Paul Makonda amtaka mwandishi kumuuliza mama yake baada ya kumhoji tuhuma za kumshambulia Lissu

Paul Makonda amtaka mwandishi kumuuliza mama yake baada ya kumhoji tuhuma za kumshambulia Lissu

Yaani kuna watu wana akili za hovyo sana kudhani jibu la makonda ni sahihi.

Kwenye ulimwengu wa uandishi wa habari. Kuna kitu kinaitwa kubalance story.

Na hii story ya makonda huyo mwandishi akiamua kumkaanga makonda anaweza kuweka bonge la headline.

Mwandishi ataweka tuhuma dhidi ya makonda kama ilivyosema na Lissu.

Kisha atasema alipoulizwa Paul Makonda juu ya tuhuma hizo. Hakukanusha wala kuonesha kusikikitishwa zaidi alijibu "kamuulize mama Yako".

HIvyo mwandishi anaweza kusema mengi mabaya dhidi ya Makonda kwa sababu makonda alipewa nafasi kujibu hoja badala hata kuikana kwanza kisha kutoa maelezo mengi. Amekaa kimya na kutoa kejeli.

Ingekuwa mahakamani naamini unajua hakimu angefanya nini. Umesomewa shitaka badala ya kulikana kwanza, umeishia kutoa kejeli
Kuna Watanzania wengi sana wajinga hayo mambo ya due diligence, ku balance story etc, hawaelewi. Au haeataki kuelewa.

Ndiyo kwanza wanamsifia Makonda.

Hata hawaoni tatizo kiongozi wa chama kitaifa kujibu kihuni hivyo.
 
Muhanga kumtaja kila mmoja anaemuhisi kuhusika bila uthibitisho usio na shaka ndani yake ndio suluhu ?



“Lakini kwenye suala la ubinaadam na kulinda uhai wa mtu wote tunakua kitu kimoja…..”

Kwahiyo ubinaadam ni upi kwenye kudhalilisha utu wa mtu?

..Lissu amewataja Magufuli, Kipilimba, na Makonda.

..Katika hao watatu nadhani Makonda is the odd one.

..Wanaopaswa kuchunguza, kukamata, na kushtaki, no jeshi la Polisi na Dpp.

..Serikali itoe taarifa kwanini waliomshambulia Lissu hawajakamatwa mpaka leo hii.
 
..sio swali la kipumbavu.

..labda kama tukio la Lissu halijakugusa. Lakini kama Mtanzania mpenda haki tukio lile kinapaswa likuguse.

..Mimi ningekuwa Paul Makonda kitu cha kwanza ningelaani tukio lile. Ningempa pole Tundu Lissu. Na ningeweka msisitizo kwamba sijakusikia.

..Kumtusi muandishi wa habari ni kukosa busara. Na kwa kukumbushia kuwa Mwalimu aliwahi kumjibu vibaya muandishi wa habari, ni kweli, lakini sote tunajua kuwa alikosea.
Mwalimu aliulizwa kuwa kuna hisia kuwa yeye Mwalimu alihusika katika njama za kutaka kumpindua Moi. Nyerere alimtaka mwandishi atumie akili zake kwa sababu Nyerere hakuwa na ugomvi na Moi wala Kenya. Nyerere aliona kama mwandishi hakufanya bidii ya kumwelewa Nyerere anasimamia nini katika siasa kabla ya kumwuliza swali hilo.
 
‘wengi tulitarajia ataulizwa…..’

Basi amefanya sahihi kutoa hilo jibu maana mpaka hapa ni dhahiri huyo muandishi alitumwa na nyie wengi.

Unaelewa tafsiri ya kuamuru?


Hiyo ya pikipiki kubeba magendo mipakani wote tumemsikia vizuri na kuwasoma watoa taarifa humu ndani, hakuna amri kwenye yale matamshi ila maelekezo na suggestions za kumaliza migogoro huku pande zote zikipata stahiki zao.

