Pata ushauri, michango na mawazo ya ufugaji wa bata wa kienyeji kibiashara

Pata ushauri, michango na mawazo ya ufugaji wa bata wa kienyeji kibiashara

Natumaini watakuja wajuvi watakupa Msaada unaohitaji . kilichonishangaza ni kukimbia ufugaji wa kuku kwa sababu ya changamoto . je kwenye bata hutakimbia tena
 
Natumaini watakuja wajuvi watakupa Msaada unaohitaji . kilichonishangaza ni kukimbia ufugaji wa kuku kwa sababu ya changamoto . je kwenye bata hutakimbia tena
NImejaribu kidogo ndani ya mda mfupi sikuona changamoto yoyote, kwanza wakihatamia wanatotoa mayai karibia asilimia 90, kuhusu usafi wa banda ... wao mda wote wanahitaji kuwa kwenye sehemu yenye minyoo wanakula.... kuhusu magonja sijaona wakiugua .... kuhusu soko ndo sijajua likoje?
 
Komaa na unachokijua na ambacho una uzoefu nacho.Ufugaji wa bata nao utakutoa resi kama hutakuwa na ujasiri wa kupambana na changamoto.

Kumbuka hakuna biashara isiyo na changamoto !!
Ninachokijua ndo hicho kimenitoa berenge ..
 
mkuu fanya hvi ,nenda duka la binadamu omba vidonge vya antibiotics rangi mbili (pink and black) ,chukua maji kidogo kama 1/1 liter (nusu ya robo) koroga unga wa hivyo vidonge kwenye maji hayo masafi, chuku sirinji jaza yale maji, chukua kifaranga kimoja kinyweshe angala matone (5drops) .Zingatia haya hiyo 1/8ltr kwa vidonge 3 na kwa vifaranga 6-8. mm nilifiwa sana na vifaranga tena wengine wanakufa wakiwa na mwezi tayari. Hii dawa pia inatibu ndui niliitumia kutibu vifaranga vyangu vya bata mzinga. All the best. Vifaranga wapewe angalau siku ya 3 baada ya kuzaliwa, kama umechelewa wape hata sasa hivi.
 
Nashukuru Kwa majibu hayo, sema sijajua tatizo in nini au Kwa sababu naaoza kufuga,,,!! cha kushangaza hawa bata nilisha watenganisha walikua wanakaa kwenye mabanda maalumu na mama zao!!

Mmoja alikua na vifaranga 16 wote wamekufa, na mungine alikuna na 18 wamebakia 8 tu,,

Vitu ambavyo nahisi vimesababisha, usafi ni banda,

Pili nilikua nalaza kiroba nawawekea pumba then nahis wamekula kinyesi chao,

Tatu nahisi baridi Kwa sababu sikuwaongezea joto lolote usiku kwenye hii winter..

Mfa maji haishi kutapatapa.!!
Mkuuu pole na majukumu.MImi ni mfugaji wa bata ila nafuga bukini na perkin.Nikushauri hao bata wa kawaida hasa akiwa na watoto hakikisha wanakula chakula kidogo na kisiwe kingi sana wakila sana wanaweza wakafa kkwa ulafi then hakikisha unatenga maji yao vizuri na ubadilishe kila baada ya masaa sita au kila siku.tatu hakikisha banda ni safi ili kuzuia magonjwa.Bata hawahitaji joto la ziada boss maana hawa ni ndege maji
 
Mkuu kuna aina nyingi za bata unatala uanze kufuga wa aina gani?

-Ndumilakuwili-
Waliozoeleka ni hawa ..
Bata wa kawaida walio sehemu nyingi (Sijui jina lao.)
images

Bata bukini
images

upload_2017-7-17_13-51-41.jpeg

Bata mzinga
upload_2017-7-17_13-49-33.jpeg
 
mkuu fuga bata bukini mkuu wanalipa sana mkuu
mimi nimewafuga for 11 years now bata mmoja analisha wenzake 20 kwa mwaka mzima
 
mkuu fuga bata bukini mkuu wanalipa sana mkuu
mimi nimewafuga for 11 years now bata mmoja analisha wenzake 20 kwa mwaka mzima
Safi sana! sokoni ana bei gani .. nawe uko wapi unipatie mbegu?
 
Waungwana, kwenye ufugaji wa kuku nimekumbana na changamoto nyingi sana. Sasa nimeamua niuze waliobaki nianze ufugaji wa bata. Kuna mambo sijajua vizuri.
1. Soko lake likoje?
2. Kuna changamoto zipi?
Kuna jamaa mmoja nilikutana naye nanenane last year alikuwa na bata wengi sana, ila hakuwa na mda wa kutoa maelekezo kwa sababu wanunuzi walikuwa wengi hivyo mda mwingi alirudi shambani Ukerewe kufuata mzigo.
Naomba alowahi kufanya biashara hii asaidie maelekezo hapa, kwa faida ya kwangu na wasomaji wengine pia.
Km inawezekana naomba tutajie changamoto kubwa ulizokutana nazo utakua umetusaidia sisi wenye ndoto za kufuga baadae
 
Mimi bata wangu nawatibu kwa kuwaweka katika banda safi muda wote, chakula na maji safi.
 
Adui mkubwa wa vifaranga wa bata ni panya. Katika miezi miwili ya mwanzo jitahidi kuwaweka kwenye banda ambalo haliwezi kabisa kuingiza panya. Panya ana uwezo wa kuua vifaranga zaidi ya 10 kwa wakati mmoja akiwatoboa macho.
Ili kusaidia wakue haraka jaribu kuwapatia chakula cha kuku cha starter kwa hiyo miezi miwili ya mwanzo.
Pole kwa hasara iliyo kukumba.

Sent from my GT-N8000 using JamiiForums mobile app
 
Mjasiriamali huwa ni "risk taker" hivyo pambana tu na hivyo changamato za kuku. Kama una soko la uhakika nakuomba usiache kufuga kuku.
yote kwa yote shikamoo Tutor B
 
Back
Top Bottom