Tetesi: Ongezeko la masharti ukitaka kufungua akaunti ya Benki lazima kuongezea kiapo cha mahakama licha ya kuwa na vitambulisho husika

Tetesi: Ongezeko la masharti ukitaka kufungua akaunti ya Benki lazima kuongezea kiapo cha mahakama licha ya kuwa na vitambulisho husika

Mkuu Britannica, asante kwa taarifa hii, kwenye ukweli unaleta za kweli kabisa tena za Moto moto kutoka jikoni, ila pia ni mpishi mzuri, ukiamua kupika, na viungo unavyo pikia, pilau na biriani zitasubiri, kama ile ya kisiwa cha Guam.
P
Unataka useme nn mkuu?
 
Ninavyojua mimi japo sio nguli wa maswala haya ni kwamba,kiapo hutumika wakati ambapo vitambulisho unavyo sawa na ni halali kabisa lakini unakuta majina yanakuwa hayako sawa kwenye baadhi ya documents zako. Mfano unaitwa Matayo Samwel kwenye vielelezo vingine ukasomeka Methew Samuel. Mara nyingi watu huwa tunasema tu kirahisi kuwa ni majina yale yale,hapo lazima utadaiwa kitambulisho. Na kuna kesi za aina mbali mbali hiyo ni moja tu ya mfanano.
Na kuhusu pesa inapoingia kuwa zaidi ya milioni 50,kibenki wakati unafungua akaunti kuna maswali wanakuuliza hata hilo la miamala ya kiasi gani unatarajia kwa mwezi huwa linaulizea,sasa wateja mara nyingi huwa tunatoa taarifa za uongo. Mfano mtu unaweza kusema aah ni pesa kidogo tu kama milioni kumi mpaka ishirini. Mtu wa benki ana anfika kaka unavyoongea na wanaweka hivyo viwango kwenue system zao.
Sasa kukiwa na kiasi zaidi ya hapo kunakuwa na alert kwenye akaunti yako lazima benki wapate uthibitisho wa hivyo viwango kupanda.
Mkuu nadhani umekariri tu,kuna mabadiliko sana kwa sasa! Mimi ni muathirika wa hii issue. Niliuza nyumba yangu mkoani zaidi ya 60mil. Me nilikuwa na akaunti yangu kwenye bank ambayo haina branch huko. Nikalazimika kufungua akaunti kwenye moja ya hizi bank zenye nasaba na serikali. Na wakati nafungua nilijieleza km nalipwa pesa za kuuza nyumba yangu. Na mtu aliyekuwa ananilipa ana akaunti hapohapo ktk ile bank. Nilifanya taratibu zote na pesa ikaingizwa. Baada ya siku 2 nilifanikiwa ku-withdraw milioni 3 na nusu. Na nikarudi dar. Nimefika dar nimekaa km wiki moja,nikaenda kumlipa mtu milioni 35 za nyumba ambayo nilitaka kununua hapa mjini. Nikakuta nimepigwa pin. Yaani mpaka hv nnavyoandika nimeshapeleka vielelezo vyote nilivyoombwa lkn bado sijaruhusiwa kutumia pesa zangu mwenyewe. Na ni kesi ya tangu mwaka Jana mwezi wa 9. Yaani hata kuchukua elf 20 siwezi. Hii nchi imeshaharibika. Nyumba sina na hela sina! Usicheze na jiwe mkuu,ndo maana kila siku anasema hela zipo!
 
Ujamaa huu unaharibu nchii na kuturudisha nyuma kimaendeleo.

Siujui ni wawekezaji gani watakuja kuwekeza kwenye nchi yenye sera mbovu kama hizi za ujamaa uchwara!
Hakuna kitu cha kijinga kama Communism jamani
 