..basi kulikuwa na FURSA kwa Makonda kutoa "maelekezo" na " suggestions" kwa Igp/Polisi kuhusu tukio la kushambuliwa Tundu Lissu ktk eneo la makazi ya viongozi wa serikali na bunge.
 
..Lissu amewataja Magufuli, Kipilimba, na Makonda.

..Katika hao watatu nadhani Makonda is the odd one.

..Wanaopaswa kuchunguza, kukamata, na kushtaki, no jeshi la Polisi na Dpp.

..Serikali itoe taarifa kwanini waliomshambulia Lissu hawajakamatwa mpaka leo hii?


Unadhani Makonda is the odd one, kwanini?

Hilo jeshi la polisi limemuita mara ngapi huyo muhanga kutoa ushirikiano ili kukamilisha hizo tuhuma?

Wanatoaje taarifa juu ya washambuliaji kukamatwa bila kuthibitisha kwanza washambuliaji ni akina nani?
 
..basi kulikuwa na FURSA kwa Makonda kutoa "maelekezo" na " suggestions" kwa Igp/Polisi kuhusu tukio la kushambuliwa Tundu Lissu ktk eneo la makazi ya viongozi wa serikali na bunge.


Ni wazi Makonda ameamua kutokutumia hiyo FURSA.

Ameamua kutumia njia ambayo kwake anaamini ni sahihi, sioni kosa lake.
 
Mwalimu aliulizwa kuwa kuna hisia kuwa yeye Mwalimu alihusika katika njama za kutaka kumpindua Moi. Nyerere alimtaka mwandishi atumie akili zake kwa sababu Nyerere hakuwa na ugomvi na Moi wala Kenya. Nyerere aliona kama mwandishi hakufanya bidii ya kumwelewa Nyerere anasimamia nini katika siasa kabla ya kumwuliza swali hilo.

..kuna tukio lingine la Mwalimu Nyerere kumjibu vibaya mwandishi wa Kenya aliyemuuliza kuhusu kumuunga mkono mmoja wa watia nia wa Uraisi kupitia Ccm mwaka 1995.

..Mwalimu alimjibu vibaya muandishi wa habari, sasa tujiulize kama tuhuma za muandishi zilikuwa za kweli au uongo. Je, Mwalimu alikuwa na mgombea au hakuwa na mgombea?

..Hili suala uliangalie zaidi KISAIKOLOJIA na jinsi watu wanavyosema ukweli au uongo.
 
Unadhani Makonda is the odd one, kwanini?

Hilo jeshi la polisi limemuita mara ngapi huyo muhanga kutoa ushirikiano ili kukamilisha hizo tuhuma?

Wanatoaje taarifa juu ya washambuliaji kukamatwa bila kuthibitisha kwanza washambuliaji ni akina nani?
usiwe chizi, kama Lisu na dereva wake wangekufa ina maana kungekuwa hakuna kesi ndivyo jinai inavyoenndeshwa nchini kwenu
 
Siku hizi Kila mtu ni mwandishi ndiyo maana habari nyingi za sikuhizi lazima utumie akili nyingi kuelewa! Mwandishi aliyena akili timamu huwezi uliza swali la kihuni kama Hilo ndiyo maana makonda kamjibu kihuni ! Mwandishi pole sana maswali hayo muulize lisu yeye ndiye anayejuwa waliompiga risasi huyo atakujibu vizuri na umuulize nini kilichopelekea kutoenda kuandikwa maelezo juu ya tukio polisi yeye atakwambia na mambo mengine kadhaa utayapata huko kwa mapolisi.

We nawe kichwa maji,Lisu alishasema Makonda alihusika yeye kupigwa risasi,sasa mwandishi alimtaka Makonda athibitishe au akanushe uhusika wake kupigwa risasi TL.mwandishi ana kosa gani hapo?Ukiangalia kwa kwa makini hilo jibu alilotoa Makonda linaonyesha kuna kitu alifanya!upo hapo?
 
Unadhani Makonda is the odd one, kwanini?

