P Funky Majani (Godfather wa Bongofleva) ni mzaliwa wa wapi? Je, ni mtanzania halisi au kachanganya?

P Funky Majani (Godfather wa Bongofleva) ni mzaliwa wa wapi? Je, ni mtanzania halisi au kachanganya?

Mkuu hao wote uliowataja ni fake. Diamond na Hasheem Kiingereza wamjuwa hivi majuzi tu na mpaka leo bado hawakijuwi vizuri ila wanajifanya hawajuwi Kiswahili....Ukisikia utumwa wa kiakili ni huu. Hasheem mpaka leo akiwa Marekani anaogopa kuongea na wamarekani weusi kuogopa kuchekwa kwa ajili ya lafudhi yake kuwa ngumu na Domo ndiyo kabisaaaa, yaani bora aongee tu Kiganda.
Hahahaaaaa jamaniiiiiiii!
 
Alikuwa na nguvu sana awamu ya JK, ndiyo maana alimpiga mtama TID Billicanas na hakutolewa nje wala kushitakiwa, ulaya issue kama hiyo anakulipa hela nzuri tu, pia yuko fit sana hata ukisalimiana na kwa kushikana mikono utalijua hilo, isitoshe ana jeuri ya pesa japo kiwango chake kwa sasa kimechukua kwa kula bata zaidi ya mazoezi.
Hakuwa na nguvu awamu ya JK bali alikuwa na nguvu wakati yupo NBA! Na huko kumtandika mitama TID hakuhusiani chochote na JK manake, tangu enzi za Mwarabu, na hatimae Mjerumani kisha akaja Mwingereza na hadi enzi za Nyerere na hadi kesho; watu wenye midomo kama TID walitandikwa na wanaendelea kutandikwa mitama!!
 
Vijana wengi wa Kitanzania hususan hawa millennials hupata shida kuongea Kiswahili kitupu kilichonyooka.

We jaribu kumsikiliza yule mwigizaji Lulu uone.

Jaribu tu kuwasikiliza wabongo fleva...hata Diamond naye siku hizi kaanza kuwa hivyo.

Yule mcheza kikapu Hashimu Thabiti ndo kabisaaa....utadhani hajazaliwa Dar au Tanzania. Huwa anapata shida sana kuongea akiwa anaongea Kiswahili.

Sijajua hasa tatizo ni nini lakini ninahisi mojawapo ya sababu ni kutaka kujifanya u wa hali na hadhi fulani [kwa kuchomekea sana maneno ya Kiingereza] na pia kutokujua vizuri lugha yoyote ile, iwe Kiswahili au Kiingereza.
hata wewe umo kwenye hili kundi
 
Habari zenu ndugu zangu
Napenda kujua historia ya huyu producer mkongwe hapa nchini nimeangalia interview zake mbalimbali nimevutiwa na uwezo wake wa kuelezea vitu pia huyu jamaa ana content Sana hababaishi.

Napenda kujua asili yake kwa sababu kwenye interview zake nyingi anaonekana kiswahili kumpa shida sana katika uzungumzaji wake kama sio mbwembwe.

Ukifuatilia interview alofanya na dj Lil omy wa times FM utagundua nilichokisema
Hivyo basi nakaribisha michango yenu kwa anayejua historia ya P-funky majani

P. Funk

Paul Majani


Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwa
Paul Matthysse
Pia anajulikana kama P Funk, Majani, Kinywele Kimoja, Mdachi nk.
Asili yake Tanzania
Aina ya muziki Hip Hop na Bongo Flava
Kazi yake Mtayarishaji
Ala Kinanda,Guitar, Kinakilishi
Miaka ya kazi mn. 1995 -
Studio Bongo Records
Ame/Wameshirikiana na Master Jay, Bonny Luv,Rajabu Marijani, Bizz Man, Boznia nk.
Paul Matthysse ( P Funk ) ni mtayarishaji wa muziki na pia mmiliki wa Studio ya Bongo Records iliyopo jijini Dar es Salaam, Tanzania.

P Funk a.k.a. Majani, ambaye ni nusu Mtanzania na nusu Mdachi, kama miaka ishirini iliyopita alikuwa na hisia za kupendelea muziki na pindi hadi kuamua kufanya kweli kuvutiwa kwake kupenda muziki ndio chanzo kikubwa kilichopelekea kufanikiwa katika muziki.

