Paul Makonda amtaka Gwajima afike ofisini kwake kutolea ufafanuzi juu ya kumkashifu Pengo

Paul Makonda amtaka Gwajima afike ofisini kwake kutolea ufafanuzi juu ya kumkashifu Pengo

.......Martina.....ni vema ungemwelewa Pengo.....Nilivyomuelewa mimi .....sio msaliti hata kidogo....tambua aliruhusi barua isomwe jimboni kwake kitu ambacho angeweza kukataa......pili walipohamua kikao kilifanyika Arusha yeye hakuwepo alikuwa ITALY na baadae INDIA.....na alisema kabisa anachotoa ni MAWAZO YAKE BINAFSI....kama yeye....alipokosea ni wapi sasa.......jamani tuweke dini zetu pembeni tuuvae Utanzania........hili taifa ni letu sote...sio la wakristu peke yao....tambua wapo wasioamini Mungu, waislam na wengine.....kila mtu akija na maazimio kutakuwa na nchi kweli..... ........SOMA ALICHOKISEMA LEO

UFUATAO ni ujumbe mfupi wa Muadhama
Polycarp Kardinali Pengo alioutoa leo katika
Kanisa la St. Joseph jijini Dar es Salaam
kuhusiana na waraka wa maaskofu uliotolewa
hivi karibuni kwa Wakristo nchini
kujiandikisha kikamilifu na kisha kuikataa
Katiba Inayopendekezwa wakati wa kura ya
maoni kwa vile haikujadiliwa kiuadilifu.
"Maaskofu hatuna mamlaka ya kuwaamulia/
kuwalazimisha waumini wetu wafanye
uamuzi gani kuhusu katiba, kuwaamulia ni
kuwadharau kuwa hawawezi kufanya uamuzi
sahihi wao wenyewe na kuingilia uhuru wao.
Waraka huu unaleta utengano katika taifa
kuwa Wakristo, tumechukua uamuzi dhidi ya
serikali na wengine....
Tuwaache waumini wafanye uamuzi kwa
tafakari yao binafsi bila shinikizo letu.....
Wakati hili linajadiliwa nilikuwa Italy katika
kusimikwa makardinali na baadaye India,
wengine wakavumisha nimelazwa,..wengine
nimefariki, lakini namshukuru Mungu hizo ni
dua za kuniongezea maisha marefu na afya
(makofi).
Nililetewa waraka nikausoma, umepitishwa
baada ya tafakari kubwa nauheshimu. Lakini
nadhani tuwaache waumini wafanye uamuzi
kwa uhuru baada ya kutafakari....
Si sahihi tukaenda katika katiba kama
Wakristo kwa shinikizo la kupinga katiba...
Wawe huru anayepinga kwa hiari yake
anayekubali kwa dhamiri yake....
Sidhani kama viongozi wa dini sasa tuna amri
ya kulazimisha uamuzi juu ya katiba....
Hivi kila dini ikianza kuchukua misimamo
kuhusu mambo ya kisiasa Tanzania
itabaki???

alichokosea pengo ni kilekile alichokosea kilaini,infwakti sio makosa ni makusudi,pengo kaulizwa waraka usomwe au usisomwe alishindwa nini kusema usisomwe?kama sio unafiki halafu baada ya kupewa za kichwa na gwajima ndio anaongea hayo matakataka,hamna kitu hapo kafeli kama kilaini.kilaini nae pesa za sadaka miaka 3 kanisa halijui kama kuna sadaka hata kununua spika na mic basi angalau waumini wakimwimbia bwana sound zitoke stereo hakuna,lahauraa salaree
 
Makondaaaaaaa!!hadi aibu! Mbona yeye kamtukana mzee lowassa matusi ya nguoni na hakuhojiwa na yeyote,yaani anatafuta sifa kijinga kabisa,hata huyo gwajima akienda nitamuona mwehu.
 
sasa nae anataa kuingiliaa uhulu au kazi za chombo kingine kama nii kosa kuna watu wanafanya hivyol huyu nae kichwa.uwa.kinapata motoo.saana
 
chizi makondo nae anataka nini?
si afadhali Gwajima anatuhumiwa kwa maneno makali dhidi ya mwingine kuliko huyu makonda kumpiga mzee wetu mheshimiwa sana Warioba?
.
 
Makonda hana authority ya kumuhoji Gwajima, au hajajua kazi anazotakiwa kufanya na mipaka yake?
 
hivi huu mvinyo wa madaraka mbona unalewesha haraka hivyo? Yaan huyu pongo hayo madaraka kapewa na nani kwenye ulimwengu huu? Daah! Ama kweli tz ni ajabu la kipekee kwa hii dunia
 
Muvi inaendelea wakuu,

Wakati Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akiwa amejisalimisha kwenye Jeshi la Polisi kwa mahojiano hali iliyopelekea Askofu huyo kupoteza fahamu; naye Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amemtaka Askofu huyo aripoti ofisini kwake keshokutwa kutoa maelezo kuhusiana na tuhuma za kumkashifu kiongozi mwenzake wa dini.


Makonda amemwandikia barua Askofu Gwajima akimtaka kufikia ofisini kwake kutoa ufafanuzi juu ya maneno makali dhidi ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki.

