Orodha ya Mistari iliyo nichanganya kwenye Biblia takatifu kuhusu Ubatizo

Orodha ya Mistari iliyo nichanganya kwenye Biblia takatifu kuhusu Ubatizo

BAKIIF Islamic

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2021
Posts
600
Reaction score
1,843
Msaada,

Kwanza kabisa, mimi ni muumini wa dini ya Kiisilamu, lakini naisoma Biblia hatua kwa hatu, Mistari ifuatayo imenichanganya sana kunako swala la Ubatizo. Inaaminika kwamba kila mtu huzaliwa akiwa ni muislamu hadi pale atapobatizwa ndio atakuwa Mkristo safi. Sasa ubatizaji nimeokutana nao katika biblia naona umegawanyika vifungu vitatu na sielewi kipi ni sahihi kufuatwa.

MATHAYO 3:11
Kweli mimi ''nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba'' bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; ''yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.''

MARKO 1:8
Mimi ''niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.''

LUKA 3:16
Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi ''nawabatiza kwa maji;' lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; ''yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto''

YOHANA 1:33
Wala mimi sikumjua; lakini ''yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, ''Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, ''huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.''
.................

Ubatizo wa Yohana ni "maji" , ubatizo wa yesu ni "roho mtakatifu na moto". Kwahiyo Yohana alibatiza watu katika maji ya mto kama yordani (maji mengi) lakini yesu na wanawafunzi wake walibatiza bila maji:

Navyofahamu "ubatizo" ni neno lenye asili ya kigiriki maana yake: "kuzama mwili wote"

kwahiyo;

1) Ubatizo wa maji: kuzama katika maji mwili wote (full immersed in water)

2) Ubatizo wa moto; ulipaswa kuwa "kuzama mwili wote katika moto unaowaka"

3) Ubatizo wa roho mtakatifu ulipaswa kuwa "kumezwa mwili wote na huyu roho mtakatifu"
..............

1) ubatizo wa maji umethibiti kutumiwa na Yohana na ata Yesu amebatizwa na Yohana kwa ubatizo huo katika mto yordani pia wakristo ata sasa wanatumia ubatizo huo "tunashuhudia"

2) ubatizo wa moto haijathibiti kutumika na yeyote, mfano wa ubatizo huu ulipaswa kuwa kama Ibrahimu katika kisa cha kuchomwa moto na Nimrod kwa kosa la kuvunja masanamu yao akatoka salama bila kuungua.

3) Ubatizo wa roho mtakatifu, haijathibiti kutumika (kama maana halisi ya neno "ubatizo") ubatizo huu ulipaswa kuwa kama kisa cha nabii Yona (Yunus) kumezwa na samaki alafu kumtema akiwa hai basi roho mtakatifu katika ubatizo huu alitakiwa kuwameza watu, na kuwatema wakiwa hai.
.........

Sasa tumeona

1) Ubatizo wa Yohana -- kutumia maji (confirmed)
2) Yesu na wanafunzi wake walibatiza bila maji lakini haikuoneshwa namna walivyobatiza watu--kivipi (hidden)
3) Swali linabaki sasa kujua "ubatizo aliofundisha paulo" --ni upi ??

Rejea hoja: "ubatizo wa Yohana na ubatizo wa Yesu" swali je Paulo kafundisha ubatizo gani ? je ndugu zetu wakristo wanafuata ubatizo gani ?


UBATIZO 2.JPG
 
Shida YAKO ni nini ndugu,kufuatilia kujua JAMBO ambalo hauna Impact nalo??

Walio wafuasi wa Yesu,yaani Waumini husika wanatambua!! Kama nawewe uko tayari Kumpokea Bwana Yesu kuwa ni Mwokozi wa Maisha YAKO,karibu! Then utapewa mafundisho na kuelewa KILA Kitu.

Hata tukikujulisha kwasasa,haitakusaidia Chochote.
 
الاشتعال بما يفيد
عن أبي هريرةَ رَضِي اللهُ عَنْهُ قالَ: قالَ رسولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
{مِنْ حُسْنِ إِسْلاَمِ الْمَرْءِ تَرْكُهُ مَا لاَ يَعْنِيهِ}.رواه الترمذي
 
Shida YAKO ni nini ndugu,kufuatilia kujua JAMBO ambalo hauna Impact nalo??

Walio wafuasi wa Yesu,yaani Waumini husika wanatambua!! Kama nawewe uko tayari Kumpokea Bwana Yesu kuwa ni Mwokozi wa Maisha YAKO,karibu! Then utapewa mafundisho na kuelewa KILA Kitu.