Mkuu nadhani umekariri tu,kuna mabadiliko sana kwa sasa! Mimi ni muathirika wa hii issue. Niliuza nyumba yangu mkoani zaidi ya 60mil. Me nilikuwa na akaunti yangu kwenye bank ambayo haina branch huko. Nikalazimika kufungua akaunti kwenye moja ya hizi bank zenye nasaba na serikali. Na wakati nafungua nilijieleza km nalipwa pesa za kuuza nyumba yangu. Na mtu aliyekuwa ananilipa ana akaunti hapohapo ktk ile bank. Nilifanya taratibu zote na pesa ikaingizwa. Baada ya siku 2 nilifanikiwa ku-withdraw milioni 3 na nusu. Na nikarudi dar. Nimefika dar nimekaa km wiki moja,nikaenda kumlipa mtu milioni 35 za nyumba ambayo nilitaka kununua hapa mjini. Nikakuta nimepigwa pin. Yaani mpaka hv nnavyoandika nimeshapeleka vielelezo vyote nilivyoombwa lkn bado sijaruhusiwa kutumia pesa zangu mwenyewe. Na ni kesi ya tangu mwaka Jana mwezi wa 9. Yaani hata kuchukua elf 20 siwezi. Hii nchi imeshaharibika. Nyumba sina na hela sina! Usicheze na jiwe mkuu,ndo maana kila siku anasema hela zipo!
Zipo Blackmail zinachezwa bank na baadhi ya Polisi na Takukuru wasio waaminifu, hufunga A/C za watu kwa visingizio vya kizushi ili mwenye A/C atoe Rushwa kwa meneja wa Bank, Ujue kila Ubaya ukitengenezwa wapo wajanja hutumia huo mwanya kujinufaisha, Kwa sasa ni mda wa vyombo vya Dola kuneemeka kupitia Ukuda wa mtukufu na Naibu Rais ndugu Bashite, huko mitaani wananchi wa kawaida wanalia njaa lakini wapo wajanja wachache wanapiga pesa kwa kwenda mbele kuliko tawala zote tokea Nchi ipate uhuru, Kufa kufaana.
 
Pamoja na kwamba hata kama utakuwa na vitambulisho vyoote husika lakin muhim kuwa na kiapo cha mahakamani kwa taarifa unazotoa wakati wa ufunguzi wa akaunt,

Wakati huo huo akaunt zote ambazo zitaonekana kupitisha hela kubwa kubwa zitachunguzwa na wakibaini hela inapita tu bila kuwa na uthibitisho wa hela zako, akaunt inazuiliwa, na kiasi chenyewe ni zaid ya milion 50 kwa miezi kadhaa
Kwa wafanyakazi wa ENI EMU BII ninyi ni mashahidi wamepokea waraka toka BII OO TII kwamba hakuna mtu ku deposit zaid ya milion 40 bila maelezo zimetoka wapi

Pia kwamba Huruhusiwi kufungua akaunt mbili za aina moja ndani ya benki moja kama ilivyokuwa zamani,

Stay tuned,


Britannica,

United States of America masharti sio kiasi hiki aisee!

Unbankable population itaongezeka!

Tulisema kitambulisho cha taifa kita-solve everything,ila naona it is useless on every step!
 
Awamu ya tano ni awamu ya kuwatia hofu wananchi kwa miaka yote tokea iimgie madarakani, lakini wajanja wachache wakiwemo mameneja wa mabenk wamepiga pesa za wateja kwa visingizio kuwa A/c zao zinachunguzwa na vyombo vya Dola wamekuwa wakila njama kisha kula pesa za watu, wametumia fursa hizo kujinufaisha na sasa Bank zinazidi kuongeza kero kwa wateja wao unategemea nini zaidi ya wananchi kuendelea kuichukia zaidi Serikali ya mtukufu toka chato?
 
United States of America masharti sio kiasi hiki aisee!

Unbankable population itaongezeka!

Tulisema kitambulisho cha taifa kita-solve everything,ila naona it is useless on every step!
Kama ni kweli kwa spidi hii itafika mahali hata mtu kutoka nyumbani kwako unashindwa maana nako kutawekewa masharti.
 
Watanzania walivyo wavivu watajenga ki room na kuzihifadhi hela zao humo majumbani mwao... Mwaka jana na mwaka huu hakuna mwekeza mpya aliye kuja kuwekeza Tanzania, hata wale matajiri wa nyumbani/Tanzania hamna hata mmoja anaepanua biashara zake tena....
Kwa kero zao hakuna Mtanzania atazipenda bank tena pia ujue mameneja wa bank wengi wamekuwa wakila njama kufunga A\c za watu kisha kuwachukulia pesa kugawana na wala njama wenzao.
 
Kama ni kweli kwa spidi hii itafika mahali hata mtu kutoka nyumbani kwako unashindwa.

Maana mkuu hakuna maana ya kitambulisho cha taifa sasa!

