Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki nchini (TEC) Padri Charles Kitima amewaasa wanasiasa kujirekebisa kwani ipo siku vijana wataleta mapinduzi miaka michache ijayo. Ameyasema haya kwenye mjadala wa maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Demokrasia Septemba 15, 2022.
"Msipo jirekebisha ninyi wanasiasa wa vyama vyote, Vijana watakuja kuleta mapinduzi miaka kumi, ishirini ijayo hamtayakwepa. Hawana kazi, mnawaibia kura, mnawayumbisha. Na wamekuwa wanakaa kimya sababu wanatuheshimu sisi wazazi wao na viongozi wao, lakini hawatavumilia milele.
Ameshauri tabia za kidemokrasia kuanzia ngazi ya familia, ukoo, kijiji, makanisani na misikitini zianze kuonekana ili zilete uhalisia hadi kwenye mazingira ya siasa.
"Mfano hapa Tanzania, sisi wote hapa ni waumini, uwe Mkristo au Muislamu. Tanzania sasa hivi mniambie ninyi Wakristo ni nani anaye mwambia Mwenyezi Mungu nimetenda dhambi kwa kuiba, au kwa kuhonga wajumbe wa kamati? Ni kama tulishasema kwenye siasa hakuna nini? Hakuna dhambi"
Ameongeza kwa kusema kuwa kama watanzania, tuna kazi kubwa sana ya kujenga zile tabia za kidemokrasia ili kuhakikisha kuwa watu wanayapata madaraka na kuwaleta watu haki zao.
"Sasa hizi tabia za kidemokrasia ambazo vilevile zinajengwa na taasisi za kidemokrasia, unaongelea tume ya uchaguzi ni namba moja kwa sababu ni kwa njia ya uchaguzi ndiyo watu wameamua kusalimisha uwezo wao wa kujitawala kwa hiyo tusiwaingilie kwenye dhamiri zao"
Katibu mkuu wa Balaza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania Padre Kitima ameonya kwamba uminywaji wa demokrasia una mwisho mbaya kwa sababu miaka si mingi vijana watachoshwa na hali hiyo na kwayo itawalazimu kufanya mapinduzi ya kidemokrasia.
Kama 'Genius' huyu, Mhadhiri wangu wa Media Law SAUT na aliyekuwa Vice Chancellor wangu SAUT nilipokuwa huko 2006 - 2009 amesema huu Ukweli Mtupu Mimi GENTAMYCINE ni nani nipinge au nimpinge?
Kasema miaka 10 hadi 20 ijayo maana yake kutakuwa na vijana wengine, hawa wanao bet sasa watakuwa wazee.
Unadhani Padre ana kichwa cha panzi kama wewe.
Vijana je ajira mnazo? Je, mnapata kazi hata kama hamna kadi za chama? Vijana mnaridhika huku mkilalamika ajira hamna na huku mumesoma na madgree mnayo lakin wazee waliokula mema ya nchi wakila teuzi baada ya kustafu? Maswali ni mengi ila kwa leo niishie hapa.
Hapo mwishoni aliposema kukosekana kwa maadili kwenye kuendesha chaguzi hapa bongolala huhitaji hata tochi kutafuta gizani, ukichukulia uchafuzi wa 2020 ambapo chama fulani kilijitwalia asilimia 99.9999 ya ushindi.
ameonya kwamba uminywaji wa demokrasia una mwisho mbaya kwa sababu miaka si mingi vijana watachoshwa na hali hiyo na kwayo itawalazimu kufanya mapinduzi ya kidemokrasia.
Hivi anadhani betting inahimizwa kwa makosa? Nikuwafanya wasijitambue wasiwaze mustakbali wao na Taifa nadhani. Mambo mengi yanapangwa lakini uzuri siyo yote yanapangwa na wanadamu.
Mkuu Suzy Elias, tafadhali jua kuwa hayo ni maoni ya Padre Kitima binafsi na si ya Baraza la Maaskofu kwa ujumla wao. Aliyasema hayo jana (nilikuwepo pale ukumbini) akiwa kama mchangiaji mkuu wa mada pamoja na Sheikh Ponda, Dr. Ananilea Nkya na Sam Awami.