PAYE kwa Wafanyakazi imepunguzwa kutoka 9% hadi 8%. Kodi kwenye marupurupu imeondolewa; hatua hii itaongeza mshahara!

PAYE kwa Wafanyakazi imepunguzwa kutoka 9% hadi 8%. Kodi kwenye marupurupu imeondolewa; hatua hii itaongeza mshahara!

Nampongeza mama Samia, anayo dhamira ya kweli ya kuipigania maslahi ya wafanyakazi...madaraja na vyeo ni hatua nzuri kwa wafanyakazi
 
Malimbikizo ya Mishahara yanalipwa mwezi huu wa tano, pia ni jambo la kushukuru, lkn pia 1% imepunguzwa.
Ahsante mama.
 
Mama yuko vizuri kumkichwa. Hajataka kupelekeshwa na hisia na kutaka cheap popularity eti aongeze tu mishahara ili ionekane "mwendazake" alikuwa na roho mbaya kutoongeza mishahara.

Turudie kusema ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi siyo suala la kufa na kupona katika nchi yenye mahitaji lukuki tena ya msingi kama nchi yetu. Wafanyakazi hawatakufa kwa kutoongezewa mishahara, na pia ieleweke kuongeza mishahara maana yake ni kuwakamua zaidi walipa kodi. Mi ni muumini wa nchi kuongozwa rational, na ni irrational kuongeza mishahara from nowhere wakati kuna maelfu ya wadogo zetu hawana ajira mtaani, na wakati huo tunapambana kodi zetu zibebeke.

Na mama ametoa maamuzi rational. Hongera sana mama.
Nyie ndo mnalalamika mkienda kwenye Taasisi za serikali mkapewa huduma mbovu haya Mambo ya kuwalipa vizuri watumishi yanaleta motisha katika kazi mtu anakua na bidii kwa sababu kazi anayofanya inamfanya aishi maisha mazuri kwa kupewa stahiki zake kwa wakati.kuja na hoja eti Kuna watu Hawa ajira uko mtaani ndo iwe sababu ya kutowaongezea mishahara watumishi ni ufinyu wa upeo katika kufikiri. Kwa sababu serikali inaajiri kwa kufuata majirani na imishaajiri inajukumu la kuboresha mishahara na mazingira ya kazi kwa mtumishi wake
 
Malimbikizo ya Mishahara yanalipwa mwezi huu wa tano, pia ni jambo la kushukuru, lkn pia 1% imepunguzwa.
Ahsante mama.
Ignorance and brainwashed addiction drive the crooks into the lioness din in which the flesh is devoured without expectations.
 
Marupurupu hayakua na kodi miaka mingi tu.

Marupurupu kama hela ya nyumba, chakula, nauli, safari nk hayakua na kodi.

Hiyo ya 8% ni ya watu wa kima cha chini cha laki 270,000.

Tunataka kodi ipungue kwa ambao mishahara wa digiti 7.

Kikubwa zaidi kodi ya ongezeko la thamani ipungue kutoka 18% hadi 15%.

Pili kodi ya kuagiza magari ipungue, watanzania tunaendesha mikweche ya miaka 20, 17 iliyopita. Tunataka kodi ipungue tusukume gari kali za miaka ya karibuni.

Kodi za gari Tanzania ni za ajabu Dunia. Nashukuru yule kamishna wa kodi za nje mlimtimua pale TRA, alikua anamshauri Magufuli ujinga. Mpumbavu sana. Alikua anajipangia kuongeza CIF ya magari ambayo alikua anajua anapoitoa mwenyewe. Nashukuru Magufuli alimshtukia baadae akamuondoa pale.

Haiwezekani watanzania tunaendesha magari ambayo huko kwa wenzetu yamepigwa marufuku. Gari ya miaka 20?

Punguza kodi za gari punguza ajali, punguza uchafuzi wa mazingira, okoa maisha.
Hapa kwenye kodi za magari ndo janga kuu kabisa.Kodi kubwa kuliko hata gharama za kutengeneza gari kiwandani.
Magari yafaa yaingie bure Ili kukuza uchumi kupitia kodi na ajira.
 
Malimbikizo ya Mishahara yanalipwa mwezi huu wa tano, pia ni jambo la kushukuru, lkn pia 1% imepunguzwa.
Ahsante mama.
Kwani mwanzo malimbikizo yalikuwa hayalipwi?

Hujasikia uhakiki wa wafanyakazi hewa na vyeti feki bado kukamilika?

