Paul Makonda akutana na Viongozi wa madhehebu na Taasisi za dini, asema anayoyafanya Rais Magufuli yanazidi maelekezo ya ilani ya CCM

Paul Makonda akutana na Viongozi wa madhehebu na Taasisi za dini, asema anayoyafanya Rais Magufuli yanazidi maelekezo ya ilani ya CCM

Titicomb,
Simameni kwenye katiba mliyoapa kuilinda, fuateni sheria kanuni na taratibu tulizojiwekea kama nchi, tuwe na level playing field kwa vyama vyote vya siasa kisha useme/uandike hayo uliyoandika. Siyo unamfunga mikono na miguu mshindani wako halafu unajisifu unajua kurusha ngumi.
 
Simameni kwenye katiba mliyoapa kuilinda, fuateni sheria kanuni na taratibu tulizojiwekea kama nchi, tuwe na level playing field kwa vyama vyote vya siasa kisha useme/uandike hayo uliyoandika. Siyo unamfunga mikono na miguu mshindani wako halafu unajisifu unajua kurusha ngumi.
Unakosea kuniambia mimi huo ushauri, sema wafuate ...
Mimi sipo chama chochote au serikalini ndio maana nawakosoa wote, au nasifia mazuri.
 
Listing ya viongozi was dini makanjanja
1. Pengo
2. Askofu wa TEC anaitwa Nyamwisobgo
3.Gamanya
4 shekhe wa Dar
5. Askofu Malasusa
6. Ongezea

Hawa hawataiona pepo,
Hiyo pepo unaionyesha wewe !?
 
Kwani sisi hatuna akili mpaka waanze kutushawishi sijui ujinga gani, hawa mashekhe wajinga wajinga wanaudhalilisha uislamu
Huwezi kuwa Sheikh halafu uuwe mjinga !
 
Listing ya viongozi was dini makanjanja
1. Pengo
2. Askofu wa TEC anaitwa Nyamwisobgo
3.Gamanya
4 shekhe wa Dar
5. Askofu Malasusa
6. Ongezea

Hawa hawataiona pepo,
Uyu gamanya ni tapeli aliwatapeli vijana sijui anaanzisha mashamba watalima matokeo yake kaomba serekali ardhi then hao vijana hakuna walichopata
 
Kesho kutwa machinjio ya kisasa ya nguruwe yakitangazwa kujengwa Dar, waislamu tutataka viongozi wetu wa BAKWATA watangaze pia kuunga mkono.
Dhamira ni kuunga mkono kila kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano.
Nguruwe haitaji kuchinjwa, huuliwa ! Jipange !
 
Nilidhani viongozi wa dini hawapaswi kuingilia masuala ya serikali na siasa, lakini kumbe sikujua kwamba kama wanaisifia na kuiunga mkono serikali, basi hapo ni ruksa kwao, lakini kama wanaikosoa na hawaiungi mkono serikali, hapo ni marufuku kwa wao kujadili masuala ya siasa na serikali inabidi wabaki tu na masuala ya kiimani na dini zao. Sawa nimeelewa sasa.
 
MODS wakati mwingine huwa mnafanya mambo yatawaonyesha ni vilaza. Sio kila thread inayomhusu mtu mmoja ina maudhui ya aina moja hivyo mnaunganisha.
Mmeunganisha thread yangu na hii hadi imepata picha tofauti.
Acheni hizo, mnachofikiri nyie sio wafikiricho wengine. Kuna dalili Fulani kama Makonda ana mkono kwa baadhi ya Mods jee JF imeanza kuwa sehemu ya "opportunity"?
 
