Pascal Mayalla ndiye aliyemchongea Erick Kabendera kwa dola

Pascal Mayalla ndiye aliyemchongea Erick Kabendera kwa dola

Based on Kifo cha Akwilina, ainisha kosa la kina Mbowe na usafi wa polisi waliopiga risasi juu ikakata kona ikajikuta imeua abiria kwenye gari then tuje tumalizie na la Mayalla!

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamani sheria inasema ushahidi uwe direct, yaani shahidi ameushuhudia kwe sensory organs zake.Mfano kuona au kusikia.sasa wewe hiyo risasi ilivyofatuliwa uliona na ilipokata kona uliona?
 
1.Sio atengwe aliyekuwa anaandika habari bila kufuata weledi na kuishia kutukana rais.
2. Unaposema hakumuita na kumuonya ina maana ye hakuwa anaingia humu jf na kusoma maandiko ya pasco au alikuwa anapuuza?
3. Kisha ndugu zake na mama yake wanapataje shida wakati alikuwa na backup ya watu wengi wakiwemo kina zitto, waende wakahudumie familia. Au anzisheni kapu la kuchangia familia yake.
4. Unapozichokoza mamlaka na kujiona shujaa jua tu utalipia gharama siku moja, ni suala la muda. Hata tundu lissu kalipia gharama. Na akiendelea atalipia tena. Kifupi dunia ina kanuni zake. Hiyo ni principle ya dunia nzima.
5. Lakini pia watz tumshukuru sana Pasco kwa kufichua habari za huyu kinyamkera ambaye ni ant government. Watu hawa wapo nchi nyingi tu. Lakini nadhani habari yake kwisha. Mtapiga makelele baada ya muda mtasahau na maisha yataendelea. Pengine atapelekewa tu tarifa za kifo cha mama yake kwa kukosa dawa. Kina zitto nao baada ya muda watakuwa bize na mambo yao na kumsahau kabisa.
Mimi nafikiri angeshitakiwa kwa makosa mabayo yapo kwenye Media Services Act,2006. Hili kuhujumu uchumi na katatisha rupia! Labda wenye mamlaka wanajua alihujumu vipi
 
Niombe wasomaji wangu muelewe kuwa sina nia mbaya ninapojaribu kuja na uchambuzi wa namna hii. Lengo langu ni kuoneshana kuwa nchi yetu iko hatarini hasa pale taaluma moja ambayo Taifa linawategemea wanaposigana katika jamii nani anayeumia zaidi!

Nakumbuka siku za hivi karibuni gazeti la the Economist lilikuja na habari ambazo Mkuu Pascal aliziita kuwa ni habari za uongo dhidi ya Rais wetu wa Tanzania.

Gazeti hilo liliwahi kuja na habari kuwa "Rais wa Tanzania hapendi kukosolewa"

Gazeti hilo baada ya kuchapishwa Pascal Mayalla alikuja na bandiko la kupinga habari ile huku akionesha jinsi ambavyo sio kweli Rais wetu anapenda kukosolewa.

Alikwenda mbali zaidi akamnukuu Rais wetu kuwa aliwahi kuwaambia wanahabari kuwa yeye anapenda kukosolewe ila akosolewe kwa Staha na kwa hoja.

Pascal Mayalla kwenye andiko lake anatolea mfano kuwa yeye Pascal Mayalla ni moja ya wanahabari ambao waliwahi kumkosoa Rais na Rais alikubali kukosolewa kwa kumjibu huku akimtania.

HOJA.

Kwanza lazma watu mjue kuwa andiko la Pascal kupinga habari ya the Economist ndio iliyoamsha watu na kuanza kufuatilia ni nani na yuko wapi anae ripoti habari hizo katika gazeti la the Economist?

Hapa naomba nieleweke, hata watumishi wa idara nyeti walianza kufatilia gazeti hilo baada ya kusoma bandiko la Pascal Mayalla hapa JF, na ndipo wakaja kugundua kuwa kumbe mwandishi wa habari zile na nyeti kupitia gazeti lile ni ndugu yetu Erick Kabendera.

Kwanini walifuatilia, kiukweli kilichoandikwa na mwandishi huyo wa habari kilikuwa na ukweli wa 100% ingawa huyu Ndugu Mayalla alikipinga kwa lengo la kujipendekeza kwa msukuma mwemzake.

Je, Pascal Mayalla alijua tangu awali kuwa Kabendera ndie anayeandika habari nyeti na kuziripoti The Economist na alishindwa kumuita kama mdogo wake na kumpa onyo?

Kimsingi kifungo cha Kabendera nadhani ni furaha kwa Mayalla kwani alimjua tangu awali na alishindwa kabisa kumuita na kumuonya ingawa wote wanatoka kanda ya ziwa.

Je, Pascal alijua Erick akifungwa tegemezi wake watalia na kusaga meno na wengine watajitokeza mitandaoni wakimlilia kwa kukosa hata fedha ya kununua Dawa?

Nadhani yote aliyajua ndio maana tangu Kabendera awekwe korokoloni hajawahi jitokeza popote kulaani kukamatwa kwa kijana huyu zaidi inasemekana ndio kwanza anatafuta makala zote zilizoandikwa huko nyuma na kuzisoma na kuzifafanua kwa vijana wa idara nyeti ili kijana azidi kubanwa.

Andiko la Mayalla dhidi ya kumtetea ndugu yake liko hapa JF linaudhi linaumiza kwani humo ndani anawataja wakosoaji wakubwa wa nchi hii ambao leo hii wamegeuziwa rangi ya unga wa ndere wao wanaita unga mweupe sasa huku wakila kuku kwa mirija.

Nasisitiza waandishi wa habari mtengeni Mayalla na waandishi wote wenye vinasaba vya ukabila na wanaoshindwa kusimamia taaluma badala yake wanaishia kujipendekeza kwa kuhofia uhai wao.

Natoa rai kwa Serikali ya Jamhuri kumwachia huru Kabendera. Tusipomdai kwa kiswahili tutawataka kwa kilugha, na hapo ndipo tutakapozuia kiongozi yeyote kuingia mkoa wa Kagera mpaka "omwana weitu mumutaishure."

======
Acha uongo nenda kamsaidie huyo msaliti mwenzio mahakamani. Eti utatuzuia kuingia Kagera sasa sisi tukitaka hata huko Kagera hutafika. Pia kumbuka ni sisi ngosha ndiyo tuliowasaidia kumtoa nduli IDD Amin alikuwa ameshaanza kuwafanya mbaya mpaka akawaachia ugonjwa wa Slim (UKIMWI). Baada ya kusumbuka na Pascal Mayalla mlitakiwa kuhangaika na huyo msaliti Erick aache usaliti la sivyo atanyooshwa.
 
Mimi nafikiri angeshitakiwa kwa makosa mabayo yapo kwenye Media Services Act,2006. Hili kuhujumu uchumi na katatisha rupia! Labda wenye mamlaka wanajua alihujumu vipi
Alikuwa anapokea pesa toka kwa mabwana zake na kuzigawa kwa wasaliti wenzie ili kuitukana serikali na Rais wake. Mbaya zaidi alikuwa anakwepa kulipa kodi kutokana na mapato yake hayo kumbuka kukwepa kulipa kodi ni predicate offence ya Money Laundering, this is according to Anti-Money Laundering Act. Nafikiri ndiyo maana ameshitakiwa na ML mkuu!
 
Aiseee
Pascal Mayalla ufataani anao kweli kweli, kwa hilo siwezi mkatalia au mtetea. Tena ni nyoka haswa mwenye vichwa viwili, kimoja mbele kimoja nyuma, kikikukosa cha mbele cha nyuma kinakungoja.

Binafsi nimeshamueleza mara nyingi sana humuhumu JF kuwa yu fataani.

Nnawashangaa sana kuwa ndiyo kwanza mnayajuwa hayo, nikizipata posts nilizowahi kumwambia kuwa yu fataani nitawawekea humu muone kuwa nililiona hilo zamani sana.


Na fataani mwengine na ndumila kuwili ni anaejiita Mzee Mwanakijiji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani Paschal Mayala ndiye Kabander aliyemfungulia kesi ya utakatishaji.

Najua Paschal ni mbumbumbu katika sekta nyingi na huwa namkabili humu lakini siyo kama unavyotaka tuamini katika hili.

Cc:
Pascal Mayalla
Huyu ni P ?
 

Attachments

Mbona sijaona ulichoandika hapo kumtuhumu huyo pascal?
What if walidukua mawasiliano ya Kabendera?
Lakini pia kumbuka kashtakiwa kwa uhujumu uchumi na utakatishaji fedha. Wacha due process of law iamue.
Aliposema habari za TISS kutesa watu kule kigoto Mwanza na kuomba ifumuliwe mbona hamkulaumu! Alikopi na kupaste habari za gazeti la Economist. Kisha kwa uzalendo akasema hili gazeti lina mtukana mtanzania imekuwa kosa!
 
