Pascal Mayalla ndiye aliyemchongea Erick Kabendera kwa dola

Pascal Mayalla ndiye aliyemchongea Erick Kabendera kwa dola

Sitaki kupinga hisia za mleta mada maana ndio uhuru wa maoni. Kwa ninavyomjua Paskali sidhani kama yupo upande wa muumiani ili kumuumiza Kabendera. Nadhani ni makala za kawaida kama makala zake nyingine. Na hizi tuhuma alizopewa leo ukichanganya na mada zake alizoandika kuhusu sakata la Acacia, natabiri Paskali kupewa cheo, kwa sababu watawala wataona hata Paskali anaweza kutuhumiwa na wanajf wenzake. Watawala wetu hupenda kutoa vyeo kwa wale wasiopendwa humu jf. Yaani atapewa cheo ili kutukomoa member wa jf na sio kwasababu ya kumchongea Kabendera.
 
Pascall yupo kitengo muda,aliingizwa na mzee wake.
Unadhani kwamba wateuaji Ni wajinga kihivyo wanapowatumia "unde covers agents"?

Wampe Uteuzi ili kuwathibitishia doubt zenu mlizonazo kwake huyo mwenzetu?

Wampe Uteuzi ili kumtoa rasmi hiyo "mask" aliyonayo?

If and only IF is true Ni mwenzao kutoka "kitengo" kile Maalum kamwe hatateuliwa ikiwa mission zao hazijakamilika, ataendelea kujinasibisha Kama alivyo ataendelea kuwa "kinyonga" ili kumatch na rangi za eneo husika atabaki kuwa "Panya" Mwenye kung'ata na kupuliza ili Kama Kuna malengo yoyote yatimie.
 
kuzisoma na kuzifafanua kwa vijana wa idara nyeti ili kijana azidi "

Mtoa mada umejawa na hisia zaidi ya uhalisia

Kwani watu wa idara hawewezi kuzisoma wenyewe?
Unahoja mufilisi zaidi nakuona unamchukia mayala unatumia hii kesi kutema povu

Kama huyo kabendera anaihujumu Nchi lazima ashughulikiwe
 
Mbona sijaona ulichoandika hapo kumtuhumu huyo pascal?
What if walidukua mawasiliano ya Kabendera?
Lakini pia kumbuka kashtakiwa kwa uhujumu uchumi na utakatishaji fedha. Wacha due process of law iamue.

Wabongo mnashangaza sana kwa UNAFIKI wa kiwango cha lami!
Kwa watu wanaosoma makala za Mayala watakubaliana kwamba huyu jamaa ni mzushi,mchonganishi na mpenda kujikomba kwa Watawala ili aonekane ni Mzalendo kumbe ni bonge la mnafiki…!
 
Paschal Mayalla anaweza kuungana na wakongwe wenzake kama Dr. Slaa, Zitto, Mtatiro, Kitila Mkumbo na wengine kupoteza ushawishi ndani ya jukaa hili baada ya kundi maalum "Folks" wa Jamii forum kuweka mijadala ya kumpinga kama walivyompinga Zitto na ACT yake, Dr. Slaa, Kitila na wengine baada tu ya wao kukengeuka.

Paschal Mayalla anatuhumiwa kumchongea mwana habari mwenzake Erick ambaye kwa sasa hatima ya uhuru wake imeshikiliwa na DPP.

Kundi hili (folks) limekuja juu na kwa hakika ndani ya siku mbili tu tayari Paschal anatoa mkono wa kwaheri ndani ya ushawishi wa Jf.

Nini kitafuata baada ya hapo?
Paschal ategemee kukutana na kila aina ya kejeli na vijembe pale atakapoanzisha ama kuchangia mada yoyote ndani ya Jukwaa hili la siasa. Aidha kundi hili (Folks wa Jf) ambao hujipambanua waziwazi kuwaunga mkono wanaharakati wanaokabiliana na madhaifu ya serikali yoyote ile itakayokuwepo madarakani lina nguvu sana ndani na nje ya Jf. Kama kundi hili likiamua kukujadili kwa mrengo hasi humu Jf basi utachafuka hata nje ya Jf. Hiyo ndiyo karma ya kundi hili.

Ikumbukwe kuwa Rais Magufuli alipoingia tu madarakani alielekea kusambaratisha nguvu ya kundi hili lakini iliwachukua wadau miezi minne tu ya utawala wake kumfahamu kiundani na kundi hili mara moja lilirudi katika makali yake na ukawa mwanzo wa ubaya wa Rais Magufuli kuanza kuonekana.

Aidha kundi hili lina maono mapana kwani tuhuma zote walizoibua kihisia tu mfano za Zitto, Dr. Slaa, Rais Magufuli na wengine wengi baada ya muda huibuka na kuwa kweli.

Wapo wakongwe kama barafu ambao wamejijengea heshima kubwa ndani ya kundi hili. Haitarajiwi kumuona mkongwe huyu akiondoka kwenye hisia nzuri za kundi hili ingawa kila kitu kinawezekana mathalan pale utakapoona tu kundi hili limeanza kuhisi kama walivyofanya kwa Paschali na sasa anakula jeuri yake.

Kundi hili ni ngumu sana kuja kumuweka mtu wao madarakani kutokana na hisia zao kali.

Nimtakie tu Paschali maisha mema mengine kabisa ndani ya Jf na awe tayari kupewa kila aina ya baya ila angalizo kwake ni kuwa kundi hili halijawahi kamwe kurejesha sawasawa heshima ya mtu aliyesaliti mawazo yao hata kama amerudi na kutubu kweli kweli mfano Nape Nnauye ambaye bado anaambiwa "Anaongea vile kwakuwa kapokonywa tonge mdomoni"
 
For sure sijaona kosa la Paschal. Unless Kama alikuwa anatumiwa.

Ukisoma mabandiko yake mengi Paschal amekuwa mtu mchokonoz tu lkn huwa hatoi hukumu Bali ana speculate hidden agenda
 
Acheni kumuonea wivu.. mbona wengi mnaleta habari humu na matokeo ya wao kujulikana na ubaya hamuwasemi!!!! Huyo mwandishi aliandika yeye y mlaumu wengine?

Endeleeni kumpandisha chati.. safi sanaaaa
 
Mimi nitaendelea tu kumkubali Pascal Mayala.Hivi jamani Pascal anamchongea vipi Erick ? Basi nampa pongezi nyingi Paschal kwa kuweza kuwa na capacity ya kushawish watu wenye taaluma zao. Big up Paschal. Keep it up.
 
Back
Top Bottom