Open Letter: Rais Samia, TRA isiyo na Support yako, ni Kifo cha Taifa

Najua ni mtumishi wa TRA,lakini ni kweli kwamba huwezi kumbembeleza mfanyibiashara asiyetaka kulipa kodi.Uta-coerse to some point,lakini akikataa ni lazima alazimishwe na sheria kufanya hivyo.
Wafanyabiashara sio waajiriwa, naona unaoverlook hilo
Tunduma wafanya biashara walihamia upande wa zambia walipoona wanasumbuliwa na kodi zisizoeleweka , na hadi leo hii baadhi hawajarudi upande wetu,. bado hujapata clue tu mfanyabiashara ni mtu gani?
unaweza kumnyanyasa muajiriwa kwa kuwa hana means , wafanyabiashara wanondoka na mitaji yao kuelekea kwenye nafuu ya kodi, na huwezi zuia hilo, mitaji ni yao na huko wanapokwenda wanapokelewa, kwa sababu watalipa kodi na kuchangia maendeleo ya nchi husika.
 
Hayo yote ni sawa kabisa mkuu,TRA wabuni new revenue sources,hilo halina ubishi,ila under scrutiny here are President Samias' statement ambayo ina potential ya kupunguza mapato.
Mapato yaliyokusanywa mengi yalikuwa cosmetic na fictious kwa vile yalitokana na dhuluma na kubambikwa/kupora ili mradi kufikia malengo yaliyokuwa yamewekwa bila uhalisia wa mapato ya biashara au faida,mitaji ilipigwa kodi na kuua biashara. Ndiyo maana biashara nyingi zikafa eg kampuni ya tumbaku morogoro.
 
Hii ni hatari sana.

KODI NDIO usalama na UHAI wa TAIFA bila kukusanya KODI basi tena ndio tunaenda kuzimu.

wafanya biashara walio wengi ni wa kwepa KODI kamwe hawawezi kulipa kodi bila kushurutishwa.

Kwenye suala la KODI viongozi wetu wawe imara.
kukwepa kodi ni kama tabia za utoro shuleni, ukitaka kutatua tatizo hili ni lazima ujiulize kwa nini wanafunzi ni watoro.
ukitjmia nguvu sana hufanikiwi na unazidi kuongeza tatizo , kuna nchi kukwepa kodi ni aibu maana kodi ipo wazi na inalipika.
 
Weee kaa kimyaaa katika kipindi deni la taifa limepanda maradufu ni kipindi cha mwendazake
 
kukwepa kodi ni kama tabia za utoro shuleni, ukitaka kutatua tatizo hili ni lazima ujiulize kwa nini wanafunzi ni watoro.
ukitjmia nguvu sana hufanikiwi na unazidi kuongeza tatizo , kuna nchi kukwepa kodi ni aibu maana kodi ipo wazi na inalipika.
Nukuu;

"Mfanyabiashara/Tajiri kuingia ktk Ufalme wa Mbiguni ni sawa na ngamia kupenya ktk tundu la sindano"


wafanyabiashara walio wengi wanataka kupata faida kwa njia yoyote ile.................

wachache ni wazalendo kwa Taifa lao, wengi ni wa kwepa kodi.

ni ukosefu tu wa maadili na uzalendo, ndio maana kuna hata baadhi ya viongozi ni wabadhirifu wa mali za umma, vivo hivyo kuna baadhi ya wafanyabiashara sio waaminifu.

Tulipe kodi kwa ajili ya kulijenga taifa letu
 
Kilichozungumzwa ni kama zile kodi za ushuru wa magari bandarini, kodi ilikuwa milioni 3 mara paap imekuwa milioni 5 na usipolipa gari linapigwa mnada. Wakati sheria zinasema tozo za kodi zinapangwa na kupitishwa bungeni wakati wa bajeti ya bunge na sio tu Kamishna wa TRA au Rais wa nchi atavyojisikia. Ndio akasema TRA tozeni kodi kwa sheria na kutoonea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…