Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Tatizo hamumjui Makonda. Tulieni kwanza.
Kwani ni mara yake ya kwanza kwa kutoa kauli zenye utata?
1. Ninawafahamu na nitawataja viongozi wote wanao uza madawa ya kulevya!!

2. Ni marufuku kwa wabunge wote kuja Dar wakati vikao vya bunge vinaendelea huko Dodoma!!

3. Ni lazima kwa Wanaume wote wa Dar wakapimwe tezi dume!!
 
Umeanza ujinga wako?

😅😅😅Ujingwa upi na wewe!!! Mmepoa kama piritoni.. chadrama futi sita bado hautaki kujiokoa.. pokea 💉💉💉

Acha nianze kuburudika na haya...
Nakanyaga nakwenda.. 2025 huyooo.. na bado.. Tuombeane uzima tuwemo humu kama kawaida.

Makonda oyeee...
Kazi iendeleee
 
Makonda anatisha sana nadhani kwa sasa ndo mtu anayetajwa sana duh jamaa riziki yake ndefu sana
 
Makonda mara zote ni mtu mwenye mawazo finyu.
wa vyovyote Makonda ni mtu wa kitengo aliyevamia siasa.

Ni mtu atakumbukwa kumfanyia vurugu Waziri Mkuu na Makamu wa Rais mstaafu Joseph Sinde Warioba.

Alipokuwa RC Dar, atakumbukwa kwa kupora magari na viwanja vya wafanya biashara kwa kutumia jina la Rais Magufuli.
Aliingia figisu za watu na wanasiasa kubambikwa kesi za madawa ya kulevya.
Hatujasahau uhusika wake kutekwa kwa Mohammed Dewji, Mo.

Suala la kushambuliwa Tundu Lissu, kuna uhusika wa Makinda usiowekwa wazi.

Sasa tuseme tu, je Makonda pamoja na hisia za uchafu ndiye msemaji wa Taasisi ya Uraisi, au ametumwa kunena kuwa kuna watu wanamchafua Rais Samia.?

Kwa vyovyote Makonda anajikweza zaidi ya uwezo wake kisiasa.

Kutoa mawazo mbadala, kwa jambo lolote lile, si kumchafua mtu.

Ni tahadhari tu, kuwa kwa kumtumia Makonda Rais anachafuka zaidi.
 
Should we we wait to hear another leakage of recorded voices? Or even short videos?
that may be the story of next time 🐒

but for now,
there is a very strong coded message behind a very able RC statement, as I have posed them in style of questions before 🐒
 
Ni kweli unampenda Sana Makonda, na hii huwa inatokea mtu fulani kumpenda mtu fulani automatic, inatokana na ku share spiritual rim, njozi na maono ya pamoja.

Ni kweli Makonda kwako ni kijana mtiifu na mnyenyekevu amekuwa hivyo tangu akiwa Mkuu wa Mkoa, alipotoka, alipokuwa mwenezi na sasa Mkuu wa Mkoa Arusha
Kwako binafsi hakuna baya lolote alilofanya na sababu unampenda hata akifanya kosa kwako huwa ni kosa dogo la utoto ambapo unaamini atajirekebisha

Madhara ya tabia za Makonda na consistence ya tabia hizo

1. Hulka ya kupenda ukuu, cheo na sifa:

a) ilianza kuonekana alipokuwa Mkuu wa Mkoa alijilinganisha na mawaziri na kuonekana mawaziri hawana lolote dhidi yake Mkuu wa Mkoa, kuna wakati alikua na msafara mkubwa kuliko waziri Mkuu na Makamu wa Rais.

Hulka hio ameendelea nayo alipokuwa mwenezi, alimdharau RC Chalamila mbele ya Kadamnasi, akamwagiza Waziri Mkuu Majaliwa kama yeye ndio Mkuu wa Chama, akifanya hivyo kwa mawaziri na ikapelekea baadhi yao kutokubaliana nae yupo Bashe ambaye alitoka hadharani kuonesha kutokukubaliana na maagizo ya Makonda swali je Cheo Cha katibu Mwenezi ni Command kwa Waziri Mkuu na Mawaziri .. Hilo nakuachia wewe Kadinali Pengo ujibu.

