Pasco Mayalla ana vielement vya unabii afungue kanisa

Pasco yuko vizuri kwakweli sema ndio hivo hatujui kiundani what really the obstacle behind
Thanks for concern
Ila kuna mda nae anasahau kabisa professional yake anaanza kushabikia pumba za ccm kuwin teuzi.
Karibu Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!
He should learn the strong men are those who stend alone
Haya ni maneno ya faraja sana, sasa nalala na amani.
P
 
Bwana Pascal Mayalla asante sana kwa ufafanuzi kuntu,mi ni mkongwe kiumri japo sikufikii,kwa ufupi watu tuliokuwepo enzi za kitimoto wote tunakukubali,kwa mtazamo wangu;Kitimoto ndio iliyokupa jina na heshima mjini

Kuhusu kudisco UDSM,chuo kizima kilifahamu kuwa umeonewa,ilikuwa ni aibu sana kwa yule mwalimu.

Humu JF pia tunakukubali hata hawa watoto wanaotukana ni utoto tu wasikukwaze.

Mimi binafsi naami wengi tumejifunza na tunaendelea kujifunza kupitia wewe.

Amani ya Bwana itawale maishani mwako,ipo siku tu utaitumikia nchi JWa mapana yake katika njia ambayo wengi tunaitamani itokee kwako iwe ni kwa teuzi au chaguzi
 
Waungane na lema au sio?
 
Kabisa mkuu kuna watu wamekalia ofisi za umma wanakula kodi zetu kichwani zero,Pascal akili nyingi yuko nje ya mfumo,not fair
Sasa huko serikalini kila mtu ambaye upstairs akiwa njema ndio awe huko mbona itakuwa balaa huku uraiani,

Acheni magugu na ngano vikae sehemu moja ili mkulima afanye kazi yake.

Pengine paskali hata hataki utezi ni nyie tu ndio mnamchawia.
 
Basi kama ni kweli mwambie hali ya umeme na umshauri asigombee 2025 maana "punda amechoka" ni hayo tu.
Mkuu Supu ya kokoto , sio kwamba najifagilia, bali ni ukweli halisi, kwenye tasnia yangu ya habari, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari very bold!, hii inapelekea nakuwa sialikwi kwenye events za habari kwa watu kuogopa maswali yangu, lakini maswali hayo, yanasaidia sana!. Mfano like swali langu kwa JPM kuhusu mikutano ya siasa, Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli ndilo limempelekea Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa!.

Hiyo ya kutogombea 2025, niliisha mshauri kitambo sana Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke ni bahati mbaya sana humu watu wenye uwezo to read in between the lines wanahesabika, watu wenye uwezo to reason the context ya mada wanahesabika, mtu bold anayeweza kupandisha bandiko kama hilo kumshauri Mama asigombee 2025 halafu yanatokea majitu majinga yanakuambia unatafuta u DC!, yanatia hasira.
P
 
Mjomba wangu pascal,Mimi Nina Imani sana na maandiko Yako...watanzania mafuvu Yao yana layers nyingi sana kupelekea uzito kualewa mambo
 
Sasa huko serikalini kila mtu ambaye upstairs akiwa njema ndio awe huko mbona itakuwa balaa huku uraiani,
Asante sana othuman dan fodio , kila nikiliona jina lako nakumbuka Usman dan Fodio, ambae jina lake pia kuandikwa Uthman au Usuman, na kwa Kiarabu ni ʿUthmān Ibn Fūdī, alizaliwa December 1754, kijiji cha Maratta, mji wa Gobir, kwa kabila la wa Hausa na wa Sokoto, nchi yao akiitwa Hausaland ambayo sasa ni Nigeria, alikuwa ni kiongozi wa Sokoto na Fulani empire, alikuwa na nguvu fulani za mystic, powers, ndiye aliyeanzisha vita vya jihad kati ya mwaka 1804 hadi 1808, na kuifanya Nigeria kuwa ni nchi ya Kiislamu licha ya kuwa ndilo taifa la Africa linaloongoza kwa idadi ya Wakristu!, alikufa mwaka 1817, hivyo kila nikikutana na post yako yoyote, kwanza inakula like yangu!.

