Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Na huo ndio ukweli tunaziita siasa matokeo siasa za kizazi kipya.
 
..kama Makonda hana mamlaka na bajeti basi anachofanya ni kupiga makelele ya kulaghai wananchi.
Hasa nilizungumzia siasa akiwa kama mwenezi. Lakini hata kama mkuu wa mkoa, siasa zake zinawaamsha watendaji kwa kiasi fulani. Ni aina ya siasa zinaeleweka kwa wananchi. Siasa za kutaka kumpendeza kila mtu na "Kistaarabu" kama za kina Nchimbi na Makalla zimepitwa na wakati.
 
Hata Mimi Mtoto wa Shule namuelews sana Komredi Makonda.
 
Siasa za kushambulia wanaotajwa wezi hata kama sio wezi. Siasa chafu kuua wasio na hatia...
 
 
Tayari ushamkubali sasa
 
Makonda siyo mwanasiasa na Makonda hafanyi siasa (labda kama hujui ni nini maana ya siasa). Makonda anafanya maigizo, ulaghai, kujipendekeza yaani kama umeshawahi kuingia circus ukaona wale ma clown, basi ndiyo mapigo ya Makonda. Ila lazima nikiri kuwa anafanikiwa kuwachota wajinga wajinga wengi sana na kuwaaminisha kuwa yeye ni kiongozi mzuri.
 
Ni ngumu mkuu wa mkoa wowote kuleta mabadiliko sababu hana mamlaka juu ya bajeti, haajiri wala hawezi kufukuza.
Kwa hiyo Makonda ana uhalali wa kufanya anayoyafanya kama hana power ya kubadilisha chochote?...
 
Shida ya wa Tz wengi ni vichwa ngumu, hapo watakuambia wale watu/wananchi/kinababa Kabwela waliokua wanaojazana katika mikutano yake wamepangwa waende.

Chukua huu mfano kujua vichwa vibovu: watu walewale waliopinga kipindi serikali inakomaa kujenga bwawa la Nyerere kwa visingizio visivyo na mantiki leo utakutana nao uku jukwaani wakifurahia na kusifu kuwepo kwa ilo bwawa. Hii ni kwasababu Mihemko, mapenzi ya vyama pasipo ku judge mambo kihalisia vimewatala. Kwasasa watu ukaa kwemye vyama vya siasa sawa na watu wafia dini, ata uende ku prove mbele yake theory fulani ye atakomaa ma msimamo wa dini yake inasemaje.
 
Swali fikirishi je serikali za Africa hujipanga kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja? Usisahau matumizi ya akili mnembo
 
matumaini na matarajio ya suluhu ya changamoto na matatizo binafsi na ya jumla kwa watu wa Arusha yameamshwa upya na kwakweli ni makubwa mno....

Leo watu wa Arusha wamepata ahueni ya mwanzo, iliyoamsha furaha, matumaini yaliyopotea kwa waliokata tamaa.....

clinic ya haki ni matumaini ya wana Arusha chini ya comrade RC.Paul Makonda...

Mwenyezi Mungu aambatane na kuandamana nawe daima, kiongozi wa mkoa wa Arusha....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…