TANZIA Pacha waliotenganishwa, mmoja afariki dunia

TANZIA Pacha waliotenganishwa, mmoja afariki dunia

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
FWaAS9kXoActJKm.jpg
Mtoto mmoja kati ya waliofanyiwa upasuaji wa kutenganishwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Neema amefariki dunia wakati akiendelea na matibabu Jumapili Julai 10, 2022.

Taarifa ya Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa MNH, Aminiel Aligaesha imeeleza kuwa hali ya Neema ilibadilika ghafla akiwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU).

Aminiel Aligaesha amesema: "Nasikitika kukufahamisha kuwa mtoto Neema ambaye alitenganishwa na mwenzake Rehema amefariki jumapili ya tarehe 10 Julai saa 3 asubuhi. Akiwa ICU hali yake ilibadikika gafla, madaktari walijitahidi kurudisha hali yake bila mafanikio na hatimaye kupoteza maisha. Twendelee kumwombea Rehema ambaye bado yupo ICU ili Mwenyezi Mungu amjalie afya njema. Bwana alitoa na Bwana ametoa, jina lake lihimidiwe sana."
 
Operation ilikuwa successful wataalamu wetu kwa kuongozwa na Mungu wanapaswa kupongezwa, hiki kilichotokea hatupaswi kuwalaumu hata kidogo, Bwana amfariji mama wa mapacha hao na mmoja aliyebaki amlinde na kumpa maisha marefu
Miezi saba watoto wazima kabisa wamefanyiwa upaduaji wiki nyingi....
 
Nilitaka kushangaa tangu lini Tanzania tukawa serious kiasi hiki na kufanya vitu vikafanikiwa.
Sisi tuko bora sana kwenye kimasihara lakini vitu vya maana mhh...
Msinipopoe mawe wakuu
Hivo ulisubiri tatizo litokee ndo uanze kukosoa?,punguza ujuaji wa kijinga hata huko unapoona ni bora huwa mambo kama haya yanatokea sana tu[emoji706][emoji706][emoji706]
 
Kwa mbwembwe na matangazo kama yote Walikataa kuwapeleka watoto watu India wakajitutumua , ona sasa matokeo yake , mnafanya majarbio kwenye maisha ya watu , hii imetokea pia majuzi , mwamba kaugua ghafla tumefika hospital fulan , daktar amefanya kaz yake , daah Wana tukaona hapa chenga , inabd tumkimbize hospital kubwa Zaid , aisee daktar si akazingua et anasema atakaa fresh tuuu , aisee kufika jion mchizi wetu akakata moto tulijilaumu kinyama kumsikiliza daktar wa mchongo
 
Back
Top Bottom