Paul Kagame katoa onyo kwa Kiswahili, walengwa mmepata ujumbe?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
Rais Paul Kagame alikuwa anaapisha mawaziri wapya hapo jana mapema. Alianza kutoa hotuba yake kwa lugha ya Kinyarwanda, lakini baadae akahamia kwenye lugha ya Kiingereza na baadaye akatoa kitisho kizito kwa lugha ya Kiswahili. Wengi wetu tumeona hicho kipande chenye lugha ya kiswahili kikisambaa huko mitandaoni hasahasa kwa raia wa Tanzania na Kenya. Kitendo cha kusambaa mtandaoni kwa kasi hivi, inaonesha kabisa walengwa wa ujumbe ni watu gani.

Kwenye FASIHI njia moja kuu ya kufikishia ujumbe ni kuifahamu HADHIRA, lakini kubwa zaidi ni kufahamu lugha ambayo HADHIRA hutumia. Siku zote kimetumika Kinyarwanda na Kiingereza, lakini leo hii na Kiswahili juu, tena sehemu ambayo anatoa vitisho. Kwenye Dakika ya 27, ameanza kuwaliza mawaziri wake kama wanafahamu lugha ya kiswahili, wakamjibu wanelewa, ndipo akaanza kuzungumza kiswahili.

Huu ujumbe siyo wa wanyarwanda, wazungumzaji wakubwa wa lugha ya kiswahili wanafahamika, hivyo hicho kitisho ni ujumbe kwenu. Hajataja mhusika, mimi binafsi sitamtaja, lakini naamini walengwa mapema leo, watakuwa washafikiwa na huu ujumbe.

Alichokisema Rais Paul Kagame ni kwamba ukubwa wa pua siyo wingi wa kamasi. Kwamba Rwanda doesn't have the means, but they have the methods (ways). Hivyo kijiografia Rwanda ni nchi ndogo isiyo na rasilimali nyingi, lakini wao siyo migomba mifupi kama wanavyofikiriwa. Binafsi naamini, haivuki miaka miwili (2) kuna mtu kwenye huu ukanda wetu wa maziwa makuu atatoa kilio kikubwa sana.

Your browser is not able to display this video.
 
Tuko busy na uchaguzi 2025.

Huko barabarani tuko busy na maving'ora 24/7 maspeed na kuweka mafoleni, sijui huwa tunawahi wapi na tunawahi nini maana yale ya msingi tunayopaswa kuyafanya hatuyafanyi..

Ruto anapambana kuongeza idadi ya diaspora wakenya duniani, wakati huo anaendeleza utaratibu wa kuzalisha skilled and intelligent workforce ya kenya ili itapakae kila kona duniani..

Tupo busy kubrainwash vijana na kuendelea kuwa chawa wa viongozi, tuko busy kuendelea kuongeza workforce pumbavu inayowaza siasa, tuko busy kufanya vijana wawe tegemezi wa baba zao wezi waliokwenye system.. We paralysized kila mahala na maadui wetu wanafuatilia nyendo zetu kila siku ili siku ikifika watuslave.
 
Na wewe usiwe mjinga,Tanzania haijalala kiasi hicho japo hatujafanya vya kutosha naona Kama unahemka kwa vijimaneno vya mfa maji hapo juu..

Tungekuwa hatufanyi kitu Leo hii tusingekuwa na urali wa biashara kuwazidi wote EAC yaana balance of trade yetu na majirani wote Ni surplus in terms of quantity and value licha ya changamoto zote..
 
Tatizo mnashinda mitandaoni badala ya kuwa busy
 
Tatizo vijana wa hivyo kama mlalamikaji hapo juu Yuko busy mitandaoni na siasa kuliko shughuli za uzalishaji
 
Ujasusi wa Kidola na kiuchumi alishamaliza Mkuu Yericko Nyerere.

Sisi tuko kwenye ujasusi wa ccm kwanza. Mengine mtajuana wenyewe.
 
Kagame kama kweli anajiamini kwanini asianzishe hiyo vita anayojitapa kila siku yuko vizuri?

Huku kujisifu kwake kila siku bila vitendo vyovyote pia kunaweza kuwa ni dalili ya mtu asiyejiamini, anajihami tu, ili aachwe aendelee kuharibu amani ya eneo la maziwa makuu.

Huyu naona anaweza kuwa anaongoza kwa mdomo na ujuaji kuwashinda marais wote wa eneo hili, lakini sio zaidi ya hapo, kwasababu kama anaona anachokozwa kila siku kwanini asiwafundishe adabu hao wachokozi?
 
Mama kamuweka BASHUNGWA wizara ya Ulinzi hakika atavuna alichokipanda kwa Mnyarwanda huyu
 
Hali yake ni mbaya sana tangu Sir Ruto kuingia imekuwa pigo kwake alijaribu kumtumia mtoto wa museveni kuchonganisha ikabuma,ni kati ya marais wapumbavu EAC anayetumika na mabeberu bila kificho
 
Unawezaje kujisifia kwa kupata 3 kati ya 15 unazostahili kupata hata kama umepata zaidi ya wengine? Suala si kuwazidi wengine, bali ni kupata kile unachostahili kulingana na uwezo ulio nao..
 
Aanzishe vita mara ngapi? Wakati congo ameshalianzisha?
 
Kunguni ya mama ipo kazini.
Endeleeni kumpamba tu ila ukweli ata nyie mnauona. Tumekuwa madaraja kwa watawala wanafanya tu kila wanachojisikia ata kama kinaliumiza Taifa.
Ipo siku mwenyezi Mungu atawapigia wale wasio na nguvu ya kutenda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…