Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Unalinganishaje watu wanaofanya mambo/shughuli/kazi tofauti?Jipime kama viatu vyako ni ndula,raba mtoni,moccasins au la kuchumpa.
 
Huu uzi uwe wa kuwaumbua kwa ushahidi usio na mashaka wale wote wanaomtupia mawe Paul Makonda aliyejipambanua kama mtetezi wa wananchi wanyonge na pia kumpa maua yake, hivyo

Kama umewahi kutatuliwa shida yako ngumu na Paul Makonda weka ushuhuda hapa, tuelezee.

Kama kuna ndugu yako, jamaa au rafiki unayemjua binafsi aliyewahi kutatuliwa shida yake ngumu na Paul Makonda weka ushuhuda hapa, tuelezee.

Kama kuna changamoto/kero muhimu ya mtaani kwako iliyowahi kutatuliwa na Paul Makonda weka ushuhuda hapa, tuelezee.

Hembu tuwaonyeshe kwa ushahidi na ushuhuda thabiti wabaya wake kwamba anayofanya kiongozi huyu sio maigizo, hadaa, hearsay na kutafuta kiki tu bali ameacha alama za kweli za historia zisizofutika kwa watu halisi.
 
Makonda anakosa balance kwenye utendaji wake, mara nyingi nikimtazama ni kiongozi ambaye ameweka mbele maslahi ya wananchi (sio kosa) huku akiwakandamiza watendaji wenzake wa serikali hasa kwa matumizi mabaya ya lugha dhidi yao, ana egoism mbaya sana isiyofaa kwa kiongozi wa umma.

Anatakiwa ajue hata hao watendaji anaowatolea lugha za maudhi nae pia ni kama mlezi wao, ajifunze kupungumza mihemko anaposikiliza kero za jamii na anapozitafutia suluhisho, simply put, ajue kuchagua maneno ya kuongea mbele ya hadhira ili asiishie kutengeneza maadui ndani ya serikali anayoifanyia kazi.
 
Wewe binafsi, jamaa au ndugu yako kuna hata jema mmoja kutoka uongozi wake ambalo mmewahi kuguswa nalo moja kwa moja?
 
Watendaji ndo mitambo ya wizi wa fedha za umma. Ngoja wapigwe spana
 
Haisaidii kitu. Makonda hataweza kutatua kero za wakazi wa Arusha kwa approach yake hiyo. Ata'burn out' kwa sababu matatizo ni mengi mno kutatuliwa na mtu mmoja. Yeye, kwa maoni yangu, si mbadala ya vyombo vilivyopo vya utatuzi wa migogoro. Kwa sasa watu wengi wanahudhuria mikutano yake ndiyo, na ni wangapi wanaondoka pale matatizo yao yakiwa yametatuliwa?

Kitu ambacho angekifanya ni kuimarisha vyombo vilivyopo vya utatuzi wa migogoro ya wananchi - kujua their strengths na weaknesses, then to build on their strengths and hapo ndipo kungekuwa na utatuzi wa kudumu wa migogoro. Lakini kwa approach yake ana'solve' tatizo kwa ku'create' tatizo lingine. Wapi na wapi? Hataweza kufanikiwa kwa approach yake. Kama Dar hakufanikiwa, hata huko hatafanikiwa as long as anaendelea kutumia the same approach.
 
Anatusaidia sana kujua ujinga wa CCM na watendaji wake wa Serikali, anayoyaanika hata kama yeye hawezi kuyafanyia kazi mamlaka za juu RAIS, VP, PM nk wanasikia wanapaswa kuact na kuleta suluhu ya matatizo.

Taifa hili limeoza kila mahala na maRC wote + maDC+maDED+maRAS wangekuwa active na wanafikika na kupambana kama Makonda nchi nzima angalau tungeweza kuyajua matatizo ya kila mahala.
 
Mkuu unalo sahau ni kuwa hata shetani husaidia watu, wema wa mtu hujidhihirisha wenyewe bila matangazo.

"Ama kweli chema chajiuza, kibaya chajitembeza".
 
 
Wewe binafsi hujawahi kuguswa na jema lake moja kwa moja?
Mkuu unataka kusema wakuu wa mkoa wengine na watendaji mbali mbali wa serikali hawawasaidi wananchi kutatua kero zao katika maeneo yao ya kazi isipokuwa Makonda pekee yake tu???
 
Simfananishi Lisu na Makonda ila ukweli kila mtu anajua Makonda ni RC wa Arusha, hivi hata RC wa Mkoa wangu namjua kwa sura na sio jina na mienendo yake kama ilivyo kwa Arusha. Unaweza sema Tanzania kuna Mkuu wa Mkoa mmoja tu,
Kweli kabisa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…