Hata tukikujulisha kwasasa,haitakusaidia Chochote.
Shida yangu ni kufahamu, Naomba kufahamisha, turudi kwenye hoja
 
الاشتعال بما يفيد
عن أبي هريرةَ رَضِي اللهُ عَنْهُ قالَ: قالَ رسولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
{مِنْ حُسْنِ إِسْلاَمِ الْمَرْءِ تَرْكُهُ مَا لاَ يَعْنِيهِ}.رواه الترمذي
وَمَا أَرْسَلْنَا مِنْ رَسُولٍ إِلَّا بِلِسَانِ قَوْمِهِ لِيُبَيِّنَ لَهُمْ
 
Ubatizo wa Yohana ambao hata Yesu alibatizwa ilikuwa ni kama desturi ya waisraeli (wayahudi ) ilikuwa ni lazima ubatizwe kwa maji lakini ubatizo anaouzungumzia Yesu ni ile hali ya mtu kufanyika upya kutoka katika utu wake wa kale na kuingia katika utu wake mpya ambao yeye Mungu alikusudia kwa wanadamu,kwa hyo ukimpokea yesu kristo na kumuamini na kukiri kuwa ni mwokozi wa maisha yako hatua itakayofuata ni kubatizwa ukiwa na ufahamu wako vyema,na kubatizwa huku uambatana na Imani,na pia ubatizo huu sio kama ule wa Yohana ambao ilikuwa ni kama desturi ya wana Israel (wayahudi) ,ubatizo wa Roho mtakatifu ni ambao unafanya mtu na kumpa mtu badiliko maisha mapya, na uki rejea kwa maana halisi ya ubatizo ni kuzamishwa kwa maji na kuibuliwa kule kuzamishwa ni kama kufishwa kwa matendo ya uaribifu na kule kuibuliwa ni kufanya upya katika utu upya ambao kristo alivyokusudia na tendo hili liliambatana na Imani ndani ya mtu,na huo ubatizo wa waRoho mtakatifu ambao ni ile hali ujio wa Yesu Kristo kwa ajili ya wanadamu kwa kuamua kujitoa kwa ajili ya maisha yetu(kazi ya msalaba) ndipo akatuachia msaidizi ambaye ni Roho mtakatifu, wadau wengine wanaweza kujazia nyama Mahala nilipokosea
 
Ubatizo wa Yohana ambao hata Yesu alibatizwa ilikuwa ni kama desturi ya waisraeli (wayahudi ) ilikuwa ni lazima ubatizwe kwa maji lakini ubatizo anaouzungumzia Yesu ni ile hali ya mtu kufanyika upya kutoka katika utu wake wa kale na kuingia katika utu wake mpya ambao yeye Mungu alikusudia kwa wanadamu,kwa hyo ukimpokea yesu kristo na kumuamini na kukiri kuwa ni mwokozi wa maisha yako hatua itakayofuata ni kubatizwa ukiwa na ufahamu wako vyema,na kubatizwa huku uambatana na Imani,na pia ubatizo huu sio kama ule wa Yohana ambao ilikuwa ni kama desturi ya wana Israel (wayahudi) ,ubatizo wa Roho mtakatifu ni ambao unafanya mtu na kumpa mtu badiliko maisha mapya, na uki rejea kwa maana halisi ya ubatizo ni kuzamishwa kwa maji na kuibuliwa kule kuzamishwa ni kama kufishwa kwa matendo ya uaribifu na kule kuibuliwa ni kufanya upya katika utu upya ambao kristo alivyokusudia na tendo hili liliambatana na Imani ndani ya mtu,na huo ubatizo wa waRoho mtakatifu ambao ni ile hali ujio wa Yesu Kristo kwa ajili ya wanadamu kwa kuamua kujitoa kwa ajili ya maisha yetu(kazi ya msalaba) ndipo akatuachia msaidizi ambaye ni Roho mtakatifu, wadau wengine wanaweza kujazia nyama Mahala nilipokosea
Ahsante sana kwa ufafanuzi wako wa Ubatizo wa Maji na ubatizo wa Roho mtakatifu, bado nasubiri ufafanuzi kuhusu ubatizo wa moto
 
الاشتعال بما يفيد
عن أبي هريرةَ رَضِي اللهُ عَنْهُ قالَ: قالَ رسولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
{مِنْ حُسْنِ إِسْلاَمِ الْمَرْءِ تَرْكُهُ مَا لاَ يَعْنِيهِ}.رواه الترمذي
Hii Ni Aya ya majini Nini?
 
1 Wakorintho 1:19
Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
1 Wakorintho 1:20
Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?
1 Wakorintho 1:21
Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.

Mkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako ili upate kuwa ndani ya kweli yake na kuvuna matunda ya utukufu wake
 
Kufuta dhambi ya asili. Waliyotenda Adam na Hawa

Ahsante kwa majibu yako. Dhana ya Dhambi ya Asili si sehemu ya mafundisho ya Kiislamu. Waislamu tunaamini kwamba wanadamu wamezaliwa bila dhambi na wana nia ya kumpendeza Mungu. Tuna uhuru wa kuchagua, unaotufanya tupotee nyakati fulani, lakini Mungu yuko tayari kusamehe daima. Ikiwa wewe unasema unabatizwa kwa kufuta dhambi ya asili inamaanisha ADAM na HAWA hawakusamehewa madhambi yao na Mwenyezi MUNGU. Ila shukran kwa jibu lako
 
Back
Top Bottom