Pasco Mayalla ana vielement vya unabii afungue kanisa

Pasco Mayalla ana vielement vya unabii afungue kanisa

Pasco yuko vizuri kwakweli sema ndio hivo hatujui kiundani what really the obstacle behind
Thanks for concern
Ila kuna mda nae anasahau kabisa professional yake anaanza kushabikia pumba za ccm kuwin teuzi.
Karibu Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!
He should learn the strong men are those who stend alone
Haya ni maneno ya faraja sana, sasa nalala na amani.
P
 
Mkuu mdukuzi , kumbe wewe wa longi!, humu JF siku hizi kumejaa madogo hawachelewi kutukana, utadhani tunalingana nao!.

Duh kumbe tulikuwa tunaishi wote Mabibo!.

Hukunitendea haki kabisa Watanzania huwa tunasalimiana hata kama hatujuani, japo mimi ni kweli niliwahi kuwa maarufu, lakini sikuwahi ku behave ki super star, mimi ni mtu wa kawaida sana!.

Ni kweli niliingia UDSM kusoma LL.B, sikuwahi ku supp hata somo moja. Mwaka wa 4, mtihani wa mwisho kuna ticha mmoja akanifutia matokeo yangu ya UE kwa somo lake hivyo nikapigwa a technical DISCO for absconded!.

Issue ilikuwa hivi, yule ticha ananijua, tulikutana mitaani mitaa ya Sinza kwenye mambo yetu yale, denti ukampita ticha, ticha akamaind hivyo akafuta matokeo yangu na kupigwa disco!.

Nikafuatilia matokea ya external examiners somo lake nina A!. Nikaapeal kwa dean by then ni Dr. Ibrahim Juma. Ticha alipoulizwa kwanini amenifutia matokeo, akamwambia dean amefuata almanac ya UDSM ili uweze kufanya UE, lazima uwe umehidhuria course work 60%. Ticha akamwambia dean hajawahi kuniona kwenye somo lake hata mara moja, akasisitiza namjua Pasco na sijawahi kumuona darasani kwangu.

Mimi nikajitetea darasa tuko wanafunzi 400!, utajuaje kama nipo au sipo?. Nikamwambia hata siku ile anauliza swali class na kuniita kwa jina, sikuitika kwasababu nilikuwa sina jibu na sio kweli sijahudhuria somo lake!.

Dean Dr. Juma akaamuliza, jee ame miss hata course work moja?. Sijamiss!. Dipo dean akampiga masomo mawili
1. Uthibitisho wa mwanafunzi kuhudhuria lecture ni kupitia attendance register na sio kuangalia sura eti unamjua na hujamuona!. Jina langu kwenye attendance register, lipo vipindi vyote!.
2. Prospectus ya chuo kwa Mwanafunzi ambaye hajahudhuria 75% anatakiwa kuwa barred na kuzuiwa ku sit for EU, mimi was not barred, mwanafunzi akiisha sit for UE na matokeo yatatoka, hawezi kufutiwa matokeo yake, hivyo nilishinda appeal, nikapata LL.B yangu with honours!.

Siko TV yoyote siku hizi. Mimi ni freelance hivyo naingia TV yoyote.

Asante ila sii kweli kuwa hakuna mwana JF anayenifikia, if tuna manabii kibao! Tanzania tulipo Sipo!. Nabii Hakubaliki Nyumbani, JF Tuna Manabii wa Kweli, Tuwatumie Walisaidie Taifa!

Asante nimekusikia, mtu akiisha kuwa Mkatoliki mzuri, hawezi kufungua kanisa.

Mimi ni mpinzani wa kuchanganya dini na siasa Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?

Ukiisha ita ni pepo la utambuzi hizo ni nguvu za giza, ila pia ni ngumu kubaini maono fulani kama yanatoka kwa Mungu au kwa shetani, mfano hapa, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke
P
Bwana Pascal Mayalla asante sana kwa ufafanuzi kuntu,mi ni mkongwe kiumri japo sikufikii,kwa ufupi watu tuliokuwepo enzi za kitimoto wote tunakukubali,kwa mtazamo wangu;Kitimoto ndio iliyokupa jina na heshima mjini

Kuhusu kudisco UDSM,chuo kizima kilifahamu kuwa umeonewa,ilikuwa ni aibu sana kwa yule mwalimu.

