Ofisi ya Rais – TAMISEMI Special Thread: Karibu tukuhudumie, tupe Maoni, Maswali, Mapendekezo na Malalamiko

Hawa waliofungua uzi halafu hawa replay hii inaonesha jinsi wananchi wanavoteseka bila kero kushughulikiwa katika maisha halisi ya mtanzania
Hao mbona ndivyo walivyo hadi maofisini kwao. Yaani hii sura waliyoionyesha hapa ndiyo sura yao halisi kabisa hata ukiwakuta ofisini kwao. Wao na ofisi ya Utumishi (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) kitabia ni mtu na pacha wake.
 
Ivi mnayatatua vipi matatizo ya MaDED kuwadhulumu wazabuni waliotoa huduma kwenye halmashauri hasa katika kipindi ambacho hao maDED hawakuwepo?
 
Ivi mnayatatua vipi matatizo ya MaDED kuwadhulumu wazabuni waliotoa huduma kwenye halmashauri hasa katika kipindi ambacho hao maDED hawakuwepo?
Pole sana mkuu,DED mpya anasemaje
 
Utaratibu wa kutoa mikopo kwa makundi maalum kuanzia mwezi huu kwa kushirikisha taasisi za kifedha(mabenki) umekaaje?
 
Poleni,changamoto zinazohusiana na uhamisho uliza utajibiwa hapa,na nina uhakika na majibu nnayo kupa
Kwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?
 
Kwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?
Hiyo ya kuhama baada ya miaka mitatu ni kwa wale wasio na connection pale TAMISEMI au UTUMISHI. Kama una connection utahama hata kama umekaa sehemu miezi mitatu tu.
 
Kwenye ess wanasema kuhama ni mpka miaka 3, jee ule wa kusubiri kuthibitishwa upo ndani ya hio mi tatu, au ni mitatu baada ya kuthibitishwa?
Iwe wa kubadilishana,iwe wa kuhama lazima ufikishe miaka mitatu
 
Hiyo ya kuhama baada ya miaka mitatu ni kwa wale wasio na connection pale TAMISEMI au UTUMISHI. Kama una connection utahama hata kama umekaa sehemu miezi mitatu tu.
Uko sahihi mkuu,connection itakutoa mahali ulipo kwenda unapotaka,kuwa makini kuna matapeli pia
 
Ushauri wangu;
Nafikiri ni wakati sasa wa kuachana na ile dhana ya kufikiri kuwa, Kila Mwalimu hata asiyekuwa na UFAULU WOWOTE kwenye somo la Hesabu anaweza kufundisha Hisabati shule za msingi kwani IMEPITWA NA WAKATI

Na hii inajidhihisha wazi wazi kwani kila mwaka takribani asilimia 80% ya wanafunzi wa shule za msingi za Umma hupata Alama 0% kwenye mtihani wa Hisabati na kuna uwezekano mkubwa kuwa; huo uwiano unaendana sambamba na Asilimia ya waalimu ambao hawana sifa ya kufundisha somo la Hisabati katika shule hizo (naamini mnatakwimu za kuonesha idadi ya waalimu wa Hisabati wenye angalau alama D ya Hesabu kidato cha nne; unaweza kuta hawafiki 15% ya mahataji, utategemea nini? kama sio sifuri) Kwa hiyo sioni haja kabisa ya kupoteza fedha za kufanya utafiti eti kwa nini wanafunzi wanafeli hesabu ambayo ndio msingi wa kila kitu, kwani sababu ipo wazi wazi kuwa, hakuna Waalimu wenye sifa ya kufundisha hesabu!

Nyongeza;
Hesabu ndio Muoarobaini wa HAYA MATATIZO YA VIKOBA/ MIKOPO UMIZA/ KUKWEPA KODI nk nk , Ukifuatilia vizuri utagundua kuwa, haya matatizo kwa kiasi kikubwa yanachangiwa na watu kutokuwa na uelewa wa Hesabu. Namaanisha wengi wao walipata alama Sifuri hivyo; hukimbilia tu kukopa bila kupiga hesabu ya marejesho na hivyo kuanza kulilia Serikali mwishoni wakidaiwa pesa nyingi.
Mfano mwingine: Kodi ya VAT ni hesabu rahisi sana ila kwa mtu aliyepata alama sifuri hawezi kuelewa na kama biashara haitoshi kuajiri mtu wa kumsaidia hesabu, anaishia kulalamika na kukwepa.....nk nk nk
MADEREVA na ajali za barabarani;
Kuendesha gari ni Hesabu (Fikiria unavyo calculate umbali wa kuovertake, unavyofanya maamuzi ya kuovertake, break nk nk) hesabu tupu.
Kama kigezo cha leseni kingekuwa na hesabu walau D, ungeshangaa ajali zikapungua hadi mkashangaa.

Kwa mtazano wangu, Ili hii Nchi iweze kuvuka hapa ilipo kwa kupata maendeleo ya haraka ya saiyansi na Technologia, Inahitaji MAPINDUZI YA HESABU (Mfano kuajiri waalimu 30,000 wa hesabu tu); hata waliopita sekondari za Umma wanajua kuwa, huko pia kuna upungufu mkubwa, nafuu yake ni kuwa, waliopo huko japo wachache Ila wana sifa ya kufundisha Hesabu.
MAENDELEO YA HARAKA HAYAWEZI KUPATIKANA BILA KUWEKA MSINGI WA HESABU!
 
Hawa waliofungua uzi halafu hawa replay hii inaonesha jinsi wananchi wanavoteseka bila kero kushughulikiwa katika maisha halisi ya mtanzania
Zamani nilikuwaga nasikia watu wakiiponda sana Tamisemi nikafiri labda majungu tu ila kupitia Hawa walioanzisha huu uzi nimegundua Tamisemi Ina wafanyakazi Vimeo balaa
 
Wale wa uhamisho admin niko hapa
Hivi kwa walimu wa shule ya msingi ili kuhamia mkoa mwingine bado ni muhimu kuhakikishiwa kimaandishi kuhusu upatikanaji wa nafasi katika halmashauri unayotaka kuhamia kwanza na kisha unatumia taarifa hiyo kama moja ya viambatanisho kwenye mfumo? Au njia nyingine yenye uhakika na nyepesi zaidi ni ipi katika haya mazingira ambapo mfumo umekuwa ni kizungumkuti?
 
Nje ya mfumo ni connection my dear
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…