Paka kuchukuliwa kama mwanafamilia kwa kutengewa bajeti yake, inakubalika?

Paka kuchukuliwa kama mwanafamilia kwa kutengewa bajeti yake, inakubalika?

FANYENI KAZI NYIE
Hahaha Poland hpo nakumbuka kuna mke wa jamaa mmoja mbongo
Ye dili zake kuuza paka anawauza bei kweli
Kwao kuna mipaka kibao wa kila aina
Wako wenye macho meusi,blue,kijani,nyekundu,njano etc
😂😂

Ova
 
Zamani nilikuwa nafunga mbwa kwa ajili ya kuwinda na ulinzi ,paka naye alikwepo ila anajitafutia chakula kivyake maana siyo panya tu anakamata njiwa ,hadi kware .Ila jioni na asubuhi mnapokamua ng'ombe anakuja pale kulia anataka maziwa tunampa hata nusu lita anajipigia zake anaondoka but maisha ya Sasa yamebadilika ,paka na mbwa wamekuwa kama mapambo tu,unakuta paka hali nyama mbichi anataka vilivyokaangwa

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Na akila vya kupikwa si ndio hawezi kuua panya kabisa
 
Alafu unakuta ndugu yako anakuomba pesa ya chakula au mtaji, unamkazia na kumpa paka msosi
 
Paka yule ana confidence balaa yani unamtofautisha na paka wetu. Jamaa kamtishia kamfukuza ila wapi, mi nimeitwa nikarekebishe kitu narudi nakuta jamaa analazimisha paka atoke. Ni wale watu hawana exposure unamuita aje kukusaidia kazi za kutumwa. Haelewi thamani ya paka kwa boss, walipokuja wenyewe wakaongea Kihindi akawafuata

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Paka wanajiona sana hao wadudu, wana nyodo za kifala sana. Unaweza mwita akakubinulia midomo akakusonya akaendelea kuangalia tv.

Ila yeye akiwa na shida zake mfano njaa au anataka kitu chochote muda wote miguuni kwako anajipitishapitisha na kujiparaza kama anataka kupigwa ukuni. Nyaaaaaau nyaaaaau nyokololo pumbavu zao..... [emoji34][emoji34][emoji34][emoji34]
 
Paka! Ni mnafki sana.

Paka anatumika hata na viumbe visivyoonekana kwa macho.

Nakumbuka kuna tajiri mmoja ( sitamtaja ) ana paka na kuku pale kwenye Yard yake masaki.

Huyo paka kwanza ni mkubwa ki umbo, yaani, yule mpuuzi ana Sofa lake na ana kitanda chake, yule paka amewekewa mfanyakazi.

Jengo ni kubwa sana na Tajiri haishi pale bali pale ana ofisi ndogo mle ndani. Wanaoishi pale ni huyo paka, kuku, njiwa na mfanyakazi.

Maisha ya mule ndani ( Boss Paka ) ukiingia kuna Sofa moja kubwa sana la langi ya dhahabu( sofa hili ni la huyo paka, ole wako ukaenda kukaa atakukata jicho hilo alafu haogopi yaan atawaka apo mpaka utainuka, jikoni yamejaa makopo ya chakula chake na cha kuku. Yaani yule paka ( sijui mm mpaka leo siamini kama kuna paka anayeishi kitajiri kama yule mpuuzi na kwanza mpaka hapa siamini kama ni paka ama Power Bank ya yule Tajiri wa mabasi.


Saa asubuhi anakula Samaki wa mchemsho, mchana kuna mavyakula wanachanganya ni vya kopo na maziwa.

Jioni saa kumi, anakula tena Nyama choma na maziwa, kisha anaenda zake kulala chumbani kwake, paka ni kauzu sana kauzu kupitiliza yaani hataki mgeni mle ndani ana jicho baya kinyama yaani mkiangaliana tu unajua huyu hafurahishwi na ujio wangu.

Saa kumi hiyo pia ni Muda wa kuku na njiwa kula.

Hawa wanapewa mikate 10, mbegu za bangi na mtama..huu mtama ni kilo 5. Kila siku..lakini hii si kesi kesi ipo pale kwa Paka Paka ana roho mbaya sana, nilijaribu kudodosa yule mfanyakazi anasema yule paka kwa sikuanatumia 40 kwenye chakula...


Kwa anayemjua Boss yoyote mwenye mabus ambaye ofisi yake ipo Masaki na Profile yake ktk whatsapp kaweka picha ya Boonge la Paka kuubwa, basi ajue huyo paka anakula elfu 40 kwa Siku, kila siku namaanisha. *****

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Paka wanajiona sana hao wadudu, wana nyodo za kifala sana. Unaweza mwita akakubinulia midomo akakusonya akaendelea kuangalia tv.

Ila yeye akiwa na shida zake mfano njaa au anataka kitu chochote muda wote miguuni kwako anajipitishapitisha na kujiparaza kama anataka kupigwa ukuni. Nyaaaaaau nyaaaaau nyokololo pumbavu zao..... [emoji34][emoji34][emoji34][emoji34]

Hayo maringo ndio uzuri wake
 
Paka ni wastaarabu ila ni pia ni mawaki laana, Uwaki wao ni pale ukimnyima msosi anakua mwizi balaa tena anatafuta na genge la paka wengine wezi wanakua na kakikundi chao wanakaa kabisa had maskani alaf usiku anakuja nao hapo home kufunua masufuria.

Alaf ni bingwa wa kukariri mitaa hata ukamtupe wapi atarudi tu home labda umteke umfunge macho ndo ukamtupe
Weeeee, wale mabwege wameumbwa na GPS tracking system. Kuna paka tulimtia katika kiroba tukatoka nae tabata st. Mary kule tukaenda mtupa kule kwenye daraja la kinyerezi kiroba kikiwa wazi ili aweze kutoka.

Yule fala wiki kadhaa baadae akarejea tena safari hii akiwa na demu na akaja wakazaa watoto.

Paka wapumbavu sana hawa wanyama [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mbwa siku zote hua ana behave Kama mtumwa lakin Paka yeye anajionaga Don.

Ndo maana wanasema hamna rafiki mzuri Kama mbwa lakin sio li Paka

Mzee umenichekesha, yaani paka anajiona kama Don... mimi kuna siku nilienda Bar moja hivi kula nyama, sasa kuna paka wakaja mmoja anaonekana kibonge hivi, si nikamtupia mfupa ambao kwa kweli ulikuwa na nyama kiasi, akaniangalia akanishusha halafu akasonya, huyoo akaondoka zake akijitingisha.. kwa hiyo nimekuelewa kabisa.. hawana maana.
 
Mi haya madudu yananikera usiku yakianza kugombana, yaani usiku wa manane yanalia kwa sauti kali kinoma, ukiyachungulia unakuta ni jike na dume yanataka kumbotana,
Hivi hawa viumbe hua hawawezi kupigana miti kimyakimya kweli au ndio makusudi tu kukarahishana usiku wa manane.
 
Back
Top Bottom