Katika barua yake, Makonda alisema ofisi yake inataka kufahamu kama uhuru wa kuabudu kikatiba ni kutokuheshimu watu wengine. “Hatuamini kama imefika wakati kwenye nyumba za ibada kumegeuka sehemu ya kutukana na kuwasema watu badala ya kuhubiri habari njema. Tunataka kujidhihirisha malengo hasa ya kutumia maneno hayo ni nini.”

11081016_360745177443838_2390948105818373976_n.jpg




Dc wangu Paul Makonda, nakupongeza kwa hili...!
 
Makonda kakonda kichwa alipopewa u-dc. Namshauri Gwajima asiende tuone game na movie itakayochezwa hapa
 
Dc hana kazi yoyote katika wilaya zaidi ya porojo tu.
Nini job description ya dc kama makonda?
 
alichokosea pengo ni kilekile alichokosea kilaini,infwakti sio makosa ni makusudi,pengo kaulizwa waraka usomwe au usisomwe alishindwa nini kusema usisomwe?kama sio unafiki halafu baada ya kupewa za kichwa na gwajima ndio anaongea hayo matakataka,hamna kitu hapo kafeli kama kilaini.kilaini nae pesa za sadaka miaka 3 kanisa halijui kama kuna sadaka hata kununua spika na mic basi angalau waumini wakimwimbia bwana sound zitoke stereo hakuna,lahauraa salaree

ndugu unachanganya mambo.....kama sio kurukia uliyoyaelewa kijuujuu......MAMLAKA YA PENGO YAPO NDANI YA JIMBO LA DSM,,,,KWA TAARIFA YAKO HAKUSHIRIKI MAZUNGUMZO YA MWISHO YALIYOFANYIKA ARUSHA.....ALIPOLETEWA WARAKA ALIUSOMA na akaupongezwa kwa jinsi ulivyoandikwa vizuri,,,,,,na akaruhusu usomwe kwenye parokia na vigango vyote DSM.....ILA AKATOA MAONI YAKE BINAFSI,,,,,,,NA NAAMINI ANGEHUDHURIA KIKAO CHA MWISHO CHA ARUSHA ANGEYASEMA......SASA ALIPOKOSEA NIWAPI,,,,,,,HUJAWAHI SIKIA HATA RAIS ANASEMA KITU THEN ANAPENDEKEZA KITU KAMA JAKAYA BINAFSI NA SIO JAKAYA RAIS,,,,,,,,PENGO KATOA MAONI YAKE KAMA PENGO NA HAYO MAONI SIO MSIMAMO WA KANISA KATOLIKI KTK JAMBO HILO........MBONA MUMTUKANE,.......YAKILAINI HAYAHUSIKI KTK HILI
 
Makonda atakuwa anahitaji maombi tu Gwajima, hilo la Pengo ni janja yake tu si mnakumbuka hata wazee wake Sitta na Mwakyembe huombewa na Gwajima wawapo matatizoni!
 
hivi kuna sheria gan inayomtaka mtu kwenda kujieleza kwa mkuu wa wilaya kama anavyotaka makonda na kwani Gwajima asipoenda kutatokea nini?.Naomba mnaojua mnisaidie kwa hili tafadhali
Mkuu, haya ni mambo ya double standards huku mkuu wa wilaya huku polisi. si sheria zipo jamani na polisi wameanza tayari. Labda angekuwa kaanza yeye. Je, akikataa kwenda itakuwaje maana hajasema lini na saa ngapi.
 
Vip kaenda na mabaunsa wake?yaani wale jamaa anavyowapigisha mbio sijui anawalipa kiasi gani
 
ndugu unachanganya mambo.....kama sio kurukia uliyoyaelewa kijuujuu......MAMLAKA YA PENGO YAPO NDANI YA JIMBO LA DSM,,,,KWA TAARIFA YAKO HAKUSHIRIKI MAZUNGUMZO YA MWISHO YALIYOFANYIKA ARUSHA.....ALIPOLETEWA WARAKA ALIUSOMA na akaupongezwa kwa jinsi ulivyoandikwa vizuri,,,,,,na akaruhusu usomwe kwenye parokia na vigango vyote DSM.....ILA AKATOA MAONI YAKE BINAFSI,,,,,,,NA NAAMINI ANGEHUDHURIA KIKAO CHA MWISHO CHA ARUSHA ANGEYASEMA......SASA ALIPOKOSEA NIWAPI,,,,,,,HUJAWAHI SIKIA HATA RAIS ANASEMA KITU THEN ANAPENDEKEZA KITU KAMA JAKAYA BINAFSI NA SIO JAKAYA RAIS,,,,,,,,PENGO KATOA MAONI YAKE KAMA PENGO NA HAYO MAONI SIO MSIMAMO WA KANISA KATOLIKI KTK JAMBO HILO........MBONA MUMTUKANE,.......YAKILAINI HAYAHUSIKI KTK HILI

yaani wewe sio mzima,alitakiwa aseme usisomwe! full stop khah! sasa hapo ndio umeandika nini,eti amelidhia usomwe lakini akatoa maoni yake, ndio huo unafiki, unaona watu wajingawajiga?kwenda na pengo wako wanafiki wakubwa
 
yaani wewe sio mzima,alitakiwa aseme usisomwe! Full stop khah! Sasa hapo ndio umeandika nini,eti amelidhia usomwe lakini akatoa maoni yake, ndio huo unafiki, unaona watu wajingawajiga?kwenda na pengo wako wanafiki wakubwa

kubishana na mtu ambaye hajitambui nikupoteza muda na rasilimali
 
Back
Top Bottom