Paul Makonda: Wananchi walioikimbia Dar warudi, Mauti hauikimbii. Siku ya Jumapili, kila mtu afanye fujo awezavyo na kupiga kelele na vigeregere!

Paul Makonda: Wananchi walioikimbia Dar warudi, Mauti hauikimbii. Siku ya Jumapili, kila mtu afanye fujo awezavyo na kupiga kelele na vigeregere!

Kwa hiyo unataka serikali iwe inazurura mabarabarani kama wehu na kusema tukupime ? Huo ni wehu. Wewe ni daktari au muuguzi unatafuta posho za kuzurura kupima?

Kinachotakiwa elimu na imetolewa kuwa ukiona dalili hizi wahi hospitali inatosha,mtu akiona dalili za corona aende hospitali au apige namba husika wenyewe waje kumbeba
U seems kukwepa my point. Sizungumzii kupima kwa style yako ambayo ni ya kijinga.

Nazungumzia kupima kwa vituo. Yaan check points kama mipakan hiv. Unakuwa na team ya madkatari wako.stationed kupima kila anae ingia na kutoka. Nazungumzia checkpoint za mikoa.. kupima kila anae ingia na kutoka.

Trust me kama kunawa uso na barakoa vingekuwa vinasaidia sana..sana sana.. leo hii nadhani ulaya na baadhi ya mataifa ya afrika yangeongoza kwa kutokomeza huu ugonjwa mapema sana..maana walienda mbali zaid.. wakatunga na sheria kabisa na kupuliza madawa.

+ mbinu unazozungumzia ni individual strategy. We need national strategy. Na hapa sizungumzii lockdown.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku ya jumapili itakuwa siku ya send off party ya kuiaga corona Tanzania na kuifungisha virago forever iende kwa mumewe shetani...
Fanyeni nyie hio send off. Mimi sidanganyiki. Tuliishaambiwa akili za kuambiwa changanya na za kwako. Mimi nikiona tu ametoka mafichoni basi hapo ndo naweza kuanza kufikiria send off.
 
Nazungumzia checkpoint za mikoa.. kupima kila anae ingia na kutoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
Cheki points zipo kibao hadi kwenye maofisi mengi tu, mabenki ,hata vyoo hata vyoo vya watu wengi kabla kuingia unachekiwa zipo kibao ila sio serikali inapima ni wahusika kwa gharama zao na wana vipimo vyao ukitaka hata nyumbani kwako jiwekee

Ukitaka nunua likipimo lako kila anayeingia nyumbani mwako hata akivaa barakoa mpime serikali haijakuzua.Hata leo jianzie checkpoint yako hata kwenye gari yako au bajaj yako ukitaka, mtu kabla ya kuingia kwenye gari yako au bajaj yako mpime!!!
 
Daresalaam kumenoga
IMG-20200520-WA0002.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
cheki points zipo kibao hadi kwenye maofisi mengi tu, mabenki ,hata vyoo hata vyoo vya watu wengi kabla kuingia unachekiwa zipo kibao ila sio serikali inapima ni wahusika kwa gharama zao na wana vipimo vyao ukitaka hata nyumbani kwako jiwekee

Ukitaka nunua likipimo lako kila anayeingia nyumbani mwako hata akivaa barakoa mpime serikali haijakuzua.Hata leo jianzie checkpoint yako hata kwenye gari yako au bajaj yako ukitaka, mtu kabla ya kuingia kwenye gari yako au bajaj yako mpime!!!
Hizo chekpoints mnaongelea hivi vipima joto?
Nyie hamnazo aise!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiutani utani tu mpaka tutashinda hii vita, kama Mr Bean anavyoibukaga mshindi bila kutumia msuli...sometimes yeye hushangaa tu na mara anajikuta tatizo limeisha.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda amesema watu wote walioikimbia Dar Es Salaam na kurudi mikoani Kwa hofu ya ugonjwa wa COVID19 (Corona) na kuwaacha watu wa Dar es salaam wakiendelaea kupiga kazi warejee jijini humo.

Aidha amesema shughuli zote za uchumi zifunguliwe na ziendelee kama zamani.Kutokana na kutanda kwa hofu ya ugonjwa wa COVID19 baadhi ya shughuli nyingi za uchumi kama biashara za bar, hotel na maduka zilifungwa na watu wengi kurejea mikoani kutokana na hofu hiyo.

Pia amesema siku ya jumapili ya tarehe 24/5/2020 itakuwa siku maalum ya kujipongeza Kwa kuishinda hofu,na kuwataka watu wa Dar es salaam kupiga kelele vyovyote wawezavyo."Kama una mziki mkubwa nyumbani kwako fungulia Kwa nguvu.Upo barabarani piga honi Kwa nguvu.Kwa kuwa tumeishinda hofu.Na mliotuacha Dar es salaam tuko salama na tunaendelea kupiga kazi."
 
Back
Top Bottom