Hii JF ya sasa ina majitu majinga mengi, yasiyo na good thinking capacity, kama kila mtu mwenye akili nzuri atapaswa kuteuliwa nani wataleta maendeleo ya nchi hii?. Wanaoteuliwa waachwe wateuliwe, halafu sisi wengine, kama tuna akili nzuri, tuzitumie basi hizo akili zetu nzuri kuleta maendeleo kwenye taifa letu huku huku tulipo na sio mpaka tuteuliwe. Mfano mzuri ni mimi mwenyewe hapa nilipo namsaidia sana Samia kuliko hata ningeteuliwa nafasi yoyote!. Msaada wangu mkubwa kwa Samia, ni kumweleza kuwa everything happens for a reason!, hakuna kitu chochote kinachotokea bila sababu, hivyo ni watu wanache mimi nikiwemo ambao tunajua sababu za ni kwanini mtu wetu yule alitwaliwa!. Blaza ni karma ilikula kichwa!, hivyo tunawajibu wa kumsaidia Mama Samia kwa kumkinga asirudie makosa ya mtwaliwa kwa kugenerate bad karma ikaja kumponza na yeye akaishia... Wito Kwa Viongozi Wetu: Unapokosea, hata kwa kujikwaa tu ulimi, tujenge utamaduni wa kuwajibika ili kumuepushia Rais wetu kubeba mzigo wa karma hivyo kitendo tuu cha kutoa elimu ya karma kwa Rais Samia ni msaada mkubwa sana kwake kuliko ningeteuliwa kushika nafasi yoyote!.
Pengine paskali hata hataki utezi ni nyie tu ndio mnamchawia.
Sio pengine huo ndio ukweli. Watu hawajui nimesoma shule moja primary na Dr. Mwinyi, shule hiyo watoto wa vigogo wote ndio tulikuwa nao kuanzia Nyerere, Kawawa, Malecela na mawaziri wote!. Dr Mwinyi alinitangulia darasa, sekondari Tambaza nimesoma class moja na mtoto wa Ben baadae Dr. Mwinyi akajoin Tambaza A level. Pia class yetu Tambaza tulikuwa na mtoto wa Nyerere.

Ilboru A level nimesoma darasa moja na mtoto wa Warioba. UDSM nimesoma na Riz-1. Nikitembelea Geita, Biharamulo, Katoro, nalala nyumbani kwa Magufuli!. Hivyo I'm a well connected person, ningetaka uteuzi ningelobby!.

Kuna watu wa ajabu ambao hatuzimikii kabisa teuzi zozote za ubwete. Mimi ni mmoja wa watu hawa!.
P
 
Mkuu mdukuzi, asante sana kwa maneno yako mazuri ya faraja kwangu mpaka machozi yamenitoka!.
Kiukweli kabisa kuwa JF, inakubidi kuwa na ngozi ngumu!, sometimes unatukanwa na vitoto vidogo vingine vinaweza kuwa ni vitoto vyako.

Thanks.
P
 
Mkubwa kumbe nawewe kuna watu wanakutia hasira japo huwaoni, JF ina wapumbavu wengi sana ndiomaana verified user wanapungua,
 
By then hakukua na Law School. Ukimaliza tayari wewe ni Mwanashweria
Mkuu KUTATABHETAKULE , haijawahi kuwa hiyo, ilikuwa ukimaliza LL.B, lazima u petition kwa CJ ndio uwe wakili na sio ukimaliza tuu tuu unakuwa wakili direct. Hii ndio sababu imenicheleweshea kuupata uwakili. Ukiwa ni mtaka haki mno sometimes it's not good, kuna vitu vingine ni haki yako you just have to let them go, hilo mimi nimeshindwa.
Nimemaliza chuo kabla ya utaratibu wa law School, nikakabidhiwa LL.B yangu enzi za law School. Nikapetition nikakataliwa eti Degree inahesabika from the day it was conferred to you na sio mwaka uliohitimu!. Kiukweli ilikuwa kazi!, mpaka kuupata huu uwakili!. Acha tuu ni wind up huku kwenye media, ndipo niuanzie uwakili na kiukweli kwa jinsi nilivyo mbishi, kuna kazi inakuja!.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…