Panya Magawa astaafu kazi ya kufichua mabomu kimataifa

Panya Magawa astaafu kazi ya kufichua mabomu kimataifa

Panya wa Tanzania mwenye sifa ya kufichua mabomu kimataifa astaafu Cambodia Magawa (panya) aliyejishindia tuzo kwa ushujaa wake anastaafu katika kazi yake ya kufichua mabomu yaliotegwa ardhini.

Kila ugunduzi alioufanya ulipunguza hatari ya kuumia au kifo kwa watu wa Kambodia. Katika kazi ya miaka mitano aliyofanya Hadi leo Magawa amefanikiwa kugundua mabomu 71 yaliotegwa ardhini pamoja na vilipuzi kadhaa nchini Cambodia na kumfanya kuwa HeroRAT aliyefanikiwa zaidi wa APOPO

Wasimamizi wake wanasema kwamba panya huyo mwenye umri wa miaka saba ameanza kupunguza kasi yake akielekea kuwa mzee na anahitaji kuheshimu mahitaji yake

Magawa ni panya mkubwa wa kijeshi wa kiafrika aliyezaliwa nchini Tanzania mnamo Novemba 2014. Alikulia katika kituo cha Mafunzo na Utafiti cha APOPO nchini Tanzania ambapo alijifunza jinsi ya kupata vilipuzi kwa kutumia hisia zake za ajabu za kunusa. Magawa kisha alihamia Siem Reap huko Cambodia mnamo 2016, ambapo alianza kazi yake yenye mafanikio.

View attachment 1808755
Watoto walio zaliwa jana waitwe MAGAWA.

PILI, serikali impe BENZI LAKE na kumjengea nyumba.
 
Nianze kwa kupongeza juhudi za SUA mpaka walipofikia na mradi huu wa Panya.

Kwani mpaka sasa wanaweza kutambua vimelea wa TB, kutegua mabomu ya aridhini n.k.

Pamoja na hayo ningetamani kusikia Panya hawa hata wameanza na shughuli nyingine tofauti tofauti.

Kwa mfano wangewezeshwa waweze kukusanya taka za plastiki, hasa hivi vya nailoni.

Ifike mahali kila Kata nchini iwe inakodisha idadi kadhaa ya Panya kwa mwezi au mwaka kwa ajili ya shughuli hizo.
 
SUA na tafiti za haja na uhakika. UDSM na tafiti za robot la mabati
 
Fahamu Panya Mtanzania Magawa ambaye amestaafu kazi ya kutegua mabomu baada ya kufanya kazi hiyo mataifa mbalimbali kwa weledi mkubwa ambapo mpaka anastaafu ametegua mabomu zaidi 109.

Magawa ameshinda medali ya dhahabu kwa uwezo wake wa kazi. inaelezwa kuwa kwa sasa ataendelea kusalia Cambodia baada ya kustaafu kutokana na kuhofia afya yake wakati wakusafiri. Lakini chumba chake na sebule kikiwa na CCTV- Camera pamoja na feni kipo.

Jina la panya magawa ambalo ni jina la rafiki yake babake Pendo Msegu (Mkufunzi) likimaanisha Mtoaji, amestaafu akiwa na umri wa miaka 7. Mkufunzi Pendo anaeleza kuwa Magawa alikuwa wa kiume lakini hakuwa kwenye mahusiano (alikuwa single) , licha ya kuwa single hakuwa na mtoto pia . Lakini anawadogo zake ambao pia wanaendelea na mafunzo hadi sasa.

[emoji232][emoji232][emoji242][emoji242][emoji242][emoji242]

FB_IMG_1624521279444.jpg
 
Back
Top Bottom