Pascal Mayalla alimtabiria Paul Makonda kuwa mgombea urais wa CCM 2025. Je, unabii wake utatimia?

Pascal Mayalla alimtabiria Paul Makonda kuwa mgombea urais wa CCM 2025. Je, unabii wake utatimia?

Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2020 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
Kwa vile 2025 bado, tuendelee kusubiria, ila sasa kuna tatizo hili
Wakuu ebu tujadili kidogo

Vurugu Kubwa zimezuka Siku ya jumatano ya tarehe 09 March 2022, Kufuatia Ugomvi wa Kugombania nyumba ya ghorofa mbili ambayo Kila mmoja, Paul Makonda na Gharib Mohammed Bilal anadai ni mali yake

Ugomvi huo Umezuka mpaka kufikia hatua ya Paul Makonda kurushiwa risasi zaidi ya 8, baada ya Gharib Mohammed Bilal Kuondoa walinzi na mafundi wa Paul Makonda kisha Kuweka Walinzi wake na Kumzuia Paul Makonda Kufika katika Kiwanja namba 60 Kilichopo mtaa wa Regent Estate Eneo la Mikocheni.

Gazeti na MwanaHabari Lili fanikiwa kuwahoji baadhi ya Watu walioshuhudia tukio hilo la kushangaza, ambao waliokwepo eneo la tukio akiwemo mwenyekiti wa mtaa ambaye alisogea mahala hapo mara baada ya Kusikia milio ya risasi kwa muda mrefu.

Baada ya mwandishi wetu Kufanya Uchunguzi wa Kina Juu ya Paul Makonda ambaye aliwahi Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Gazeti letu limebaini kuwa Kiwanja hicho ni Mali yake halali ambayo ameuziwa na Gharib Bilal terehe 18 november mwaka 2013 kwa Hati za mauziano wakati Makonda hajawa hata Kiongozi wa Serikali Bado, Wakati huo mkewe ndiye aliyekuwa anafanya Kazi Katika shirika lisilo la kiserikali la IFAKARA HEALTH INSTITUTE

Gazeti la MwanaHabari limefanikiwa Kuona nyaraka hizo mbalimbali , ambapo Gharib Mohammed Bilal alisaini Mkataba wa mauziano na Paul Makonda chini ya Kamishina Wa Kiapo Wakili Ibrahim Shinen

(pichani ni Mkataba wa Mauziano ya Kiwanja na Picha za Garib Bilal na Paul Makonda, ukiithibitishwa na Kamishina wa viapo wakili Ibrahim Mashinen)

Uchunguzi wa Gazeti la MwanaHabari umebaini kuwa Paul Makonda na Gharib Mohammed Bilal Wanafahamiana kwa Muda mrefu sana kabla hajawa Kiongozi wa Serikali, Wakati wa awamu ya Nne ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete

pia Gazeti la MwanaHabari limeona nyaraka nyingine ambazo zimesainiwa na Mke wa Gharib Bilal ambaye ni Bi Salha Islam Sahaag ikimruhusu na Kutoa idhini kwa Paul Makonda Kubadili hati ya Umiliki ambayo pia Gharib Bilal alimkabidhi Makonda kama Sehemu ya mauziano yao mbele ya Kamishina Wa viapo wakili Ibrahim Shinen Mwaka huo huo 2013
(Pichani ni Nyaraka ya Kuridhia Kubadili Hati Iliyo ikiwa na Picha ya Mke wa Gharib Mohammed Bilal)


Katika hali ya Kushangaza Gharib Mohammed Bilal ameibuka ghafla wakati huu na Kudai Kiwanja ambacho alimuuzia Paul Makonda ambaye tayari ameshajenga Jengo la Ghorofa mbili za makazi zaidi ya familia moja katika Kiwanja hicho kuwa bado ni Mali yake.

Kitu ambacho kimezua Maswali Kwanini sasa.? na Muhusika alikuwa wapi wakati Kiwanja hicho kimeanza Ujenzi zaidi ya miaka 6 nyuma mwaka mmoja baada ya mauziano mpaka Leo Jengo linakaribia Kuisha.

Uchunguzi wa Gazeti umebaini Kuna Wanasiasa walionyuma ya mpango huu wa kumdhoofisha na Kuhakikisha Paul Makonda

Baadhi ya watu Walio karibu Gharib Mohammed Bilal kwa muda mrefu wa Wameshangazwa na uhasama huo, kwa sababu wanawahamu familia ya Gharib Mohammed Bilal na Paul Makonda ni Familia rafiki kwa muda Mrefu ambazo zimekuwa zikisaidiana kwa raha na matatizo

Watu hao wanasema kuwa Naibu Waziri mmoja wa awamu ya sita kwa Jina la Ridhiwani Kikwete ndiye anaye mchochea mfanyabiashara huyo Kupora nyumba ya Paul Makonda na Kisha kutaka kumilikishwa yeye

Aidha Gharib Bilal anatajwa pia katika Kile Kinachodaiwa mkakati wa Kumdhalilisha Paul Makonda kwa Kufadhili Kesi dhidi ya Pual Makonda ambayo imefunguliwa na mwanasiasa mmoja wa Upinzani ambaye amekuwa kwenye Vita na Paul Makonda yeye na magazeti yake kwa ufadhili wa pesa za Gharib Mohammed Bilal kama Sehemu ya Kumkomoa na Kumdhalilisha Paul Makonda

Baada ya kuona Kesi ile haina tija na haija fanikiwa anachokitaka cha Kumdhalilisha na kumdhoofisha Paul Makonda

Sasa Gharib Mohammed Bilal ameingia Ulingoni yeye mwenyewe mchana kweupe kwa Kutaka kupora mali za Paul Makonda ikiwemo Jengo la ghorofa mbili la Kiwanja namba 60 Mtaa wa Regent Estate, Mikocheni kisha Kumpatia Naibu Waziri wa Ardhi Ridhiwani Kikwete mali hiyo.

Mkakati huo Ulinaswa Kufuatia Kikao cha January 15 2022, Siku saba baada ya Ridhiwani Kikwete Kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Gharib Bilal alimuita mwanasiasa huyo Katika moja ya Majengo yake (Appartment) anazomiliki Masaki kwa ubia wa Kampuni ya GSM na Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete ambapo mtoto wa Rais Mstaafu Miraji Kikwete anaishi katika jengo hilo

Kikao Kilikuwa ni Kuhusu Kupora jengo la Paul Makonda Mikocheni kisha Kumkabidhi Ridhiwani Kikwete kama atafanikisha Mpango huo ambapo Gharib Bilal amenukuliwa akisema "Kuliko yule Mbwa akae pale Kwemye Kiwanja nilichomuuizia, Bora Uchukue wewe, Kama akitaka pesa yake ya Kiwanja nitamrudishia"

Kazi ambayo Ridhiwani Kikwete alienda Kufanya na Kutoa hati nyingine kwa Jina la Gharib Mohammed Bilal mbali na Kuwa hati ya mwanzo Gharib Bilal alimkabidhi Paul Makonda na anajua ipo wapi ila walitengezea nyingine kwa kisingizio cha ya Kwanza imepotea .

Naibu Waziri Ridhiwani Kikwete kupitia Wizara ya Ardhi alitoa hati nyingine kwa Jina la Gharib Bilal tarehe 31 January 2022, siku 22 baada ya Kuapishwa Kushika nyadhifa hiyo Wakati Waziri Wa Ardhi Angelina Mabula akiwa mgonjwa Kitandani na bado ajaapishwa kuanza kazi Rasmi.

Baada Ya Paul Makonda kutaarifiwa Mchezo huo na Wasamaria Wema katika Wizara ya Ardhi, alikwenda Wizara ya Ardhi na Kuonyesha Nyaraka za Mauziano na Makabidhiano Wizara ya Ardhi, kiasi Kupelekea maafisa wa Ardhi Kujiridhisha na Kuweka zuio la hati Mpya iliyotoka kutotambulika Kisheria (Caveat)

Watu Walio Karibu na Naibu Waziri huyo wa Ardhi wanasema, Mwanasiasa huyo aliapa Kusaidia mkakati wa Kumdhoofisha na Kumdhalilisha Makonda kama Sehemu ya Kulipa Kisasi kwa Mwanasiasa huyo Kufuatia Kutajwa kwake katika kashfa ya Kujihusisha na madawa ya Kulevya wakati Ule Paul Makonda akiendesha operesheni maalum ya Kuwataja hadharani watu wote wanaojihusha na usafirishwaji na uuzaji wa madawa ya Kulevya


