TANZIA Padre Paul Haule ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele

TANZIA Padre Paul Haule ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele

Mhashamu Askofu Mkuu Jude Thaddaeus Ruwa'ichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam anasikitika kuwatangazia kwamba leo tarehe 18/08/2021 saa 10.30 jioni hii mpendwa wetu PADRE PAUL HAULE ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele.

Akiwa katika matibabu ktika Hospitali ya Kardinali Rugambwa Ukonga.

Tutataarifiwa taratibu zingine za mazishi zitakapopangwa. Tumuombee apumzike kwa amani.

Pd. Vincent Mpwaji
Chancellor.

Marehemu Alikuwa Mkurugenzi wa Tumaini Media


Mkuu Trillion kwanini umeweka emoji ya kucheka kwenye habari ya msiba?
 
Kiongozi bora ni yule anaye watangulia kondoo kwa mbele kama magufuli hata kama akifa siyo huyo mama mwoga anayejali maisha yake zaidi kuliko taifa sisi tumeamua kumuenzi magufuli kwa kutokuchanjwa hata kama tutakufa hadi itakapo patikana chanjo ya akika ya covidi
Chanjo haina matatizo kihivyo mkuu, ni vile chanjo zenyewe hamna, na uwezo wa wakuzinunua haupo. Kelele tu zimekua nyingi.
Virusi Delta vikukute huna chanjo mwilini inakuua tu. Wenye chanjo wataumwa kidogo na kupona.

Achana na legacy za hovyo za Mwendawazimu yule.
 
Hii imenifanya nikaangalie video yake ya mwisho pale st peters. Magufuli alivyomsema jaji Mihayo kisa kavaa mask. Na siku ina masaa 48.Ila Mungu jamani acha tu.
Jaji mzima akageuka kitukoo[emoji1787][emoji1787][emoji1787].na wapambe wa mwenye heri jiwe wakashangiliaaa
 
Acha masihara mpaka kuna wadosi kadhaa waliokuwa wamechanjwa wamevutwa kwa korona ila hutaambiwa. Ni matajiri wakubwa. Magufuli hapaswi kubezwa.
Siwezi kumbeza mtu aliyededi kwa uzembe wake mwenyewe. Mzee alizoea kuropokea wabongo akadhani na kirusi pia kinaropokewa... kikamtendea miujiza fasta...
 
Wakuu,

Habari hii pia sikuiona JF, kama ipo mods watanisaidia ku-merge. Nia yangu ni kuweka rekodi hapa JF.

IMG_5418.jpg



PAROKO Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Petro ‘St Peters’ Jijini Dar es Salaam, Padri Paul Haule, amefariki dunia Agosti 18, 2021 saa 10:30 jioni wakati akitibiwa katika Hospitali ya Kardinali Rugambwa iliyopo Ukonga.

Mbali na kuwa paroko msaidizi, Padri Haule alikuwa Mkurugenzi wa Matangazo Radio Tumaini.
 
Back
Top Bottom