TANZIA Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

TANZIA Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

Mwili wa aliyekuwa mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), mhandisi Patrick Mfugale umewasili katika viwanja vya hospitali ya Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuagwa.

Viongozi mbalimbali wamewasili katikahospitali hiyo akiwemo naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Godfrey Kasekenya, katibu mkuu wa Wizara hiyo, Joseph Malongo, mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri na wabunge mbalimbali.

Pia wapo viongozi mbalimbali wa Tanroads, wawakilishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa dini pamoja ndugu, jamaa na marafiki.

Kwa mujibu wa ratiba mwili wa Mfugale utapelekwa Uwanja wa ndege wa Dodoma saa 10:00 jioni kwa ajili ya kusafirishwa kuelekea jijini Dar es Salaam ambapo utaagwa tena katika ukumbi wa Karimjee kesho.

Mfugale alifariki dunia Jumanne Juni 29, 2021 saa 5 asubuhi katika hospitali ya Benjamin Mkapa.

PIA SOMA:
- TANZIA - Patrick Mfugale wa TANROADS afariki dunia Jijini Dodoma

Source: Mwananchi
Sahihisha kichwa cha habari...mi nilidhani ni yeye kumbe mwili.
 
Pamoja na Mambo mengine hebu turudi nyuma kidogo.
Mfugale alizaliwa December 1953
Alipashwa astaafu 2013 December.
Ni kitu gani kimemfanya anganganie madaraka ilhali Tanzania Kuna ma graduate wengi sana wanaoweza kukalia kile kiti?
Kama kulikua hakuna wa kumrithi, inamaana wataleta beberu au mchina pale.
Enyi wahanga mliopo serikalini na mashirika ya Uma , hebu mjiheshimu mustaafu umri ukifika ili mkafaidi hela zenu pamoja na kucheza na wajukuu.
Habari hii iwafikie hata wabunge na mawaziri.
Mtu unafia board room kisa huwezi ku handle stress za dot.com.
Mtu bado unasaka pesa ilhali hata Cha asubuhi unakisikia kwenye kipindi Cha tiGO. Hiyo pesa Ni ya Nini Kama huwezi kutafuna vipaja?
mrangi
Mshana Jr
mama kubwa
Bushmamy
Alikuwa anapenda kuongea na vijana wengi na baadhi walikuwa wanamuuliza hili.....na alikuwa anawajibu bila kusita kwamba ataachaje kufanya majukumu ya kitaifa na wakati vijana hamjitambui? Kwa kiasi usemi wake una mantiki vijana wengi ni pumba + mashudu....angalia tu hata comments nyingi hapa jukwaani. Jokes all the time like small girls!!
 
Unatakiwa muda mwingine ufurahie maisha ili uweze kuishi miaka mingi, angalia kama Jakaya yuko na afya njema.
 
Huyu Mzee tumpe heshima yake anayostahili, ni rahisi kwa vijana ku joke na kutukana ila mchango wa Mhandisi Mfugale hapa Tanzania ni mkubwa sana kuliko hawa wanaombeza na ambao nina hakika wengi hawaufahamu mchango wake. Sasa tunataka tumsifu mzungu aliyetutawala au tumsifu huyu Mtanzania mwenzetu aliyefanya kazi inayoonekana tena kwa uadilifu na kwa jitihada kubwa??
 
Mwili wa aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale utaagwa leo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Baada ya hapo mwili utapelekwa nyumbani kwa mwendazake, Kimara Temboni, kisha Julai 3 utapelekwa Ifunda, Iringa, na kuzikwa huko Julai 5, 2021.
 
Jana nilikuwepo pale Benjamini Mkapa pamoja na viongozi wengine wa chama na serikali, na waombolezaji wengine, kutoa heshima zetu za mwisho.
 
Aliyetoa hotuba kwa upande wa watoto nimeshindwa kuendelea kuisikiliza. Looh " Huyu mzee.... lah. Watoto tunao.
.
 
Huyu alipandishwa sana chat na JK. Alipokuwa kwa JPM akazidi kumpandisha chati na inasemekana akamgeuka hata JK. Sasa undani wa kifo chake ukoje? Mbona ilikuwa ghafla vile! Ni corona kweli ile?
 
Huyu alipandishwa sana chat na JK. Alipokuwa kwa JPM akazidi kumpandisha chati na inasemekana akamgeuka hata JK. Sasa undani wa kifo chake ukoje? Mbona ilikuwa ghafla vile! Ni corona kweli ile?
Unapo sema akamgeuka hata jk unamaanisha nini alimgeuka ktk mambo gani?
 
Jamani Mzee wa Msoga ni mstaafu sasa. Ameachana siku nyingi na siasa za moja kwa moja za kujibishana kisiasa majukwaani, tumuache ale pensheni yake na apumzike na wajukuu zake.
 
Back
Top Bottom