B. Akajipa msafara wa magari na kuwa yeye ndiye mtu anayewindwa Sana auwawe mara afanye ziara mkoani alale Dar kwa Maaskofu.

C. Akagoma kufuata maelekezo ya Katibu Mkuu Comred Nchimbi, Kadinali wewe unajua Askofu Mkuu wa Jimbo ndiyo mkuu wako wa kazi kama wewe ni padri au askofu msaidizi sharti ufuate maelekezo yake, kazi yako inakuwa kupeleka ushauri na mapendekezo na kuomba kibali cha utekelezaji. Makonda hakutaka kufuata uratibu wa kawaida kuwa ndani ya Chama Yuko chini ya Katibu Mkuu, Bali yeye alitaka ndio asikulizwe na aongoze, kwa kuwa hakuwa cooperative hii kitu imekisumbua Sana Chama ndipo Rais kaona isiwe tabu ampe ukuu wa Mkoa kwa sababu ni dhahili anagombana na kila mtu ndani ya Chama.

d. Imetokea tena alipofika Arusha, kujikusanyia Msafara wa Magari, Gari yake ya RC tena yenye bendera kupakia watoto wake (watu wa protocol wanaelewa zaidi je bendera na plate namba yenye cheo fulani inaweza kutumika ndivyo sivyo..?)

haya Leo tena kutuhumu mawaziri kuwa wanamtukana Rais hili jambo limefedhehesha Baraza la mawaziri, nchi na vyombo kwa ujumla, je ni kuwajulisha mawaziri kuwa hawezi kuwatii sababu kimsingi mkuu wa mkoa si mkubwa kwa Waziri ndio mana yuko chini ya Tamisemi. Kwan kauli hio Makonda kajitwalia uwaziri Mkuu wake na kuonesha baadhi ya mawaziri hawana hadhi ya kumtuma kwa kile tuu yeye anawaona wanamtusi Rais wa JMT

Hii tabia yake ya Ufitini, uchonganishi, kupenda madaraka, uzushi na uongo bado kwako Kadinali unaonaje ni makosa madogo....?
Vipi kwa Baraza la mawaziri wanaichukuliaje na wanamchukuliaje kijana wako kipenzi?

Viongozi wanaishi kwa kuheshimiana hata kama hawajakubaliana, mfano Kinana na Nchimbi, wapo washindanu January na Mwigulu wote hao si kitu kimoja lakini wanaishi kwa kuheshimiana bila kuvuka mipaka

Uungwana ni kitendo
Kama Kadinali utamwacha Makonda na tabia hizi lambda kwako ndio sifa za uongozi, Sisi tunasema Yetu Macho
kijana anafanya kazi nzuri, asifitinishwe na wazee wastaafu 🐒
 
Tarehe 13 mwezi uliopita, Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Dr. Samia Suluhu Hassan alitoa msimamo wake kama mkuu wa nchi na wa CCM kuhusu 'makundi' na 'watoto' wake kisiasa.

Katika hafla ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua, Rais Samia alisema kwa umakini, umadhubuti na wazi kabisa kuwa yeye hana makundi wala watoto ndani ya chama chake na Serikali.

Rais Samia akaenda mbele na 'kuwakemea' wote wanaojitanabaisha kuwa ni watoto wa Mama au wa kundi la Mama. Alihitimisha kuwa viongozi wote kwa ujumla wao ni watoto wake.

Jana, kwenye Maadhimisho ya Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine, RC Makonda amesikika akijitanabaisha kuwa yeye ni mtoto wa Rais Samia. Amesikika mara mbili akisema 'Mama yangu' kwenye kauli zake, tena mbele ya Rais Samia.

Kwanini Makonda atofautiane na kukinzana na msimamo wa Rais Samia kwa kujitaja kama 'mtoto wa Mama Samia'? Makonda alilenga au analenga nini?
 
Back
Top Bottom