Maana kile ndio kila kitu,kina SS number,finger prints,your full data on the national database,etc.

Ambapo akiingia anaona kila kitu.Then wanarudi kinyume wanasema Kitambulisho hakina utoshelezi inatakiwa some other things,hivyo hakina maana to begin with!

USA ukiwa na Social Security number to unaaminika kila mahali maana data zako zipo legitimately kwenye system.

Baada ya kurahisisha vitu wanazidi weka vitu vinakua vigumu mnooo!

You know what will happen?

Watu wengi hawataweza kumiliki account,hela nyingi waziweka kwenye mpesa,nk!

Tegemea mobile money volume to triple or quadruple from now on.

Of which it is even harder for government to regulate!

Vikampuni vidogo sana vitahamia mobile money too.Na hivi vikampuni ni vingi!

Mabenki mengi yatakufa,we will see this happen more next year!
 
Mkuu Daudi asante, maana angalau embe lina umbo zuri, dogodogo na liko smooth, ingekuwa umenitukana kichwa kama dafu, nazi au boga, ningekasirika.
P
Pole Paskal hizo ndizo changamoto za mitandaoni, lakini tambua kuwa wananchi wamechoka kunyanyaswa na CCM mpaka wamepagawa sasa
 
Black market itapaa kwa sana.
Crypto currency itapaa pia

Banking inaenda kufa kifo kibaya

Itafata mobile money huko watapiga pin kwenye utoaji wa hela
 
Maana mkuu hakuna maana ya kitambulisho cha taifa sasa!

Maana kile ndio kila kitu,kina SS number,finger prints,your full data on the national database,etc.

Ambapo akiingia anaona kila kitu.Then wanarudi kinyume wanasema Kitambulisho hakina utoshelezi inatakiwa some other things,hivyo hakina maana to begin with!

USA ukiwa na Social Security number to unaaminika kila mahali maana data zako zipo legitimately kwenye system.

Baada ya kurahisisha vitu wanazidi weka vitu vinakua vigumu mnooo!

You know what will happen?

Watu wengi hawataweza kumiliki account,hela nyingi waziweka kwenye mpesa,nk!

Tegemea mobile money volume to triple or quadruple from now on.

Of which it is even harder for government to regulate!

Vikampuni vidogo sana vitahamia mobile money too.Na hivi vikampuni ni vingi!

Mabenki mengi yatakufa,we will see this happen more next year!
Too bad. Lakini lazima kuna motive behind this, itajulikana au inajulikana tayari. Kuna kitu tu.
 
"Ujamaa upo wapi katika hayo aliyoyaelezea Britannica hapo juu.

Ni jambo la kusikitisha sana kwa baadhi ya watu kudhani kwamba maana ya 'Ujamaa' ni kuzuia watu wasiwe na maisha bora.

Tafsiri hii wanailazimisha kila mahali panapotokea kuwa na matatizo ya uchumi, hata kama matatizo hayo hayana uhusiano wowote na Ujamaa.

Kwa hiyo jambazi akiua na kupata pesa nyingi na kufanikisha maisha yake, tusifu kuwa "Ubepari" ni mzuri?

Unapotoa mfano wa Kenya kufanikiwa kwa ubepari, ina maana Kenya wanaruhusu utakasishaji wa pesa kupitia kwenye mabenki?

Unapoimba,' Ujamaa, Ujamaa', umezuiwa kufanya shughuli zako halali kwa kufuata taratibu ili ujiletee mafanikio, au unataka uachiwe mianya ya kuwaumiza wengine?

China bado ni waCommunist, wameendelea mpaka walipofikia wakiwa ndani ya mfumo wa kiCommunist. Leo wewe bado umelala kwenye nyimbo zilezile walizoachana nazo wengi. Usidhani Ubepari ni kila kitu. Beza 'Ujamaa, lakini elewa kwamba nao una mchango mkubwa katika ufanisi wa taifa lolote, hata huko wanakojitambulisha kuwa Mabepari wa Ulimwengu.

Achana na nyimbo za kutapishwa kama Kasuku. Tumia akili yako uliyojaliwa kupambanua mambo.muhimu kama haya.

Kama utaratibu ni mbaya benki, sio lazima iwe sababu ya 'Ujamaa'.
Twende sawa kwanza, ujamaa si ukomunisti?
 
Back
Top Bottom