Pre GE2025 Paul Makonda: Gambo usitake umaarufu wa kijinga, uwe unahudhuria vikao vya maendeleo Mkoa wa Arusha

Pre GE2025 Paul Makonda: Gambo usitake umaarufu wa kijinga, uwe unahudhuria vikao vya maendeleo Mkoa wa Arusha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tatizo la makonda ni kujiona yupo juu ya kila mtu, mkuu wa mkoa huwezi kuongea na waziri unampiga piga bega kama hawara yako huo ni utovu wa nidhamu mkubwa sana na ni dharau kabisa, nayote hiyo inatokana na kujiona yuko juu na ana nguvu pamoja na kwamba cheo chake ni cha chini.
Nidhamu ni kutumikia wananchi mambo mengine Waafrica tunapenda kujitukuza tu!
Waziri ni mtumishi wa wananchi kama ni nidhamu anayestahili kupewa ni mwananchi!
Wewe ndo wale mkipata cheo mnataka kuabudiwa badala ya kutumikia wananchi!
Huyo Waziri ni nani mpaka umuone anastahili kuheshimiwa sana kana kwamba ukiwa Waziri basi sio mwanadamu wa kawaida!
Taifa hili linatakiwa liwaheshimu sana wananchi sio kuabudu viongozi!
 
Nidhamu ni kutumikia wananchi mambo mengine Waafrica tunapenda kujitukuza tu!
Waziri ni mtumishi wa wananchi kama ni nidhamu anayestahili kupewa ni mwananchi!
Wewe ndo wale mkipata cheo mnataka kuabudiwa badala ya kutumikia wananchi!
Huyo Waziri ni nani mpaka umuone anastahili kuheshimiwa sana kana kwamba ukiwa Waziri basi sio mwanadamu wa kawaida!
Taifa hili linatakiwa liwaheshimu sana wananchi sio kuabudu viongozi!
Mbona mkuu wa mkoa mwenyewe anapenda kuheshimiwa tena sio kuheshimiwa tu anapenda kuabudiwa na kunyenyekewa, mtu anaye tafuta sifa huwa yupo hivyo , kama ingekuwa kweli wananchi kwanza madaraka nyuma basi msingekuwa mnawateka wanao wakosoa na kuikosoa mambo yake ya hovyo, mbona mnateka na kuuwa hao wananchi wakiyasema mabaya yenu kama kweli mnawatumikia wao?wapeni full power basi ili tujue kweli mnawatumikia kikamilifu, siyo kutafuta kukubalika kwa kuwachafua viongozi wenzio ukowa nyuma ya mtutu wa bunduki, Acha unafiki?
 
Mbona mkuu wa mkoa mwenyewe anapenda kuheshimiwa tena sio kuheshimiwa tu anapenda kuabudiwa na kunyenyekewa, mtu anaye tafuta sifa huwa yupo hivyo , kama ingekuwa kweli wananchi kwanza madaraka nyuma basi msingekuwa mnawateka wanao wakosoa na kuikosoa mambo yake ya hovyo, mbona mnateka na kuuwa hao wananchi wakiyasema mabaya yenu kama kweli mnawatumikia wao?wapeni full power basi ili tujue kweli mnawatumikia kikamilifu, siyo kutafuta kukubalika kwa kuwachafua viongozi wenzio ukowa nyuma ya mtutu wa bunduki, Acha unafiki?
Unaushahidi au unaongea tu kwa mihemko!
Hao waliotekwa ni nani kawateka na kwa ajili ya nini mimi sijui!
Ila nakwambia tu mara nyingi watu kama nyinyi ndo mnasumbua sana mkipata nafasi.
Mzizi wa Mamlaka na uongozi ni watu na hao watu au wananchi ndo wanapenda kutumikiwa na kuheshimiwa!
Kwa hiyo kiongozi kushikwa bega na kiongozi wa umri na cheo karbia sawa ni urafiki na linaonesha bond kati ya viongozi,Hata Biden anapenda sana kushika mikono na mabega ya viongozi wenzake alkadharika Trump.
 
