Papa Francis, Lissu, machampioni halisi wa haki, usawa na uhuru duniani

Palestina palestina.

Unakera
 

1. Mkuu niliandika uzi huu:

Mbowe, Lissu wafundeni wafuasi Falsafa ya Chama

nikiugulia hizo #7 na #8 mawazoni mwangu kwa maana yake kamili.

2. Ya kwamba:

Kama Maji Maji au Mau Mau ilikuwa halali, iweje lawama kwa wapalestina?

Huu nao ukiwa Uzi mwingine wenye mauzui hayo hayo!

3. Ni aibu kuwa tumejikita kuwa waumini wa dini na watu badala ya kuzijua haki zetu na kuwa waumini nguli wa "usawa, uhuru na demokrasia."

4. Inatia moyo kuwa wakristo na waislam wanaiiishi imani yao kuhusu mambo ya LGBTQ kiasi kuwa kwenye hili wako pamoja, hata dhidi ya Papa kama kina Bujibuji Simba Nyamaume (bila kujali dini) wanavyo jitanabaisha; bila kuwa na hofu!

5. Kama #4 hapo ni hivyo kwanini sisi tusiwe na misimamo yetu madhubuti na hata kuwakabili Lissu, Mbowe au samiana hata kuwakemea au kuwataka kupisha njia au hata viti, kama wakithubutu kutaka kutanga mbali na misingi yetu imara ya imani?

6. #5 hapo siyo kuwa kIna allen kiwelella, Erythrocyte, JokaKuu, Retired, imhotep nk watakwambia unataka kuonja sumu kwa ulimi na kusimama dhidi ya wenye uthubutu huo?

7. #5 hapo, kulikoni kuwaacha viongozi wetu au awaye yote kukiuka misingi yetu ya uhuru, haki, usawa, au demokrasia Kwa kujua au kutokujua, huku tukikenua kwa uchawa chawa tu kama wa akina Lucas mwashambwa, johnthebaptist, au Kamanda aliechoka; kama inavyotokea kwenye mengi uchwara ya kikristo na kiislamu?

8. Kwani ni siri kuwa wakristo brainwashed kama wewe na MK254 labda ni mburula, mazezeta, viazi mbatata kupitiliza labda kuliko hata wale(ISIS, Alshababu nk) wa kiislam wa kufanana nao?

9. #5 hapo kwa nini mawazo ya yeyote yasipimwe kwa hoja za msingi, kiasi hoja za kijinga hata kama ni za Mbowe, Lissu, Papa, Samia au binadamu awaye yote zipimwe dhidi ya hoja za wengine si Kwa sura au nafasi ya mtoa hoja?

10. Tunahitaji uumini mkomavu uliotukuka baina yetu kama huu:



Vinginevyo labda tukacheze gombesugu tu ndugu zangu kwani tunavyofanya sasa kama viongozi wetu wenyewe ni aina za kina Mpaji Mungu na kelele zao za vyura.

11. Imani zajengwa kwa mafunzo yenye kueleweka; kama Mbowe na Lissu wanalipuuza; maoni ya FaizaFoxy kwako kuhusu Haji Duni yasikilizwe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…