Pascal Mayalla ndiye aliyemchongea Erick Kabendera kwa dola

Pascal Mayalla ndiye aliyemchongea Erick Kabendera kwa dola

Mkuu Hufi Leo, kwanza sikujitokeza kujibu tuhuma hizi kwa kuzipuuzia tuu kuwa kwa vile huu ni uongo na uzushi, uongo mwingine na uzushi ukiuupuuzia tuu utayeyuka na kupita tuu kama upepo hivyo nilipuuza kwa matumaini ni upepo tuu na utapita. Lakini leo baada ya kifo cha mama yake, nimeona nisiendelee kunyamaza hivyo ndio nimejotokeza leo na kukujibu in points format.

Hatua yangu ya kwanza, ni kutuma Salaam maalum kwa rais Magufuli.

Kisha nikawaka hoja zako in points format ili kujibu kila hoja
  1. Hukuna uthibitisho kuwa ni andiko langu lilipelekea jarida hilo lifuatiliwe, hakuna uthibitisho wowote kuwa sasa jarida hilo linafuatiliwa na hakuna uthibitisho wowote kuwa Eric Kabendera ndie mwandishi wa makala mimi nilizokuwa nazileta humu.
  2. Mimi sina uthibitisho wowote kuwa watu wa Idara nyeti walianza kufuatilia jarida lile baada ya bandiko langu humu jf, lakini kwa vile hata sisi humu jf hatujuani nani ni nani, its good to know that na pia sikuwahi kumjua mwandishi wa makala zile, I'm now learning from you.
  3. Kwenye makala zangu nilikiwa naweka kila cha kweli na cha uongo, niliukubali ukweli na kuupinga uongo na sio kwa lengo la kujipendekeza kwa Msukuma mwenzangu. Kazi ya mwandishi wa habari ni kusema ukweli na kuandika ukweli, mimi ni mkweli, msema kweli na mwandika ukweli bila kujali ukweli huo utamfurahisha nani au kumchukiza nani.
  4. Naendelea kusisitiza sikuwahi kumjua mwandishi ni nani, ila hata ningemjua, as long as anachoandika ni kweli, bado nisinge muita mwandishi yoyote kumuonya kwa kazi yake yoyote bali bado ningeendelea kukosoa au na mimi kuandika makala zangu kwenye magazeti yangu ninayoandikia. Hapa nilipo kuna waandishi wengi critical tunafahamiana na kuheshimiana, andiko lolote linajibiwa kwa andiko na sio kwa kuitana.
  5. Hii ni personal opinion, kuna watu wenye roho za kishetani ambao wanafurahia binaadamu wenzao wanapopata matatizo, very unfortunately mimi sii miongoni mwa watu wa kundi hili, wanaonijua wananijua na wanaonisoma, wananisoma.
  6. Kwavile tangu mwanzo sikujua kama ni Eric Kabendera wala sikujua nini kitatokea, pia hili sikulijua.
  7. Hili sii kweli.
  8. Ungeliweka hilo andiko
  9. Waandishi wa habari hawawezi kulifanya hili.
  10. Nimeunga mkono rai yako.
Nampa pole sana Eric Kabendera kwa mapito anayopitia.
Unahusika kwa namna moja au nyingine juu ya kifo cha mama kabendera. Furahi basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wanaompinga mayalla so ndo wale wale vibaraka, kila mtz mwenye nia njema na Tz hawezi ku-expose mambo ya ndani kwa maadui. Jeshini hao huwa hawana uhai
Watu wakipotezwa, wakiuawa, tukae kimya kwa kumlinda nani? Unaweza kutueleza katika zile makala za lile jarida ni zipi za uongo? Wewe utajisikiaje kesho unaamka mumeo katekwa kauawa au mama yako katekwa kauawa na hakuna taarifa yeyote ya kiuchunguzi?

Wewe utajisikiaje umeolewa unaambiwa hakuna kupeleka sherehe nyumbani na badala yake ukishavalishwa Pete na shela mkishatoka kanisani uvue shela lako uende nyumbani ukapumzike na mumeo?

Au utajisikiaje jimboni kwenu maendeleo hayafiki kwa vile mlichagua upinzani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwann
Watu wakipotezwa, wakiuawa, tukae kimya kwa kumlinda nani? Unaweza kutueleza katika zile makala za lile jarida ni zipi za uongo? Wewe utajisikiaje kesho unaamka mumeo katekwa kauawa au mama yako katekwa kauawa na hakuna taarifa yeyote ya kiuchunguzi?

Wewe utajisikiaje umeolewa unaambiwa hakuna kupeleka sherehe nyumbani na badala yake ukishavalishwa Pete na shela mkishatoka kanisani uvue shela lako uende nyumbani ukapumzike na mumeo?

Au utajisikiaje jimboni kwenu maendeleo hayafiki kwa vile mlichagua upinzani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwann Unatuhumu serikali kuhusu utekaji??? Unaushahidi utuwekee hapa au ni hisia zako tu, wanaouawa umejiridhisha ni serikali inayohusika? Weka ushahidi hapa. Mm hauwezi kuniaminisha uongo usio na evidence, hizo ni tuhuma tu ambazo siyo Mara ya kwanza kuzisikia toka awamu za nyuma.
 
Based on Kifo cha Akwilina, ainisha kosa la kina Mbowe na usafi wa polisi waliopiga risasi juu ikakata kona ikajikuta imeua abiria kwenye gari then tuje tumalizie na la Mayalla!

Sent using Jamii Forums mobile app

Kila mtu anawajibika na maneno yake, mi namuwajibisha aliyesema Paskal ni mbaya, ya Akwilina kamuwajibishe aliyeyazungumza! Hii ni rahisi sana
 
Hili suala nadhani lifike ukomo. Tuhuma zimetolewa na ndugu yetu Pascal kaamua kujibu tuhuma hizo kwa uwazi kabisa.
Tusimbebeshe tuhuma nzito bila ushahidi na ubaya wa Mganga DPP wala sio haki kumpatia mwingine. Kabendera kaandika kwa magazeti hayo ya nje alio ona ni ukweli. Kama uongo serikali ilipaswa kukanusha na kusemea ukweli wake, au kumshtaki Kabendera kwa makosa halisi na sio kutafuta kubambika makosa yasiyo na dhamana kwa kusudio LA kumkomoa.
DPP analofanya ni uhalifu mkubwa sana, eitha katumwa au kajipanga.
 
Kwann

Kwann Unatuhumu serikali kuhusu utekaji??? Unaushahidi utuwekee hapa au ni hisia zako tu, wanaouawa umejiridhisha ni serikali inayohusika? Weka ushahidi hapa. Mm hauwezi kuniaminisha uongo usio na evidence, hizo ni tuhuma tu ambazo siyo Mara ya kwanza kuzisikia toka awamu za nyuma.
Wewe uwekewe ushahidi nani nakuweka kuwa mwamuzi...? Are you the court foolish..?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hili namtetea Paschali Mayala, aliyemchongea atakuwa yule marehemu wa hazina ambaye inasemakana kajinyonga, japo ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuwa aliuliwa kabla ya kutundikwa mtini, inawezekana pia mayala naye ni mmoja wa waandishi wa hilo gazeti, huwezi jua, lakini kumchongea mtu sizani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom