Pascal Mayalla: CHADEMA watengeneze kwanza Katiba mpya ya chama chao kabla ya kukimbilia katiba ya nchi, wawatendee haki wabunge 19

Pascal Mayalla: CHADEMA watengeneze kwanza Katiba mpya ya chama chao kabla ya kukimbilia katiba ya nchi, wawatendee haki wabunge 19

Mwandishi wa habari nguli nchini na mwanasheria Pascal Mayalla amesema Chadema wanapaswa kurekebisha kwanza katiba ya chama chao kabla ya kukimbilia kudai katiba mpya ya nchi.

Pascal amesema Chadema hawana fedha za kuitisha kikao cha kujadili rufaa za wabunge wake wa viti maalumu sasa fedha za kuendeshea " harakati " za kudai katiba ya nchi watazitoa wapi?

Mayalla amewataka Chadema wamwache Rais Samia atengeze uchumi kwanza kwa sababu katiba mpya haiko katika Ilani ya uchaguzi ya 2020/35.

Nawasalimu kwa jina la JMT!
Kabla ya kuanza kudai katiba mpya , tunajukumu la kuanza kudai katiba ya chama chetu, hakika hii ya sasa imepitwa na wakati ina mfumo usiotoa uhuru kwa wanachama ,
Kiti cha mwenyekiti imekuwa nafasi ya kudumu , mfumo wa kupata uongozi wa matawi nao umejaa ukiritimba

Katiba mpya ya Chadema ni sasa.
We byembalilwa wee...!, unataka kuizungumzia katiba ya Chadema...
tembelea kwanza mitaa hii... Pascal Mayalla: CHADEMA watengeneze kwanza Katiba mpya ya chama chao kabla ya kukimbilia katiba ya nchi, wawatendee haki wabunge 19 na hii Fukuza Fukuza ya Uanachama: Kumbe Katiba ya CHADEMA ina makosa? na hii Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Kufutwa Kwa Mujibu wa Katiba!... Endapo ...!

P
 
Je, Paskali ana hoja?

Tuanze kwa kuitazama Katiba ya CHADEMA. Inahitaji marekebisho?
Bila shaka, inahitaji Mabadiliko. Katiba ya CHADEMA haielezi ukomo wa Kiongozi kuwa Mwenyekiti wa Chama. Ndiyo, kuna vipindi vya uongozi lakini kiongozi anatakiwa apewe ukomo wa muda wa kuwa Mwenyekiti. Ahudumu kwa miaka 8 aachie ngazi damu mpya zichukue kijiti.

Katiba yao inamruhusu Mwenyekiti aendelee kugombea mpaka atakapoamua mwenyewe kuacha.

Kwa hiyo ni dhahiri katiba yao inahitaji marekebisho.

Juu ya Swala la Wabunge Covid 19.
Paskali ameamua tu kujitoa ufahamu. Ila katika Chama chochote, kilichofanywa na Wabunge hao 19 siyo cha kufurahisha na wala hakipaswi kunyamaziwa. Siyo CHADEMA wala CCM ambaye angekuwa tayari kunyamaza kwa upuuzi uliofanyika.

CHADEMA kwa sasa wangekazania kufuatwa kwa Katiba iliyopo kuliko kuipigia kelele Katiba mpya. Ni swala ambalo linahitaji muda. Na Mh Rais kasema atalifanyia kazi miaka ijayo.
Nimekuelewa ila Pascal Mayala sijamwelewa hata kidogo kile kitendo kilichofanyika kwa Wabunge 19 wa viti maalum si cha kiungwana tusisubiri mpaka watu wafe ndiyo tuanze kuwananga kuwa walikosea,na kama ni uanasheria basi ni uanasheria wa kufaulu mitihani na si uanasheria wa kuzingatia sheria.
 
Pasco ametema MADINI YA ALMASI mno.

Chadema ni "The Comedy"..