Humu JF pia tunakukubali hata hawa watoto wanaotukana ni utoto tu wasikukwaze.

Mimi binafsi naami wengi tumejifunza na tunaendelea kujifunza kupitia wewe.

Amani ya Bwana itawale maishani mwako,ipo siku tu utaitumikia nchi JWa mapana yake katika njia ambayo wengi tunaitamani itokee kwako iwe ni kwa teuzi au chaguzi
 
Nilianza kumuona miaka ile na kipindi chake cha Kitimoto.

Nikaja kukutane nae UDSM akisoma LLB na mimi nikisoma kozi ngumu kuliko zote pale chuoni, namkumbuka akinesanesa na pikipiki lake viunga ya UDSM au Mabibo Hostel nilipokuwa naishi.

Mwaka 2005 Au 2006 NIlikuwa napata lunch Hill Park, tukajikuta tuko meza moja, ila kwa vile alikuwa star sikumshobokea, Kama ilivyo desturi yangu ya kuwakaushia mastaa so hanijui, simjui.

Kwa bahati mbaya wote tulidisco chuo,Mimi nilidisco sababu ya ugumu wa masomo ila mwenzangu nasikia ilikuwa ni figisu figisu tu za prof mmoja sio sababu ya uwezo mdogo.
Baada ya kudisco nikakimbia nchi tena kwa mara ya pili. Sikuwahi kumuona tena zaidi ya kumsoma JF na mimi siangalii TV sijui yuko TV gani siku hizi.

Kupitia JF Nimekuwa nikifuatilia maandishi yake, nara kadhaa, niseme tu maandishi yake yana unabii ndani yake, orodha ni ndefu sana nikiweka hapa hapatoshi, vitu vingine huchukua miaka hata mitano kutokea, hakuna mwana JF anayemfikia kwa hilo.

Kama hana pepo wa utambuzi basi ana roho mtakatifu. Nafahamu yeye ni mkatoliki Mzuri ila afungue tu kanisa atapata wafuasi. Nafahamu pia anapenda siasa, madhabahuni pia ni sehemu sahihi ya kupiga siasa kama akina Mama Rwakatale, Kakobe, Gwajima, Pengo, Mtikila, Sheikh Ponda, Alhad Musa wote hao wanapiga siasa kwenye mimbari.

Atumie hilo pepo la utambuzi au roho mtakatifu aliyenae kuwafikia wengi.

Maana kila utawala unamsukumia kambo utadhani hana kitu kichwani na kwa umri wake sitegemei kuona akipata teuzi,

Ni ushauri tu.
Waungane na lema au sio?
 
Kabisa mkuu kuna watu wamekalia ofisi za umma wanakula kodi zetu kichwani zero,Pascal akili nyingi yuko nje ya mfumo,not fair
Sasa huko serikalini kila mtu ambaye upstairs akiwa njema ndio awe huko mbona itakuwa balaa huku uraiani,

Acheni magugu na ngano vikae sehemu moja ili mkulima afanye kazi yake.

Pengine paskali hata hataki utezi ni nyie tu ndio mnamchawia.
 
Basi kama ni kweli mwambie hali ya umeme na umshauri asigombee 2025 maana "punda amechoka" ni hayo tu.
Mkuu Supu ya kokoto , sio kwamba najifagilia, bali ni ukweli halisi, kwenye tasnia yangu ya habari, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari very bold!, hii inapelekea nakuwa sialikwi kwenye events za habari kwa watu kuogopa maswali yangu, lakini maswali hayo, yanasaidia sana!. Mfano like swali langu kwa JPM kuhusu mikutano ya siasa, Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli ndilo limempelekea Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa!.