Mwenyekiti Wa mtaa wa Regent Estate,Mikocheni amekiri katika Kikao Kilicho fanyika katika Jengo hilo mara baada ya vurugu na Kurushiana risasi Kilicho fanyika Chini ya Kamanda wa Polisi Wa Wilaya ya Kipolisi ya Oysterbay aliyetambulika kwa Jina moja la Wendo, Kuwa wao manamtambua Paul Makonda kuwa Mmiliki wa Jengo hilo kwa sababu Wamekuwa wa Kumuona Mtaani hapo anajenga na Kuleta Vifaa Vya Ujenzi kwa zaidi ya miaka 5 iliyopita

Alisema "Makonda ameshiriki Katika Kukarabati hata hizi barabara za mtaa huu, Katika Kuleta vifusi na hii lami Unayo iona hapa ilikupata urahisi wa Kufika katika Jengo hili"

Gazeti limewahoji pia baadhi ya Viongozi wa Serikali ambao hawakutaka Kutajwa kwa sasa, wametoa Ufafanuzi kuwa Serikali Inafahamu mikakati yote michafu dhidi ya Paul Makonda ni Visasi na udhalilishaji kwa sababu wao kama Serikali Walitoa wito wenye Ushahidi Kamili wa Kuporwa mali Kwenda Takukuru Kufungua malalamiko lakini Hakuna hata mmoja aliye fanya hivyo.

Badala yake Watu wamekuwa Wanatumia mitandao ya Kijamii na njia nyinginezo, Wakati Swala la Ujenzi Wa Nyumba ya Makonda Serikali Inafahamu kupitia Fomu za Umiliki wa Mali kwa Viongozi wa Umma na mara Kadhaa Vyombo Vya Dola Vimefika eneo la Ujenzi kama Sehemu ya Utejelezaji majukumu Yake asingeweza Kujenga pale alafu Serikali isijue, Kwa sasa Makonda anakaa katika nyumba za Kupanga za Serikali (TBA) pale Oysterbay

Wadau wengine wamekerwa na Madai ya Garib Mohammed Bilal kumuhusisha moja kwa moja Paul Makonda na Hayati Rais John Pombe Magufuli kama Sehemu ya kulipiza Kisasi kwa Serikali Ya awamu ya TANO Kupitia Makonda ambaye aliwahi Kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam.

Wengi Wana amini Serikali ya awamu ya tano ya hayati John Pombe Magufuli imemsaidia sana Garib Mohammed Bilal hasa katika Ugomvi wake wa familia baada ya Kushutumiwa Kumwaga tindikali na Kaka yake Said Mohamed Saad ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Home shopping Center kisha kuhamisha Umiliki wa mali za Kaka yake akiwa Kwenye Matibabu huko Nchini Dubai mpaka kufikia Ndugu hao Kutaka kuuana

Serikali ya awamu ya tano imepata lawama nyingi sana Juu ya kumkingia kifua Gharib Mohammed Bilal katika Maswala ya Ukwepaji Kodi, Utoroshaji wa makontena bandarini na tabia ya Kubadili Majina ya Kampuni kila kukicha wengi Wanahisi Serikali ilimbeba sana, hastahili Kuonyesha Chuki kama anayo onyesha Sasa.
Asante Sana kwa taarifa hii, naomba Mimi Mwanajeiefu mwenzenu, niwe mtu wa kwanza kuwajulisha kuwa hii vita ya kutaka kumdhalilisha mpakwa mafuta wa Bwana, Paul Makonda, sasa ndio mwanzo WA mwisho wa hasidi huyu!. Karma ndio itamaliza kila kitu. Simaanishi Makonda ni malaika, bali, ni binaadamu kama binadamu wengine, hakuna mkamilifu, hivyo na yeye kuna makosa ametenda na tayari karma imeisha mshughulikia, hivyo kwa maonevu anayotendewa na hasidi huyu, ni Mungu, Baba ndiye atamlipia.
Kwanza mafanikio yake ni kutoka kwa Mungu. Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Kisha, Wale mnaosubiri kwa hamu Makonda atumbuliwe, mtasubiri sana!. Ukiwa ni mpakwa mafuta, ni mpakwa mafuta!

Hivyo, hata kampeni batili ya kutaka kumpora kiwanja, ni upepo tuu na utapita.

Watu kumfanyia fitna na majungu, Makonda, hawakuanza leo Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .

Yote haya yatapita, na Makonda atasimama.
P
 
Kugombea ni jambo moja na kupata kura ni jambo jingine. Lakini sio kwa CCM hii ya wanafiki ambao huwa wanampa kura Rais kwa asilimia 💯. BTW huyo bwege asahau kabisa.
 
Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2025 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
Mkuu Yohana Mbatizaji, johnthebaddest , hii ngoma bado iko very valid!
Niliwahi sikia kuwa vyombo vya dola vilimwambia Magufuli amuondoe Makonda ila yeye tu aligomaga kutokana na kumpenda sana.

Kwa nafasi mpya aliyoteuliwa na Chama chake nina uhakika mwenyekiti wake ajipange kuletewa kila siku taarifa zinazotokana na mapungufu yake.

Swali langu
Je waliomteua Makonda kuwa Katibu Mwenezi wanajua hizi changamoto zake? Hawakuuliza hata kwenye vyombo vya dola?

Wakati utaongea!
Mkuu Lord denning , you might be right kwenye yote hayo, kwasababu hakuna mkamilifu, ila human beings are not static, they are dynamics and hence, they change with time. Kwa mapito aliyoyapitia amejifunza humility, he will be the best of the best!.

Ili kumjua vizuri, anzia hapa Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Kisha Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam

Akawa RC wa DSM na akafanya makubwa ikiwa ni pamoja na kupitishwa kwenye tanuri la moto kupikwa akaiva kisawasawa

Kwa wale mnaopenda kujua mapito aliyo yapita karibuni pande hizi
Najua kuna watu bado hawaamini hili linawezekana, naomba kuwathibitishia, lisilo wezekana kwa binadamu, kwa Mungu linawezekana!.
P
 
Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2020 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
Yule naye ni bendara fuata upepo
 
Kwa vile 2025 bado, tuendelee kusubiria, ila sasa kuna tatizo hili

Asante Sana kwa taarifa hii, naomba Mimi Mwanajeiefu mwenzenu, niwe mtu wa kwanza kuwajulisha kuwa hii vita ya kutaka kumdhalilisha mpakwa mafuta wa Bwana, Paul Makonda, sasa ndio mwanzo WA mwisho wa hasidi huyu!. Karma ndio itamaliza kila kitu. Simaanishi Makonda ni malaika, bali, ni binaadamu kama binadamu wengine, hakuna mkamilifu, hivyo na yeye kuna makosa ametenda na tayari karma imeisha mshughulikia, hivyo kwa maonevu anayotendewa na hasidi huyu, ni Mungu, Baba ndiye atamlipia.
Kwanza mafanikio yake ni kutoka kwa Mungu. Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Kisha, Wale mnaosubiri kwa hamu Makonda atumbuliwe, mtasubiri sana!. Ukiwa ni mpakwa mafuta, ni mpakwa mafuta!

Hivyo, hata kampeni batili ya kutaka kumpora kiwanja, ni upepo tuu na utapita.

Watu kumfanyia fitna na majungu, Makonda, hawakuanza leo Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .

Yote haya yatapita, na Makonda atasimama.
P
"Neno litasimama
Neno litasimama
Neno litasimama
Mambo yote yatapita
lakini Neno litasimama!."

Hii ni chorus ya wimbo fulani!.
P
 
Labda
Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2020 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
 
Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2020 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
Labda mgombea Urais wa wasukuma!
 
Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2020 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
Unaweza kutimia
Wanabodi, kwenye bandiko hili Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia... nilishauri
Wanabodi,

Hili ni bandiko la kuhamasisha a mass mobilization ya kupata kundi kubwa la watu, kuunga mkono kwa dhati, juhudi kubwa zinazofanywa na Mkuu Mhe. Paul Christian Makonda, katika vita mbalimbali,

Hivyo hili ni bandiko la wito kwa kuwaomba ndugu, jamaa na marafiki wa dhati, wanaomjua Makonda kwa karibu na kwa ukweli, njooni tujitokeze kwa wingi, kumtetea Makonda tunayemfahamu dhidi ya uongo na uzushi unaozushwa na kusambazwa na mapapa wauza unga

Ndugu, Jamaa na Marafiki, Tujitokeze Kwa Wingi Kumtetea Makonda
Paskali.
Hata baada ya kuteuliwa kuwa Mwenezi wa CCM, Paul Makonda bado anapigwa vita na wasiomtakia mema, wasioitakia mema CCM na wasio itakia mema Tanzania.

Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi, na kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, mamlaka kuu ya nchi ni wananchi, kupitia katiba, serikali ya CCM ilifanya mabadiliko ya katiba kinyume cha katiba na kupoka ukuu wa mamlaka kuu ya wananchi, na kuikakabidhi kwa chama cha siasa, ambapo sasa mamlaka Kuu ya nchi ni chama tawala, CCM ndio imeshika hatamu kuongoza serikali, hivyo katika ukuu wa chama, CCM ndio kila kitu, hivyo Makonda kama msemaji wa CCM, kikao cha CCM kinaweza kumwagiza Rais wa JMT atekeleze jambo lolote lililoelekezwa kwenye ilani ya CCM, Katibu Mwenezi ndie msimamizi wa ilani ya CCM, ana mamlaka yote ya kumuamrisha hadi Rais wa JMT, atekeleze ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo Makonda yuko very right kumuamrisha Waziri Mkuu na kumpa ultimatum ya miezi 6 kumaliza migogoro yote ya ardhi ya nchi hii.

Na baada ya miezi 6, kama Waziri Mkuu, Majaliwa Kasim Majaliwa atashindwa kuitatua migogoro yote ya ardhi, atakuwa ni ameshindwa kazi, Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi, itakutana na kumuagiza Rais wa JMT, kumuondoa Waziri Mkuu, kwa kushindwa kazi na kumteua Waziri Mkuu mwingine mwenye uwezo.

Hata ikitokea Rais Samia ameshindwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM, chama kinaweza kumfuta uanachama na hivyo kupoteza urais!, hivyo Mwenezi wa CCM ni mtu mkubwa sana, kuliko serikali yote ya Tanzania, na hii ndio maana halisi ya Party Supremacy, CCM ndio imeshika hatamu za kuiongoza serikali ya Tanzania .

Hongera sana Mwenezi mpya wa CCM, Paul Makonda, kuiheshimisha CCM, endelea kutoa maagizo na ultimatum kwa viongozi wote kuhusiana na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM, wewe ndiye msimamizi wa ilani ya CCM!.

Angalia ilani ya CCM imeelekeza nini kuhusu Bunge la JMT, toa maelekezo kwa Spika with ultimatums, Spika akishindwa kutekeleza Spika anaondolewa!, enzi za Spika Sitta, aliponea chupu chupu kuondolewa, kuna mtu mmoja very powerful ndani ya CCM aitwae "The King Maker" ndie alimuokoa Spika Sitta kwa kumpa maelekezo Mwenyekiti wa CCM, JK, na hii ndio salama yake!.

Makonda angalia ilani ya uchaguzi ya CCM inasema nini kuhusu mhimili wa Mahakama, toa maagizo with ultimatum kwa Jaji Mkuu atekeleze.

Angalia ilani ya uchaguzi inasema nini kuhusu majeshi, ulinzi na usalama, toa maelekezo with ultimatum kwa Amiri jeshi Mkuu na kwa Mkuu wa majeshi, IGP , etc.

Ila kwa nafasi ambazo sio za kichama kama Jaji Mkuu, Mkuu wa Majeshi, CAG, Mwenyekiti wa NEC, Msajili wa Vyama vya Siasa, Wakuu wa vyombo vya Ulinzi, Mwenyekiti wa Tume ya Utawala Bora na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma ambao ni wateule wa rais, Paul Makonda anaweza kuwapa maelekezo bila ultimatums kwasababu hawa chama hakiwezi kuwafanya chochote, na badala yake, chama kitampa maelekezo mamlaka yake ya uteuzi ambaye ni Rais wa JMT, awaondoe!.

Kiukweli ninamkubali sana Paul Makonda!, Tangu nilipoanza kumkubali Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
He has never let me down!. Tena niliwahi kushauri Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze... ushauri huu still stands, kwasababu miaka hii 4 ya Mama ni kumalizia awamu ya Magufuli, awamu ya baada ya Magufuli inaanza 2025, ila Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke hivyo you never know with politics, everything is possible!.

Paul Makonda kanyaga mwendo, chapa kazi, kazi iendelee!.
Paskali.
 
Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mchambuzi wa maswala ya siasa.

Wakati fulani siku za nyuma kupitia hapa JF alimtabiria Mkuu wa Mkoa mstaafu Paul Makonda kuwa Mgombea Urais wa JMT kupitia CCM 2025.