Katiba yao INAWASHINDA....leo waiweze ya NCHI?

Hivi hawa akina "Jangala" wanashindwaje kuwaiga wenzao CCM wenye katiba LULU?!!!

#KaziIendelee
Katiba lulu wenye wasimamizi feki wasiozingatia sheria na utu wa Mtanzania,useless kabisa.
 
Mpaka pale atapopatikana Mwenyekiti wa CHADEMA kutoka kanda ya ziwa hasa hasa Msukuma hapo ndipo mtakatambua kuwa CHADEMA ni chama cha watanzania lakini leo ni cha kihuni kwa vili mwenyekiti si Msukuma.
chadema mwambieni mbowe ukweli kwamba mnasimamia misingi ya demokrasia ilio ya kweli, msimuogope! haya mambo ya anaachia ngazi atakapochoka yashapitwa na wakati nyerere alikua wa mwisho kufanya hivi
 
Mpaka pale atapopatikana Mwenyekiti wa CHADEMA kutoka kanda ya ziwa hasa hasa Msukuma hapo ndipo mtakatambua kuwa CHADEMA ni chama cha watanzania lakini leo ni cha kihuni kwa vili mwenyekiti si Msukuma.
aya mambo ya ukabila yashapitwa na wakati, apatikane mwingine wa uchagani sio mwenyekiti miaka100
 
Mwandishi wa habari nguli nchini na mwanasheria Pascal Mayalla amesema Chadema wanapaswa kurekebisha kwanza katiba ya chama chao kabla ya kukimbilia kudai katiba mpya ya nchi.

Pascal amesema Chadema hawana fedha za kuitisha kikao cha kujadili rufaa za wabunge wake wa viti maalumu sasa fedha za kuendeshea " harakati " za kudai katiba ya nchi watazitoa wapi?

Mayalla amewataka Chadema wamwache Rais Samia atengeze uchumi kwanza kwa sababu katiba mpya haiko katika Ilani ya uchaguzi ya 2020/35.

Nawasalimu kwa jina la JMT!

Ila kaka P unaonekana umechoka sana kiharakati. Inawezekana umefikia mwisho wa mwanzo umeanza mwanzo wa mwisho.

Its a big U turn kutoka kutetea wananchi hadi kutetea watawala kwa kila kitu.

Lakini ndio kunogesha mjadala!! Ukiwareshia mawe mengi yanaweza kuwafaa kujenga nyumba!! Kila jambo lina sababu!!
 
..hana hoja kwasababu sio Chadema peke yao wanaodai katiba mpya.
Suala la katiba mpya sio suala la vyama vya siasa bali suala linalohusu wananchi wote.

Ccm kama chama tawala kinachofaidika na status quo hakiwezi kuwa na ajenda ya katiba mpya kwenye manifesto yake.

Hakuna uhusiano kati ya kuchelewesha kupata katiba mpya ili uchumi uboreke if anything kupatikana kwa katiba mpya kutaharakisha uchumi kuboreka kwani kutakuwepo na taasisi imara za kuzuia matumizi mabaya ya rasilimali za nchi!
 
Mwandishi wa habari nguli nchini na mwanasheria Pascal Mayalla amesema Chadema wanapaswa kurekebisha kwanza katiba ya chama chao kabla ya kukimbilia kudai katiba mpya ya nchi.

Pascal amesema Chadema hawana fedha za kuitisha kikao cha kujadili rufaa za wabunge wake wa viti maalumu sasa fedha za kuendeshea " harakati " za kudai katiba ya nchi watazitoa wapi?

Mayalla amewataka Chadema wamwache Rais Samia atengeze uchumi kwanza kwa sababu katiba mpya haiko katika Ilani ya uchaguzi ya 2020/35.

Nawasalimu kwa jina la JMT!
Kutoa maoni ni bila malipo, aendelee tu kutoa maoni yake hata kama anachosema hakina tija
 
Back
Top Bottom