Hiyo ya kutogombea 2025, niliisha mshauri kitambo sana Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke ni bahati mbaya sana humu watu wenye uwezo to read in between the lines wanahesabika, watu wenye uwezo to reason the context ya mada wanahesabika, mtu bold anayeweza kupandisha bandiko kama hilo kumshauri Mama asigombee 2025 halafu yanatokea majitu majinga yanakuambia unatafuta u DC!, yanatia hasira.
P
 
Mkuu Supu ya kokoto , sio kwamba najifagilia, bali ni ukweli halisi, kwenye tasnia yangu ya habari, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari very bold!, hii inapelekea nakuwa sialikwi kwenye events za habari kwa watu kuogopa maswali yangu, lakini maswali hayo, yanasaidia sana!. Mfano like swali langu kwa JPM kuhusu mikutano ya siasa, Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli ndilo limempelekea Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa!.

Hiyo ya kutogombea 2025, niliisha mshauri kitambo sana Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke ni bahati mbaya sana humu watu wenye uwezo to read in between the lines wanahesabika, watu wenye uwezo to reason the context ya mada wanahesabika, mtu bold anayeweza kupandisha bandiko kama hilo kumshauri Mama asigombee 2025 halafu yanatokea majitu majinga yanakuambia unatafuta u DC!, yanatia hasira.
P
Mjomba wangu pascal,Mimi Nina Imani sana na maandiko Yako...watanzania mafuvu Yao yana layers nyingi sana kupelekea uzito kualewa mambo
 
Sasa huko serikalini kila mtu ambaye upstairs akiwa njema ndio awe huko mbona itakuwa balaa huku uraiani,
Asante sana othuman dan fodio , kila nikiliona jina lako nakumbuka Usman dan Fodio, ambae jina lake pia kuandikwa Uthman au Usuman, na kwa Kiarabu ni ʿUthmān Ibn Fūdī, alizaliwa December 1754, kijiji cha Maratta, mji wa Gobir, kwa kabila la wa Hausa na wa Sokoto, nchi yao akiitwa Hausaland ambayo sasa ni Nigeria, alikuwa ni kiongozi wa Sokoto na Fulani empire, alikuwa na nguvu fulani za mystic, powers, ndiye aliyeanzisha vita vya jihad kati ya mwaka 1804 hadi 1808, na kuifanya Nigeria kuwa ni nchi ya Kiislamu licha ya kuwa ndilo taifa la Africa linaloongoza kwa idadi ya Wakristu!, alikufa mwaka 1817, hivyo kila nikikutana na post yako yoyote, kwanza inakula like yangu!.

Hii JF ya sasa ina majitu majinga mengi, yasiyo na good thinking capacity, kama kila mtu mwenye akili nzuri atapaswa kuteuliwa nani wataleta maendeleo ya nchi hii?. Wanaoteuliwa waachwe wateuliwe, halafu sisi wengine, kama tuna akili nzuri, tuzitumie basi hizo akili zetu nzuri kuleta maendeleo kwenye taifa letu huku huku tulipo na sio mpaka tuteuliwe. Mfano mzuri ni mimi mwenyewe hapa nilipo namsaidia sana Samia kuliko hata ningeteuliwa nafasi yoyote!. Msaada wangu mkubwa kwa Samia, ni kumweleza kuwa everything happens for a reason!, hakuna kitu chochote kinachotokea bila sababu, hivyo ni watu wanache mimi nikiwemo ambao tunajua sababu za ni kwanini mtu wetu yule alitwaliwa!. Blaza ni karma ilikula kichwa!, hivyo tunawajibu wa kumsaidia Mama Samia kwa kumkinga asirudie makosa ya mtwaliwa kwa kugenerate bad karma ikaja kumponza na yeye akaishia... Wito Kwa Viongozi Wetu: Unapokosea, hata kwa kujikwaa tu ulimi, tujenge utamaduni wa kuwajibika ili kumuepushia Rais wetu kubeba mzigo wa karma hivyo kitendo tuu cha kutoa elimu ya karma kwa Rais Samia ni msaada mkubwa sana kwake kuliko ningeteuliwa kushika nafasi yoyote!.
Pengine paskali hata hataki utezi ni nyie tu ndio mnamchawia.
Sio pengine huo ndio ukweli. Watu hawajui nimesoma shule moja primary na Dr. Mwinyi, shule hiyo watoto wa vigogo wote ndio tulikuwa nao kuanzia Nyerere, Kawawa, Malecela na mawaziri wote!. Dr Mwinyi alinitangulia darasa, sekondari Tambaza nimesoma class moja na mtoto wa Ben baadae Dr. Mwinyi akajoin Tambaza A level. Pia class yetu Tambaza tulikuwa na mtoto wa Nyerere.