Nilidhani viongozi wa dini hawapaswi kuingilia masuala ya serikali na siasa, lakini kumbe sikujua kwamba kama wanaisifia na kuiunga mkono serikali, basi hapo ni ruksa kwao, lakini kama wanaikosoa na hawaiungi mkono serikali, hapo ni marufuku kwa wao kujadili masuala ya siasa na serikali inabidi wabaki tu na masuala ya kiimani na dini zao. Sawa nimeelewa sasa.
Hizi double standard zinaiumbua sana Serikali
 
Mange aliambiwa mwaka jana ndio wa mwisho kwake kuwasema watu. Mpaka leo kimyaaa.
Ha haha wambie wamchokoze waone moto wa binti yule! Mie siungi mkono kauli zake za matusi kwa watu lakini kuna nyakati ananifurahisha kwa kuwa mkweli na anaweza kukomesha kiongozi yeyote mwenye tabia mbovu kwa kuchimba historia yake chafu na kumbamiza kisawasawa akaufyata.
Hebu waambie wamchokoze waone!
 
Ha haha wambie wamchokoze waone moto wa binti yule! Mie siungi mkono kauli zake za matusi kwa watu lakini kuna nyakati ananifurahisha kwa kuwa mkweli na anaweza kukomesha kiongozi yeyote mwenye tabia mbovu kwa kuchimba historia yake chafu na kumbamiza kisawasawa akaufyata.
Hebu waambie wamchokoze waone!
Naona katulia anapambana na majukumu yake binafsi.
 
Anaandika Malisa GJ

John Stuart Mill aliwahi kusema ukizoea kujipendekeza sana unaweza kumtukana mtu unayejipendekeza kwake ukidhani umemsifia.

Dar - Mbeya 900 Kms.
Dar - Mwanza km 1200 Kms.
Mwanza - Musoma 400 Kms.
Dar - Mtwara 600 Kms.
Iringa - Dodoma Km 240
Dodoma - Arusha Km 260

Na nyingine nyingi zilizojengwa kabla ya JPM. Kimsingi utawala uliojenga barabara nyingi zaidi tangu uhuru ni utawala wa Kikwete. Alianzisha miradi mingi ya barabara hata alipoondoka aliacha mingine ikimaliziwa ambayo JPM alichofanya ni kuizindua tu.

Mwaka 2005 nilitoka Arusha kwenda Dodoma kwa basi, ilikua safari ya kutwa nzima kuzungukia Chalinze. Leo ukitoka Arusha asubuhi, saa 4 unakunywa chai Dodoma kwa kupitia Kondoa. Wananchi wa Iringa nao kwenda Dodoma walilazimika kuzunguka Morogoro. Lakini kwa sasa ni mwendo wa masaa machache kupitia Mtera. Unaweza kutoka Iringa kwenda Dodoma kufanya shopping na ukageuka tena Iringa siku hiyohiyo.

Tuache kujipendekeza. Lets give credit where credit is due. JK pamoja na madhaifu yake mengine lakini ndiye aliyeunganisha mtandao wa barabara nchini kuliko Marais wote waliomtangulia na hata huyu aliyemfuatia.

JPM ana yake aliyofanya lakini si kwenye barabara. Kwenye ndege apewe credit (regardless zinajiendesha kwa hasara). Kwenye reli apewe credit (japo ni mradi wa hasara). Lakini kwenye barabara NO THANK U. Hakuna nominal impact.

JK alitaka kuwa na mtandao wa barabara wa kuunganisha mikoa yote jirani. Akaanza Dom to Iringa (via Mtera), Arusha to Dom (via Kondoa), Singida to Tabora (via Itigi) etc.

Lakini ndoto hii ya JK imezimwa. Barabara ya Singida - Tabora ambayo JK alishajenga zaidi ya 250Kms, JPM ameshindwa kumalizia 80Kms tu zilizobakia. Kipande kinachounganisha Morogoro - Tanga JK alikijenga, but JPM kashindwa kumalizia 70Kms tu za Turiani - Handeni. Kipande cha Sikonge - Chunya kimetelekezwa, Njombe - Moro (via Lupembe) kimetelekezwa, Ifakara - Songea kimetelekezwa.

Leo tunaambiwa JPM ndio anaongoza kwa kujenga mtandao wa barabara? Labda hizi za Goba na Kinyerezi, ambazo hata hivyo zilijengwa na JK yeye kafanya kumalizia tu.!
 
Back
Top Bottom