1. Kwanza kabisa napenda kukujuza Kuwa kauri ya kwamba Mtu huzaliwa mwisilamu akibatizwa ndiyo anakuwa mkiristo ni uongo. Lejea history ya uisilamu umeanza miaka 600 baada ya ukristo. Swali hapa kabla ya uisilamu kuja mtu alikuwa anazaliwa Kama Nani? Na kubatizwa anakuwa mkiristo.
2. Unachanganya Kati ya neno Moto na Roho Mtakifu. Maana yake Roho=Moto. Hivyo Roho Mtakifu pia huitwa upepo au moto. Rejea.
1.Waebrania 1:7
[7]Na kwa habari za malaika asema,
Afanyaye malaika wake kuwa pepo,
Na watumishi wake kuwa miali ya moto.
2.Matendo ya Mitume 2:1-3
[1]Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
[2]Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
[3]Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.
Hivyo Roho Mtakatimu ni upepo na ni moto.
Lakini nakukumbusha Kuwa Yesu akibatizwa kwa maji sema Kuwa ubatizo wake ulikuwa wa nguvu za Roho Mtakifu ambaye ni moto.
Rejea
1. Yohana 3:5-6
[5]Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
[6]Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
2.Yohana 3:5-6,22-23
[5]Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
[6]Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
[22]Baada ya hayo Yesu na wanafunzi wake walikwenda mpaka nchi ya Uyahudi; akashinda huko pamoja nao, akabatiza.
[23]Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa.
Yesu alibatiza kwa maji.
Pia mitume walibatiza kwa maji
Matendo ya Mitume 8:36-39
[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [
[37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
[38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
[39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.