Kwa sababu mgombea urais wa JMT kupitia CCM 2020 atakuwa kijana, Je utabiri wa Pascal Mayalla utatimia?

Ngoja tuone.

Maendeleo hayana vyama!
Arusha ni mapito tuu, Nampongeza huyu Mwamba, Paul Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha , ambao ni Geneva ya Africa.

Ila kwa maoni yangu, hii teua, tengua, hamish, na tumbua ya Rais Samia, is not healthy at all!, it's a sign of weakness mahali!.

My honest opinion, CCM haina mtu mwingine yeyote ambaye ni the best kwenye uenezi zaidi ya Makonda!.
Ili Rais Samia afanikiwe, asiwasikilize sana wahafidhina wa CCM, sometimes
wanamuingiza chaka!, kama hili la kumuondoa Makonda kwenye uenezi na kumpelekea RChuga , kiukweli kabisa hapa wahafidhina wa CCM, wamemuingiza Mama chaka.

Japo siungi mkono hizi teua leo badilisha kesho, Waenezi 5, ndani ya miaka 5!
1. Polepole
2. Shaka
3. Mjema
4. Makonda
5. The upcoming one!.

Hi sio picha nzuri!, ila nasisitiza kuna tatizo kidogo mahali Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda tuendelee kumpa muda, ata stabilize.

Hongera Paul Makonda kurudishiwa u RC, very soon itathibitika huyu aliyepo kwenye u RC wa Mkoa wetu hawezi!, soon utarudishwa RC DSM, jiji litanyooka!.
P
 
Arusha ni mapito tuu, Nampongeza huyu Mwamba, Paul Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha , ambao ni Geneva ya Africa.

Ila kwa maoni yangu, hii teua, tengua, hamish, na tumbua ya Rais Samia, is not healthy at all!, it's a sign of weakness mahali!.

My honest opinion, CCM haina mtu mwingine yeyote ambaye ni the best kwenye uenezi zaidi ya Makonda!.
Ili Rais Samia afanikiwe, asiwasikilize sana wahafidhina wa CCM, sometimes
wanamuingiza chaka!, kama hili la kumuondoa Makonda kwenye uenezi na kumpelekea RChuga , kiukweli kabisa hapa wahafidhina wa CCM, wamemuingiza Mama chaka.

Japo siungi mkono hizi teua leo badilisha kesho, Waenezi 5, ndani ya miaka 5!
1. Polepole
2. Shaka
3. Mjema
4. Makonda
5. The upcoming one!.

Hi sio picha nzuri!, ila nasisitiza kuna tatizo kidogo mahali Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda tuendelee kumpa muda, ata stabilize.

Hongera Paul Makonda kurudishiwa u RC, very soon itathibitika huyu aliyepo kwenye u RC wa Mkoa wetu hawezi!, soon utarudishwa RC DSM, jiji litanyooka!.
P
Naunga mkono 100%
 
Kwa vile 2025 bado, tuendelee kusubiria, ila sasa kuna tatizo hili

Asante Sana kwa taarifa hii, naomba Mimi Mwanajeiefu mwenzenu, niwe mtu wa kwanza kuwajulisha kuwa hii vita ya kutaka kumdhalilisha mpakwa mafuta wa Bwana, Paul Makonda, sasa ndio mwanzo WA mwisho wa hasidi huyu!. Karma ndio itamaliza kila kitu. Simaanishi Makonda ni malaika, bali, ni binaadamu kama binadamu wengine, hakuna mkamilifu, hivyo na yeye kuna makosa ametenda na tayari karma imeisha mshughulikia, hivyo kwa maonevu anayotendewa na hasidi huyu, ni Mungu, Baba ndiye atamlipia.
Kwanza mafanikio yake ni kutoka kwa Mungu. Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Kisha, Wale mnaosubiri kwa hamu Makonda atumbuliwe, mtasubiri sana!. Ukiwa ni mpakwa mafuta, ni mpakwa mafuta!

Hivyo, hata kampeni batili ya kutaka kumpora kiwanja, ni upepo tuu na utapita.

Watu kumfanyia fitna na majungu, Makonda, hawakuanza leo Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .

Yote haya yatapita, na Makonda atasimama.
P
Wasukuma ndo mambo kama haya yanayowafanya mnaonekana washamba.
 
Back
Top Bottom