Hao mbona ndivyo walivyo hadi maofisini kwao. Yaani hii sura waliyoionyesha hapa ndiyo sura yao halisi kabisa hata ukiwakuta ofisini kwao. Wao na ofisi ya Utumishi (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) kitabia ni mtu na pacha wake.Hawa waliofungua uzi halafu hawa replay hii inaonesha jinsi wananchi wanavoteseka bila kero kushughulikiwa katika maisha halisi ya mtanzania
Sizingui mkuu niko serious tangu mwanzoni niliwambia hao jamaa hawawezi kuendesha hii page.Acha kuzingua... Waanzisja Uzi wameukimbia. Waliufungua ili iweje!?
Poleni,changamoto zinazohusiana na uhamisho uliza utajibiwa hapa,na nina uhakika na majibu nnayo kupaHawa waliofungua uzi halafu hawa replay hii inaonesha jinsi wananchi wanavoteseka bila kero kushughulikiwa katika maisha halisi ya mtanzania
Ivi mnayatatua vipi matatizo ya MaDED kuwadhulumu wazabuni waliotoa huduma kwenye halmashauri hasa katika kipindi ambacho hao maDED hawakuwepo?Ndugu wana JamiiForums,
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), kupitia thread hii, tutapokea Maoni, Ushauri, Malalamiko, Mapendekezo yako Mwananchi. Tunakuhakikishia kuchukua hatua stahiki kwa haraka zaidi kwa kile utakachokiwasilisha kwetu.
Ikumbukwe kuwa tangu Mwaka 1961 hadi sasa Ofisi ya Rais –TAMISEMI imekuwa ni Wizara inayojitegemea na madhumuni ya kuwepo kwa Serikali za Mitaa ni kupeleka Madaraka kwa Wananchi ambapo chimbuko lake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Sura ya 8, Ibara ya 145 na 146.
Hadi sasa Nchi ina Mikoa 26, Wilaya 139, Halmashauri 184, Tarafa 570, Kata 3,956, Vijiji 12,319, Vitongoji 64,361 pamoja na Mitaa 4,263.
Majukumu ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI
yanatekelezwa katika ngazi ya Makao Makuu, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuzingatia Hati ya Rais ya Mgawanyo wa Majukumu (Presidential Instrument) iliyotolewa na Rais Mei 2021, majukumu ya OR-TAMISEMI ni pamoja na:-
i) Kuratibu utekelezaji wa Sera ya Maendeleo Mijini na Vijijini na Upelekaji wa Madaraka kwa Umma (D by D);
ii) Kuratibu huduma mijini kama vile usafirishaji, maji na usafi wa mazingira;
iii) Kusimamia Tume ya Utumishi wa Walimu;
iv) Kuratibu na Kusimamia Tawala za Mikoa ili ziweze kuziwezesha Halmashauri kutekeleza wajibu wake;
v) Kuratibu Usimamizi na Uendeshaji wa Shule za Msingi na Sekondari nchini kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM);
vi) kusimamia na kuratibu shughuli za utolewaji wa huduma za Afya ya Msingi, Ustawi wa Jamii na Lishe
vii) Kuratibu na kusimamia mifumo na miundombinu ya TEHAMA katika Ofisi za Wakuu wa Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi
viii) Kujenga uwezo wa watumishi wa OR-TAMISEMI ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi
ix) Kuratibu shughuli za wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo
x) Kusimamia utendaji wa Mashirika, Taasisi, Programu na miradi iliyo chini ya OR-TAMISEMI
Kupitia JamiiForums.com unaweza kuwasiliana nasi (OR-TAMISEMI) kwa kutuma ujumbe wako kwenye sehemu ya kuweka maoni hapo chini au tutumie kupitia Private Message (PM).
Pia, tunapatikana kupitia:
Instagram @ortamisemi
Twitter @ortamisemitz
Facebook Ofisi ya Rais-Tamisemi
Website www.tamisemi.go.tz
YouTube @ortamisemi
Watssap channel: Ofisi ya Rais - TAMISEMI
Anuani
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
S.l.P 1923 Dodoma - Tanzania,
Telephone: +255 262 321 234
Fax: +255 262 322 116
Email: ps@tamisemi.go.tz
Complain: ps@tamisemi.go.tz
Kituo cha Huduma kwa Mteja
+255 735 160 210 au +255 26 216 0210
Kuanzia saa 1:30 asubuhi mpaka saa 10:30 jioni
Pole sana mkuu,DED mpya anasemajeIvi mnayatatua vipi matatizo ya MaDED kuwadhulumu wazabuni waliotoa huduma kwenye halmashauri hasa katika kipindi ambacho hao maDED hawakuwepo?
Sawa nimekuelewa...Sizingui mkuu niko serious tangu mwanzoni niliwambia hao jamaa hawawezi kuendesha hii page.
Mi nipo kufafanua baadhi ya vitu kwa sababu navijua
Kwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?Poleni,changamoto zinazohusiana na uhamisho uliza utajibiwa hapa,na nina uhakika na majibu nnayo kupa
Siredi haina mwenyewe... Yaani ni usanii mtupu.Kwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?
Hiyo ya kuhama baada ya miaka mitatu ni kwa wale wasio na connection pale TAMISEMI au UTUMISHI. Kama una connection utahama hata kama umekaa sehemu miezi mitatu tu.Kwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?
Iwe wa kubadilishana,iwe wa kuhama lazima ufikishe miaka mitatuKwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?
Nipo hapa kwa ajili ya masuala ya uhamisho,usisite kuuliza jana mtandao ulikuwa unasumbuaSiredi haina mwenyewe... Yaani ni usanii mtupu.
Uko sahihi mkuu,connection itakutoa mahali ulipo kwenda unapotaka,kuwa makini kuna matapeli piaHiyo ya kuhama baada ya miaka mitatu ni kwa wale wasio na connection pale TAMISEMI au UTUMISHI. Kama una connection utahama hata kama umekaa sehemu miezi mitatu tu.
Zamani nilikuwaga nasikia watu wakiiponda sana Tamisemi nikafiri labda majungu tu ila kupitia Hawa walioanzisha huu uzi nimegundua Tamisemi Ina wafanyakazi Vimeo balaaHawa waliofungua uzi halafu hawa replay hii inaonesha jinsi wananchi wanavoteseka bila kero kushughulikiwa katika maisha halisi ya mtanzania
Hivi kwa walimu wa shule ya msingi ili kuhamia mkoa mwingine bado ni muhimu kuhakikishiwa kimaandishi kuhusu upatikanaji wa nafasi katika halmashauri unayotaka kuhamia kwanza na kisha unatumia taarifa hiyo kama moja ya viambatanisho kwenye mfumo? Au njia nyingine yenye uhakika na nyepesi zaidi ni ipi katika haya mazingira ambapo mfumo umekuwa ni kizungumkuti?Wale wa uhamisho admin niko hapa
Nje ya mfumo ni connection my dearHivi kwa walimu wa shule ya msingi ili kuhamia mkoa mwingine bado ni muhimu kuhakikishiwa kimaandishi kuhusu upatikanaji wa nafasi katika halmashauri unayotaka kuhamia kwanza na kisha unatumia taarifa hiyo kama moja ya viambatanisho kwenye mfumo? Au njia nyingine yenye uhakika na nyepesi zaidi ni ipi katika haya mazingira ambapo mfumo umekuwa ni kizungumkuti?