Kwenye miaka 1991-92 wakati yupo bado shule IST (International School Of Tanganyika. Alikuwa mtundu mtundu kwenye studio za pale shule.. kupiga- piga midundo mbali mbali ya hapa na pale na kufoka-foka(Rap music) na pia alikuwa mbele sana kwa kupiga musiki kwenye Pati mbali mbali.. na hapo alikuwa kupenda sana musiki kwa ujumla.



Yaliyomo
[1Elimu ya Muziki na Uzoefu Wake

Elimu ya Muziki na Uzoefu Wake[hariri | hariri chanzo]
P-Funk alikwenda kimasomo ya Mlio (sound) engineering kwa miezi 18 pale Amsterdam, Netherland kabla ajaingia kwenye kutayarisha muziki. Alikuwa anajua kitu anachotaka kufanya. Mwaka 1995 akiwa na vifaa vyake vichache alianzisha kampuni yake ya kurekodi muziki nyumbani kwake. Na ni katika kipindi hicho hicho neno ’Bongo’lilipokuwa linatawala katika misemo ya kiswahili cha mitaani na lilikuwa linaelezea hali halisi ya maisha ya Dar es Salaam na ndio kipindi hicho album ya Bongo ilipozinduliwa. Akiwa bado ni mtayarishaji muziki mdogo, amefanikiwa kupata umaarufu mkubwa katika fani ya muziki na hasa katika milipuko ya nyimbo zenye ladha ya Bongo.

Anakubali kuwa amepata sana utaalam na mbinu kutokana na kufanya kazi watayarishaji wengine wa muziki wa Kitanzania kama Master J, Bonny Love na Rico. Mawazo yake na namna ya kuyaoainisha na muziki ndio hasa ambacho kinafanya muziki wake ufanikiwe.

Tuzo Alizopata[hariri | hariri chanzo]
Wasanii Aliowainua[hariri | hariri chanzo]
Kwanza alianza kwa kumpandisha chati Juma Nature, ambaye ndio nyota wa nyimbo za Bongo Flava, akaendelea kwa kutayarisha santuri ya Solo Thang, AY, Zay B, Sista P, Mike T na pia alishawahi kufanya kazi na Professor Jay alipotoa santuri yake mwenyewe.

P Funk ana wasanii wengine wengi wanaotumia nembo ya kampuni yake katika utengenezaji wa albamu.

Pia Anajulikana Kama[hariri | hariri chanzo]
  • P Funk
  • Halfani
  • Majani
  • Kinywele Kimoja
  • Mkono wa mungu
Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani wa Afrika bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu P. Funk kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.




kazi ni kwako soma
 
hata wewe umo kwenye hili kundi
Ah wapi.

Mimi nina uwezo wa kuongea na kuandika lugha moja kwa ufasaha wa hali ya juu kabisa bila kuchanganya na lugha ingine.

Kama ni kimombo basi naweza kukiandika na kukiongea mwanzo mwisho.

Kiswahili nacho vivyo hivyo. Ikija kwenye Kisukuma ndo usiseme kabisa. Hiki ndicho huwa najivunia zaidi kukijua. Kwangu ni fahari ya aina yake ingawa zamani niliwahi kuchekwa na kudhihakiwa kuwa eti naongea 'kilugha'. Dokezo hapo ni kwamba ukiongea 'kilugha' basi wewe ni mshamba.

Kwa hiyo kwangu mimi ni tofauti kabisa. Huwezi kuniweka kwenye hilo kundi.

Halafu unajua nini? Watu huwa wanastaajabu na kubaki midomo wazi wanapogundua kuwa naweza kuongea Kisukuma tena kile cha Ntuzu kabisa bila hata kwakwaru.

Mimi ni namba ingine kabisa.
 
Cha ajabu ni kipi? Umaskini wako ndio umekufanya uishi mbali na wazazi wako.

Bakhresa mpaka leo anakaa na watoto wake wote pale Masaki.

Akili za kimaskini ni mbaya sana, nimefanyakazi KLM na mama yake Paul ni swahiba wangu mtoto ninayemjuwa mimi ni Paul na mama yupo mwenyewe hivi kuna ubaya gani mama kukaa na mtoto wake?

Chunguza kwa makini hata wahindi wanaishi kifamilia, hata huko mamtoni nimezunguka sehemu nyingi matajili kwenye Mansion zao wanaishi kifamilia.

Hizi dhiki zetu za kumaliza sabuni bafuni na kuongezeana gharama za chakula ndio zinasababisha kijana mdogo eti naye kapanga chumba!
Poverty.
Mbona povu p funk
 
Back
Top Bottom