TISS Ilikuwepo muda mrefu sana inawezekana kulikuwa hakuna sheria, lakini mimi nimeelewa uwapo wa TISS tangu miaka hiyo ya sabini. Kuna ndugu yangu mmoja alikuwa ofisa wa TISS wakati wa Nyerere, na alikuwa anaishi maisha kama yuko mbinguni. Kama uliwahi kumfahamu jamaa anaitwa Walingozi, basi huyo ndiye aliyekuwa chuma cha pua wa TISS.
Mwanozni mwa miaka ya themanini ilikuwa ni almanusra tu na mimi ningeinga TISS ila nadhani hawakupenda maisha yangu ya ujana wakati huo kutokana purukushani zangu nyingi sana za wakati huo. Ila Takuru walinifanya kuwa ripota wao kwa kipindi fulani ingawa bila malipo yoyote bali malupululupu tu- ambayo yalikuwa yananitosheleza haja zangu wakati huo.