Salaam Wakuu,
Rais Samia katika Kongamano la Wafanyabiashara wa Oman na Tanzania, amesema kuna umuhimu Mkubwa wa kuangalia Usafiri wa Majini akimanisha Meli yenye Uwezo wa kusafirisha Wanyama wakiwa hai kutoka Tanzania kwenda Oman.
Watu hapa wasifikilie Wanyama Pori tu, Bali ni Habari njema kwa Wafugaji wa Tanzania kwani sasa Wataanza Kusafirisha Ng'ombe, Sungura, Kitimoto, Mbuzi, Swala, Twiga nk hasa kwa wawindaji wenye Vitaru.
Pia kazungumzia kuhusu meli za Kuvua samaki Bahari Kuu.
Amewataka Oman waje kuwekeza Tanzania ardhi ipo ya kutosha.
Watanzania Kaeni Mkao wa kula.
............................................................................
Rais Samia akiwa kwenye kongamano Kiuchumi nchini Oman, amesema kuwepo kwa vyombo vya usafirishaji vya majini kusafirisha wanyama walio hai na bidhaa mbalimbali kwenda Oman kutaboresha biashara kati ya pande hizo mbili
Pia amegusia japokuwa tuna makubwa ya kuvua, kwa sasa hamna uvuvi wenye tija kwa taifa, amesema “kuna nchi zinakuja Tanzania kuvua na hatuwezi kuwafukuza kwa sababu hatuna vifaa, hivyo wanavua na kuondoka, hili ni eneo lingine ambalo tunaweza kushirikiana kwa pamoja”
Amesema kuwa kongamano la mwaka huu limekusudia kuangazia namna Tanzania itashirikiana na Oman katika sekta za utalii, kilimo, Uzalishaji (viwanda) mifugo na uvuvi na usafirishaji wa majini.
Magu hatarii🥲🥲
1. JPM anajenga Reli ya Mwendo kasi – SGR.
2. JPM anajenga Bwawa la Umeme – Nyerere HydroPower.
3. JPM amenunua Ndege 13 aina tofautitofauti.
4. JPM amejenga Ikulu kule Dodoma na yale Magorofa ya Wizara kule Mji wa Serikali Dodoma ( Mtumba) Magufuli City
5. JPM amehamisha Makao Makuu ya Serikali na ameijenga Dodoma imekuwa Jiji
6. JPM amejenga FlyOver Dar es Salaam pale Ubungo na TAZARA
.
7. JPM amejenga daraja la Tanzanite pale Selander.
8. JPM ametengeneza huu Mfumo wa Kompyuta wa Malipo ya Serikali.
9. JPM alikuwa anaweka umeme hadi Vijijini (kwa Tsh. 27,000/= tu.)
10. JPM ameshawishi Bomba la Mafuta kutoka Uganda lipite Tanzania.
11. JPM anajenga daraja la Kingongo Ferry Busisi kule ziwa Victoria.
12. JPM amejenga Meli kubwa mbili mbili kila ziwa, yaani Ziwa Victoria 2, Ziwa Tanganyika 2 na Ziwa Nyasa 2.
13. JPM amejenga Hospital za Kanda kubwa nne… Dodoma, Mara, Mtwara, Geita na Songea
14. JPM amejenga Hospitali za Wilaya Zaidi ya 70
15. JPM amejenga Mradi Mkubwa wa Maji ya Victoria kule Tabora
16. JPM amejenga Mradi wa Maji Mkubwa Arusha
17. JPM amejenga Barabara ya Njia Nane Dar es Salaam hadi Kibaha
18. JPM alikuwa anajenga Mizani za Kisasa kabisa Kwenye Barabara zote kubwa
19. JPM amejenga Vituo vya Afya Zaidi ya 500
20. JPM amejenga na Kununua Rada 4 za AirPort
21. JPM amejenga Viwanja vya Ndege Mara, Iringa, Mbeya, Chato, Songea na Rukwa
22. JPM amejenga Masoko ya Madini kila Mikoa yenye migodi ya madini
23. JPM amejenga ukuta wa Mirerani na kuweka Camera za Ulinzi
24. JPM amejenga Bandari Kilwa, na kuzipanua Bandari Mtwara, Tanga na Dar es Salaam
25. JPM amejenga Masoko ya Kisasa zaidi, ya maana kama Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam
26. JPM amejenga Bus Stand za Kisasa Zaidi mikoani kama Dodoma, Mwanza, Dar es Salaam nk
27. JPM amenunua Vifaa Tiba kama MRI, CT Scan, Vifaa vya Kufanyia Oparations za Moyo pale JKCI Wagonjwa wanatoka nchi jirani kuja kutibiwa Tanzania
28. JPM amejenga Vivuko vya Majini sehemu mbalimbali kama Mafia, Kilwa, Ukerewe
29. JPM amejenga Barabara za Lami za adabu miji mingi sana, Barabara zina mifereji, Taa, na Taa za kuongozea magari.
30. JPM amejenga Shule za Msingi na Sekondari na kukarabati za zamani zikawa Bora kama Vyuo vikuu
31. JPM ametengeneza Vitanda kwenye mahospitali watu hawalali chini.
32. JPM ametengeneza Madawati karibia shule nyingi sana wanakaa kwenye Madawati.
33. JPM kajenga Hostel pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) uhaba wa vyumba umepungua.
34. JPM akasimamia mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu, na boom likawa linatoka kwa wakati (Migomo Vyuoni imeisha).
35. JPM aliamua kutusomeshea Watoto bila kulipa ADA ya Shule (Msingi na Sekondari)
36. JPM kafufua reli ya Kati na reli ya kwenda Moshi hadi Arusha.
37. JPM alikuwa anajenga kiwanda cha Sukari cha Magereza Morogoro.
38. JPM amejenga Kiwanda cha Viatu vya Jeshi – Lukaranga Moshi viatu haviagizwi tena nje ya nchi.
39. JPM anajenga Kiwanda cha Vifaa Tiba na Dawa huko Njombe.
40. JPM anajenga Barabara za Mwendo Kasi Mbagara hadi Gerezani Kariakoo
41. JPM amejenga FlyOvers pale Veta na Uhasibu Dar es Salaam.
42. JPM amejenga Vituo Vya Polisi, Nyumba za Askari Polisi na Magereza.
43. JPM amejenga yale Magorofa ya pale Magomeni na aliruhusu watu wakae bure kwa Miaka 5..
Hongera kwa jembe JPM.
Watu waache maneno ya ajabu, watu wafanye Yao tuyaone.
wasikae kutwa kumuongelea Hayati.. Rose Muhando aliimba Jifunze kwa waliofanikiwa..
📌📌Hayati Magufuli hakuwaji kwenda kuomba mikopo na wawekezaji ulaya.