuzwa kazi kwa kukosoa tozo akamatwa na Jeshi la Polisi akiwa nyumbani kwake

Taarifa zilizotufikia hivi punde Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limemkamata Ofisa wa TRC aliyefukuzwa kwa kukosoa tozo, Jonas Afumwisye akiwa nyumbani kwake.

Wakili wake Peter Kibatala akizungumza na MwanaHALISI kwa njia ya simu amesema Afumwisye amempigia simu na kumweleza kuwa Polisi wamemfuata nyumbani kwake na kuondoka naye kuelekea Central Polisi.

My Take: #KataaWahuni
 
Safi sana, wakati mwingine lazima heshima iwepo mjini
 
Kwa serikali hii ya chawasynthesis lazma muhuni atakomeshwa! Kwanza kavujisha barua aliotwangwa na boss.

Hio situation ya hivyo ilinikutaga staki kukumbuka nilipigwa disclipinary comittee round 2 nikapangua accusations ila mwisho walitumia ubabe tu sababu VC alitaka nikomeshwe.
 
Wameshajigeuza kuwa miungu wa duniani! Ila kwa bahati mbaya mwisho wa siku wote tunaenda ardhini.

Watawatesa, watawatisha, na kuwaua binadamu wenzao! Na wenyewe siku yao ikifika, watalala kaburini.
 
Taarifa zilizotufikia hivi punde Jeshi la Polisi Dar es Salaam limemkamata Ofisa wa TRC aliyefukuzwa kwa kukosoa tozo, Jonas Afumwisye akiwa nyumbani kwake. Wakili wake Peter Kibatala amesema Afumwisye amempigia simu na kumweleza kuwa Polisi wamemfuata na kuelekea Central Polisi.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…