Mkuu Hufi Leo, kwanza sikujitokeza kujibu tuhuma hizi kwa kuzipuuzia tuu kuwa kwa vile huu ni uongo na uzushi, uongo mwingine na uzushi ukiuupuuzia tuu utayeyuka na kupita tuu kama upepo hivyo nilipuuza kwa matumaini ni upepo tuu na utapita. Lakini leo baada ya kifo cha mama yake, nimeona nisiendelee kunyamaza hivyo ndio nimejotokeza leo na kukujibu in points format.

Hatua yangu ya kwanza, ni kutuma Salaam maalum kwa rais Magufuli.

Kisha nikawaka hoja zako in points format ili kujibu kila hoja
  1. Hukuna uthibitisho kuwa ni andiko langu lilipelekea jarida hilo lifuatiliwe, hakuna uthibitisho wowote kuwa sasa jarida hilo linafuatiliwa na hakuna uthibitisho wowote kuwa Eric Kabendera ndie mwandishi wa makala mimi nilizokuwa nazileta humu.
  2. Mimi sina uthibitisho wowote kuwa watu wa Idara nyeti walianza kufuatilia jarida lile baada ya bandiko langu humu jf, lakini kwa vile hata sisi humu jf hatujuani nani ni nani, its good to know that na pia sikuwahi kumjua mwandishi wa makala zile, I'm now learning from you.
  3. Kwenye makala zangu nilikiwa naweka kila cha kweli na cha uongo, niliukubali ukweli na kuupinga uongo na sio kwa lengo la kujipendekeza kwa Msukuma mwenzangu. Kazi ya mwandishi wa habari ni kusema ukweli na kuandika ukweli, mimi ni mkweli, msema kweli na mwandika ukweli bila kujali ukweli huo utamfurahisha nani au kumchukiza nani.
  4. Naendelea kusisitiza sikuwahi kumjua mwandishi ni nani, ila hata ningemjua, as long as anachoandika ni kweli, bado nisinge muita mwandishi yoyote kumuonya kwa kazi yake yoyote bali bado ningeendelea kukosoa au na mimi kuandika makala zangu kwenye magazeti yangu ninayoandikia. Hapa nilipo kuna waandishi wengi critical tunafahamiana na kuheshimiana, andiko lolote linajibiwa kwa andiko na sio kwa kuitana.
  5. Hii ni personal opinion, kuna watu wenye roho za kishetani ambao wanafurahia binaadamu wenzao wanapopata matatizo, very unfortunately mimi sii miongoni mwa watu wa kundi hili, wanaonijua wananijua na wanaonisoma, wananisoma.
  6. Kwavile tangu mwanzo sikujua kama ni Eric Kabendera wala sikujua nini kitatokea, pia hili sikulijua.
  7. Hili sii kweli.
  8. Ungeliweka hilo andiko
  9. Waandishi wa habari hawawezi kulifanya hili.
  10. Nimeunga mkono rai yako.
Nampa pole sana Eric Kabendera kwa mapito anayopitia.
P
Lakini vipi kuhusu kabendera maana Kuna bandiko himu limewahi kukuhusisha na kumchongea kabendera hujawahi kukanusha kwa ufasaha. # binadamu wote ni ndugu zangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Karibu
P
 
Watanzania wengne ni vimbelembele sana sijui tunahitaji vyeo!!!! Hata wakat mwngne cjui tu hata mm nakubaliana na andiko hili ndg #paschal Kuna mazingira huwa Kama naona ananyenyekea na kupiga magoti serikali kana kwamba there is something in needy....anyway ndio hivo jamaa yupo ndani na anasota
My regards to all ....
Kumnyang'anya tonge mtu sio kazi nzuri kabsa acheni aongoze muda wake utaisha tu
 
Alipoitwa bungeni ndg bwana Paschal Kama ukifuatilia kwa undani Kuna speed ya kuikosoa serikali na bunge kiujumla ilpungua kutoka kwa huyu ndg...hapo huwa nahisi pengne alitishiwa au la Basi aliahidiwa nafasi sio bure Paschal na najua hawezi sema
 
Back
Top Bottom