Hilo jeshi la polisi limemuita mara ngapi huyo muhanga kutoa ushirikiano ili kukamilisha hizo tuhuma?

Wanatoaje taarifa juu ya washambuliaji kukamatwa bila kuthibitisha kwanza washambuliaji ni akina nani?

..Makonda is the odd one kwasababu kwa tukio kama lile chain of command inakuwa nimekwenda nje kidogo.

..Mwanzoni Polisi walikuwa wanadai wameshindwa kuchunguza kwasababu Lissu amekimbia nchini.

..Madai hayo yamethibitika kuwa ni uongo. Lissu amekuwepo nchini. Na amefika mara kadhaa ktk vituo vya Polisi. Juzi tu Lissu aliitwa Polisi kuandika maelezo kuhusu mkutano alioufanya maeneo ya Loliondo.
 
Kuna baadhi ya majibu huwezi kushangaa mtu kujibiwa maana ameuliza swali la kipuuzi
wewe kwa akili zako unaona ni swali la kipuuzi? hoja hapa makonda na hasa wanasiasa wakishindwa au ukiwabana sawasawa wanaruka kama alivyoruka makonda.
mfano mwengine Pasco alimuuliza Magufuri swali badala ya kujibu Magufuri akasema mbele ya waandishi kuwa "mayala kwa kiruga chao ni njaa"
cc pasco
 
..Makonda is the odd one kwasababu kwa tukio kama lile chain of command inakuwa nimekwenda nje kidogo.

..Mwanzoni Polisi walikuwa wanadai wameshindwa kuchunguza kwasababu Lissu amekimbia nchini.

..Madai hayo yamethibitika kuwa ni uongo. Lissu amekuwepo nchini. Na amefika mara kadhaa ktk vituo vya Polisi. Juzi tu Lissu aliitwa Polisi kuandika maelezo kuhusu mkutano alioufanya maeneo ya Loliondo.


Bado sijaridhika na hiyo sababu yako ya kumfanya Makonda “the odd one” vinginevyo tuseme ni easy target to accuse?

Sio mwanzoni tu, hata kipindi cha uchaguzi 2020 wakati wa kampeni ameitwa mara ngapi na hakwenda badala yake akamjibu IGP wa wakati huo kupitia mikutano yake ya kisiasa majukwaani?

Kuwepo kwa Lissu nchini ni sahihi lakini katika uwepo wake aliitikia wito wa dhahama yake mara ngapi?

Ulitaka alipoenda kuandika maelezo Loliondo wamlazimishe kuitikia wito wa tuhuma zake juu ya dhahama dhidi yake?
 
Bado sijaridhika na hiyo sababu yako ya kumfanya Makonda “the odd one” vinginevyo tuseme ni easy target to accuse?

Sio mwanzoni tu, hata kipindi cha uchaguzi 2020 wakati wa kampeni ameitwa mara ngapi na hakwenda badala yake akamjibu IGP wa wakati huo kupitia mikutano yake ya kisiasa majukwaani?

Kuwepo kwa Lissu nchini ni sahihi lakini katika uwepo wake aliitikia wito wa dhahama yake mara ngapi?

Ulitaka alipoenda kuandika maelezo Loliondo wamlazimishe kuitikia wito wa tuhuma zake juu ya dhahama dhidi yake?

..Lissu angestahili lawama kama jeshi la Polisi lingemuita kutoa maelezo kuhusu tukio lake halafu akakataa.

..Kinachotokea sasa ni aibu kwa jeshi la Polisi. Kwamba wameweza kumhoji Lissu kuhusu mkutano wa Loliondo lakini wameshindwa kumhoji kuhusu shambulizi alilofanyiwa.

..Na kuna kipindi tulishuhudia Lissu akifika kituo kikuu cha Polisi Dodoma. Na alifika hapo baada ya mawasiliano na miadi na makamanda wa Polisi wa Dodoma.

..Binafsi sijashawishika na maelezo na mwenendo wa jeshi la Polisi kuhusiana na jaribio la kumuua Lissu.
 
Back
Top Bottom