Ilboru A level nimesoma darasa moja na mtoto wa Warioba. UDSM nimesoma na Riz-1. Nikitembelea Geita, Biharamulo, Katoro, nalala nyumbani kwa Magufuli!. Hivyo I'm a well connected person, ningetaka uteuzi ningelobby!.

Kuna watu wa ajabu ambao hatuzimikii kabisa teuzi zozote za ubwete. Mimi ni mmoja wa watu hawa!.
P
 
Bwana Pascal Mayalla asante sana kwa ufafanuzi kuntu,mi ni mkongwe kiumri japo sikufikii,kwa ufupi watu tuliokuwepo enzi za kitimoto wote tunakukubali,kwa mtazamo wangu;Kitimoto ndio iliyokupa jina na heshima mjini

Kuhusu kudisco UDSM,chuo kizima kilifahamu kuwa umeonewa,ilikuwa ni aibu sana kwa yule mwalimu.

Humu JF pia tunakukubali hata hawa watoto wanaotukana ni utoto tu wasikukwaze.

Mimi binafsi naami wengi tumejifunza na tunaendelea kujifunza kupitia wewe.

Amani ya Bwana itawale maishani mwako,ipo siku tu utaitumikia nchi JWa mapana yake katika njia ambayo wengi tunaitamani itokee kwako iwe ni kwa teuzi au chaguzi
Mkuu mdukuzi, asante sana kwa maneno yako mazuri ya faraja kwangu mpaka machozi yamenitoka!.
Kiukweli kabisa kuwa JF, inakubidi kuwa na ngozi ngumu!, sometimes unatukanwa na vitoto vidogo vingine vinaweza kuwa ni vitoto vyako.

Thanks.
P
 
Mkuu Supu ya kokoto , sio kwamba najifagilia, bali ni ukweli halisi, kwenye tasnia yangu ya habari, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari very bold!, hii inapelekea nakuwa sialikwi kwenye events za habari kwa watu kuogopa maswali yangu, lakini maswali hayo, yanasaidia sana!. Mfano like swali langu kwa JPM kuhusu mikutano ya siasa, Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli ndilo limempelekea Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa!.

Hiyo ya kutogombea 2025, niliisha mshauri kitambo sana Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke ni bahati mbaya sana humu watu wenye uwezo to read in between the lines wanahesabika, watu wenye uwezo to reason the context ya mada wanahesabika, mtu bold anayeweza kupandisha bandiko kama hilo kumshauri Mama asigombee 2025 halafu yanatokea majitu majinga yanakuambia unatafuta u DC!, yanatia hasira.
P
Mkubwa kumbe nawewe kuna watu wanakutia hasira japo huwaoni, JF ina wapumbavu wengi sana ndiomaana verified user wanapungua,
 
By then hakukua na Law School. Ukimaliza tayari wewe ni Mwanashweria
Mkuu KUTATABHETAKULE , haijawahi kuwa hiyo, ilikuwa ukimaliza LL.B, lazima u petition kwa CJ ndio uwe wakili na sio ukimaliza tuu tuu unakuwa wakili direct. Hii ndio sababu imenicheleweshea kuupata uwakili. Ukiwa ni mtaka haki mno sometimes it's not good, kuna vitu vingine ni haki yako you just have to let them go, hilo mimi nimeshindwa.
Nimemaliza chuo kabla ya utaratibu wa law School, nikakabidhiwa LL.B yangu enzi za law School. Nikapetition nikakataliwa eti Degree inahesabika from the day it was conferred to you na sio mwaka uliohitimu!. Kiukweli ilikuwa kazi!, mpaka kuupata huu uwakili!. Acha tuu ni wind up huku kwenye media, ndipo niuanzie uwakili na kiukweli kwa jinsi nilivyo mbishi, kuna kazi inakuja!.
P
 
Back
Top Bottom