Kwa nini anaongea huku anamshika shika bega waziri kama mtu mdogo kwake?!
Huyu mkuu wa mkoa protocol hazijui au waziri hajui protocol
Kushikana shikari mabega ni kama anampa maelekezo waziri
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda akiambatana na Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha Lami ya Mianzini-Olemringaringa amemtaka Mbunge wa Arusha Mjini Mhe. Mrisho Gambo kuwa anahudhuria vikao mbalimbali vya maendeleo ndani ya Mkoa wa Arusha, badala ya kuwasubiri Viongozi wa Kitaifa na kuzungumzia kero mbalimbali ndani ya Jimbo lake.

Mhe. Makonda ameeleza kuwa kufanya hivyo ni kutafuta huruma ya wananchi kinyume cha taratibu, akiziita kuwa ni siasa zisizokuwa za maendeleo kwa wananchi, akiagiza kuwa ni muhimu kwa Viongozi wateule na wa kuchaguliwa kushiriki vikao vya kupanga na kuamua kuhusu maendeleo ya Mkoa wa Arusha.

Kauli ya Mhe. Makonda inafuatia maombi ya Mhe. Gambo aliyeomba kwa Waziri wa Ujenzi kujengewa barabara ya Kilombero pamoja na ufungaji wa taa kwenye barabara mbalimbali za Jiji la Arusha, masuala ambayo kulingana na Mhe. Makonda yalishajadiliwa na maamuzi kutolewa kwenye vikao mbalimbali vilivyofanyika chini ya Maagizo ya Mawaziri mbalimbali wa Kisekta ikiwemo Kikao cha mapema leo asubuhi kilichohudhuriwa na Waziri wa ujenzi Mhe. Abdallah Ulega na Waziri wa fedha Mhe. Mwigulu Nchemba.
Makonda hakumtendea haki Gambo.Mbunge hata kama analijua jambo linalohusu maendeleo ya jimbo lake,bado anatakiwa aliongee au aliulizie hadharani ili wapiga kura wake nao wapate taarifa ya kinachoendelea.
 
Huwezi kutumia maneno makali kwa kiongozi mwenzio mbele ya vyombo vya habari.
Napendekeza mheshimiwa Rais Samia, huyu RC Makonda atenguliwe.
Naaam.
 
Huwezi kutumia maneno makali kwa kiongozi mwenzio mbele ya vyombo vya habari.
Napendekeza mheshimiwa Rais Samia, huyu RC Makonda atenguliwe.
Naaam.
Hayo mawazo ni ya watu wajinga tu wasiopenda uwajibikaji!
Hata Zito Kabwe japo ni mpinzani bado hajaunga mkono hoja za Mrisho Gambo kujitetea!
Kwa kifupi Gambo ana sifa za kijinga!
 
Mbona yeye ni mpenda kuongea public katika mambo mengi?

Anajisahaurisha kuwa huwa anaitisha mikutano ya hadhara na kuanza kuhoji watendaji juu ya mambo ambayo tayari yapo serikalini?

Huyu Makonda lazima ana matatizi ya kiakili Leo hii kageuka ghafla kuwa muumini wa vikao? Hataki tena habari za mambo hadharani?

DAB ni tatizo. japo Gambo naye ni walewale tu. shoe wine!

YESU NI BWANA&MWOKOZI
 
Pamoja na Yote bado RC makonda amezingua sana Kumdharirisha Gambo mbele Ya kandamnasi tena Kiongozi aliyechaguliwa na Wananchi hio haijakaa Poa, Kesho Gambo akiwa Boss wake?

Makonda ajifunze Kuheshimu Viongozi wenzie mana hata Chongolo aliwahi Kumkolomea wakati ni RC Dar baadae tuliona Chongolo anakuja kuwa Boss wake hii haijakaa Poa ivo Viti vya Kuteuliwa una Serve at the wish ya aliyekuchagua Tusijione sana tumefika
Anakuja kuwa Boss wake ? Chongolo alikimbia mapema kabisa
 
Back
Top Bottom