Ole Sendeka: Waziri Pindi Chana anataka Simanjiro, Ngorongoro na Longido kuwa Mapori ya akiba. Wamasai hatutakubali kamwe!

Ole Sendeka: Waziri Pindi Chana anataka Simanjiro, Ngorongoro na Longido kuwa Mapori ya akiba. Wamasai hatutakubali kamwe!

Naona ile pride ya mimi Mmasai wa Arusha inaenda kuftika. Serikali inawapeleka Handeni kwa Wazigua.



Watawakuta na wenzao wambulu wapo walijipeleka wenyewe mapema katika harakati za kutafuta maisha na wanajishughulisha na shughuli za kilimo na ufugaji vizuri tu!
 
Yaani wilaya nne zigeuzwe mapori ili waarabu wawinde na kusafirisha wanyama wetu bila bughudha!! Na watu wanakuja na justification!!! Kweli rushwa inapofusha macho, hata hao waarabu wanatuna sisi manyani kweli


Wilaya zenyewe ni zipi Kwani ?

Yani inashangaza nyie?!
 
Mbunge wa Simanjiro amesema nia ya Waziri Chana ni kuifuta jamii ya kimasai kwenye uso wa Arusha kwa kuzibadili wilaya nne kuwa pori la akiba.

Ole Sendeka amesema one mvua like just hili halitawezekana.

Spika Tulia ameingilia kati kutaka Ole Sendeka atoe ufafanuzi wa kisheria kuhusu mapori ya akiba.

Ole Sendeka amechemka kutoa ufafanuzi wa kisheria kwamba Waziri anataka kufunga wilaya nne za Wamasai.

Huyu mzee anayeitwa olesendeka ni mfano wa wabunge wengi wa ccm ambao wanaliona tatizo badala ya kutoa mbadala kwa suluhisho la mtatizo wanaongea kutafuta Kiki za kisiasa shame upon them
 
Ukweli CCM inataka kuwafuta wa masai asee
Naona kila comment unajaribu kuingiza uvyama ili kulazimisha hoja yako iungwe mkono na wanaharakati uchwara, lkn kinachofurahisha wengi wanakupuuza, na kuzipita comments zako kimya kimya kama hawazioni. Ni kwa vile haujui tu kwamb watu wote humu washafaham kama wewe ni mchunga ng'ombe wa Kenya, unaetaka kubaki katika ardhi yetu kwa masilahi ya mabwanyenye wa nchi yako. Shame on you.
 
Mbunge wa Simanjiro amesema nia ya Waziri Chana ni kuifuta jamii ya kimasai kwenye uso wa Arusha kwa kuzibadili wilaya nne kuwa pori la akiba.

Ole Sendeka amesema one mvua like just hili halitawezekana.

Spika Tulia ameingilia kati kutaka Ole Sendeka atoe ufafanuzi wa kisheria kuhusu mapori ya akiba.

Ole Sendeka amechemka kutoa ufafanuzi wa kisheria kwamba Waziri anataka kufunga wilaya nne za Wamasai.
Wacha wakulane menyewe ,CCM kwa CCm yetu macho!
 
Walipomtoa tu Lukuvi na kumuweka mtoto wa mlamba asali kauli ya ndugai lazima itimie. Kuna watu kwao pesa ni muhimu kuliko utu.
Apendae pesa Katu hatoshiba pesa siku akikua ataona yooote ni bure tupu zaidi ya kuukimbiza upepo tu. Pesa Ina thamani pale usipokuwa nayo.
 
Hao wamasai wakiwa tanzania wanajiita watanzania..wakiwa kenya wanajiita wakenya,na kenya wanajifanya wajanja wakatimwingine kuzuia watarii wanaokuja tanzania...sasa sisi tunawahamishia.wamasai.wetu pwani .halafu kule tunaweka mpaka imala kabisa kwenye mipaka yetu ya hifadhi kati yetu nakenya...
Mzungu.akitaka kuona mmasai wa tanzania aje tanzania kweli na akitaka kuona mmasai wa kenya abaki kenya...

Hizo njia za ushirika wa hifadhi nakenya ndio.njia zinazosafirisha madini yetu,tembo.wetu na mambo mengine...
 
..Spika anamkatisha-katisha mchangiaji Mh.Ole Sendeka na hampi muda wa kujenga hoja yake.


Ole sendeka ametumwa na watu kutoka nje na hakujiandaa, hakuingia akiwa amekamilika akaishia kufuta hiyo hoja yake.

Kuna tafsiri potofu ya kinachofanywa na serikali kutoka kwa wanaharakati na haiwezi kuwasaidia wao na wale wanaofikiwa na hiyo tafsiri, haiwasaidii chochote.
 
Hao wamasai wakiwa tanzania wanajiita watanzania..wakiwa kenya wanajiita wakenya,na kenya wanajifanya wajanja wakatimwingine kuzuia watarii wanaokuja tanzania...sasa sisi tunawahamishia.wamasai.wetu pwani .halafu kule tunaweka mpaka imala kabisa kwenye mipaka yetu ya hifadhi kati yetu nakenya...
Mzungu.akitaka kuona mmasai wa tanzania aje tanzania kweli na akitaka kuona mmasai wa kenya abaki kenya...

Hizo njia za ushirika wa hifadhi nakenya ndio.njia zinazosafirisha madini yetu,tembo.wetu na mambo mengine...
Majirani wanatuibia tangu tukiwa watoto na kibaya zaidi wakishafanya hivyo wanaongea maneno ya dharau dhidi yetu.

Hayo yamefika mwisho, ni lazima tuheshimiane. SSH ametumia gharama kubwa kuendeleza pale alipoishia JPM katika suala zima la kuipatia heshima nchi wanayoongoza, akaenda mbali kwa kuandaa royal tour ili hata wale wachache wenye mitazamo ya kizamani waweze kupewa uelewa mpya wa nchi hizi mbili.
 
..hatuna utamaduni wa kusikiliza hoja mpaka mwisho bila kumkatisha-katisha mchangiaji.

..mimi nimeona kuna kitu alichokuwa nacho Ole Sendeka lakini kwasababu ya kusakamwa na Spika ameshindwa kuchangia na hoja yake kueleweka.
Spika amemuacha aongee mpaka mwisho halafu akaombwa asome tafsiri ya sheria iliyoandikwa katika makaratasi aliyoingia nayo bungeni, Ole sendeka akashindwa na kuishia kufuta hoja yake!.

Unajaribu kumpaka matope Dr Tulia lakini anayo substance pana sana akiwa ni spika mwanasheria.
 
Ole sendeka ametumwa na watu kutoka nje na hakujiandaa, hakuingia akiwa amekamilika akaishia kufuta hiyo hoja yake.

Kuna tafsiri potofu ya kinachofanywa na serikali kutoka kwa wanaharakati na haiwezi kuwasaidia wao na wale wanaofikiwa na hiyo tafsiri, haiwasaidii chochote.
..kuna pande mbili zinazokinzana. Kwa hiyo, Ole Sendeka ametumwa, na wanaompinga nao wametumwa.

..Tunapaswa kujiuliza, kwanini migogoro ktk eneo hilo haiishi?

..Serikali ilikuwa wapi mpaka idadi ya wafugaji na mifugo imekuwa kubwa na sasa wanadai inaathiri uhifadhi?

..Kungekuwa na mpango endelevu wa kutoa elimu, na incentives, kuwabadilisha wachungaji kuwa wafugaji, na kuwapatia maeneo ya kufuga, serikali ingeweza kuepusha mgogoro tunaoshuhudia sasa hivi.
 
Spika amemuacha aongee mpaka mwisho halafu akaombwa asome tafsiri ya sheria iliyoandikwa katika makaratasi aliyoingia nayo bungeni, Ole sendeka akashindwa na kuishia kufuta hoja yake!.

Unajaribu kumpaka matope Dr Tulia lakini anayo substance pana sana akiwa ni spika mwanasheria.

..Spika alikuwa anamlazimisha Ole Sendeka asome vifungu vya sheria vile anavyotoka yeye Spika.

..Kwa maoni yangu Ole Sendeka alitakiwa apewe nafasi kusoma vifungu vya sheria vile ambavyo yeye alikuwa amejiandaa kwa hoja yake.

..Naamini mchangiaji yeyote mle bungeni hatakiwi kukatishwa-katishwa kama ialivyofanyiwa Ole Sendeka.

..Hata kitendo cha kumpa TAARIFA mbunge wakati akichangia nakiona ni bugudha. Huo ndio mtizamo wangu.
 
Madam spika awaache wabunge wazungumze hoja zao na serikali aitake izijibu, anapoikingia kifua serikali na kutaka isisemwe, anakosea.
 
Ole sendeka ametumwa na watu kutoka nje na hakujiandaa, hakuingia akiwa amekamilika akaishia kufuta hiyo hoja yake.

Kuna tafsiri potofu ya kinachofanywa na serikali kutoka kwa wanaharakati na haiwezi kuwasaidia wao na wale wanaofikiwa na hiyo tafsiri, haiwasaidii chochote.
Bwashee mule bungeni hakuna asiyetumwa
 
..Spika alikuwa anamlazimisha Ole Sendeka asome vifungu vya sheria vile anavyotoka yeye Spika.

..Kwa maoni yangu Ole Sendeka alitakiwa apewe nafasi kusoma vifungu vya sheria vile ambavyo yeye alikuwa amejiandaa kwa hoja yake.

..Naamini mchangiaji yeyote mle bungeni hatakiwi kukatishwa-katishwa kama ialivyofanyiwa Ole Sendeka.

..Hata kitendo cha kumpa TAARIFA mbunge wakati akichangia nakiona ni bugudha. Huo ndio mtizamo wangu.
Alipewa muda wa kutosha na hata angepewa saa nzima bado asingeweza kujieleza vyema kwani vifungu vya sheria havikuwemo kati ya makaratasi yake.

Naibu waziri alijibu kwa hasira kwani alichukulia kama vile serikali inataka kuwaonea wamasai wakati eneo la hifadhi halina watu.

Kuna suala la kizalendo linafanywa na serikali tatizo la watanzania siku zote ni tafsiri potofu kuenezwa kwa haraka kuliko zile sahihi.
 
Back
Top Bottom