Jipe moyo hewa
 
Nyie ndo mnalalamika mkienda kwenye Taasisi za serikali mkapewa huduma mbovu haya Mambo ya kuwalipa vizuri watumishi yanaleta motisha katika kazi mtu anakua na bidii kwa sababu kazi anayofanya inamfanya aishi maisha mazuri kwa kupewa stahiki zake kwa wakati.kuja na hoja eti Kuna watu Hawa ajira uko mtaani ndo iwe sababu ya kutowaongezea mishahara watumishi ni ufinyu wa upeo katika kufikiri. Kwa sababu serikali inaajiri kwa kufuata majirani na imishaajiri inajukumu la kuboresha mishahara na mazingira ya kazi kwa mtumishi wake
Nyerere baba yetu wa taifa alifanya mengi mazuri lakini kama ilivyo kwa binadamu hakuna mtu asiye na kasoro. Miongoni mwa kasoro hizo ni kujenga nchi ambayo serikali ndiyo kila kitu, na kuiita nchi hiyo ya wakulima na wafanyakazi. Matokeo yake serikali yetu ni miongoni mwa serikali kubwa sana kimatumizi, na zaidi ya asilimia 75 ya makusanyo ya TRA yanalipa mishahara ya wafanyakazi wa serikali.

Mi mwenyewe mfanyakazi wa serikali lakini sometimes linapokuja suala la nchi ni upuuzi kuangalia maslahi binafsi. Hapa kazini kwangu taasisi ya umma kuna magari ya serikali yanapigwa mnada. Nilimuuliza dreva yana shida gani haya magari hadi mnayapiga mnada, jibu lake lilinihakikishia kwamba hii nchi bado sana aisee. Yaani gari moja linalopigwa lilikuwa gari la kutumia bosi wetu wa zamani lakini alipokuja mwingine akataka la kwake jipya. Hilo la zamani zima kabisa ila ndio hivyo halitumiki tena inabidi lipigwe mnada.

Nirudie tena, hizo ni pesa za walipa kodi, na walipa kodi wenyewe orijino ukiona jinsi wanavyojibana ili walau biashara zao ziende licha ya uchumi tepetevu msingekuwa na hizo hulka za matumizi mabovu ya pesa za walipa kodi. Kama suala la kutoa huduma za serikali liwe transaction, kwamba daktari wa hospitalini alipwe kulingana na thamani ya huduma yake, mwalimu, nesi, polisi, n.k, vivyo hivyo, mi naona ni sawa tu. Na ndivyo serikali inavyopaswa kuendeshwa kwa tija na itafutwe model ya kuquantify tija ya kila sekta ya umma kifedha, na wafanyakazi wa kila sekta walipwe kulingana na tija yao. Ila kwa sasa haiko hivyo, wengi wa wafanyakazi wa umma huduma zao hazilingani na mishahara wanayolipwa. Matokeo yake nchi haina uwezo wa kuongeza mishahara wakati huo huo itekeleze miradi ya maendeleo.
 
Serikali imepunguza kodi ya PAYE kutoka 9% na sasa itakuwa 8%

Punguzo hili litasababisha mshahara kuongezeka kadhalika kodi kwenye marupurupu imeondolewa.

Kazi Iendelee!
Hii 1% cut inawahusu watu wa kima cha chini. Kama wewe unapata mshahara kuanzia laki 540000. Endelea na kazi.
 
Marupurupu hayakua na kodi miaka mingi tu.

Marupurupu kama hela ya nyumba, chakula, nauli, safari nk hayakua na kodi.

Hiyo ya 8% ni ya watu wa kima cha chini cha laki 270,000.

Tunataka kodi ipungue kwa ambao mishahara wa digiti 7.

Kikubwa zaidi kodi ya ongezeko la thamani ipungue kutoka 18% hadi 15%.

Pili kodi ya kuagiza magari ipungue, watanzania tunaendesha mikweche ya miaka 20, 17 iliyopita. Tunataka kodi ipungue tusukume gari kali za miaka ya karibuni.

Kodi za gari Tanzania ni za ajabu Dunia. Nashukuru yule kamishna wa kodi za nje mlimtimua pale TRA, alikua anamshauri Magufuli ujinga. Mpumbavu sana. Alikua anajipangia kuongeza CIF ya magari ambayo alikua anajua anapoitoa mwenyewe. Nashukuru Magufuli alimshtukia baadae akamuondoa pale.

Haiwezekani watanzania tunaendesha magari ambayo huko kwa wenzetu yamepigwa marufuku. Gari ya miaka 20?

Punguza kodi za gari punguza ajali, punguza uchafuzi wa mazingira, okoa maisha.
Hi ni moja ya ahadi yangu nitakokuwa mgombea wa Urais.......ha ha ha ha ha ha. Nimeliona miaka mingi sana hili. Tukipunguza Kodi ya MAGARI, Magari mengi yataongezeka, mafuta yatanunulika sana, vipuri, matengenezo na kadhalika. Importation tax ya magari nchi hii inaumiza mno. Japo madhara ya magari mengi ni uchafuzi wa mazingira.
 
Serikali imepunguza kodi ya PAYE kutoka 9% na sasa itakuwa 8%

Punguzo hili litasababisha mshahara kuongezeka kadhalika kodi kwenye marupurupu

Je hii ni kwa wafanyakazi sekta zote au wa umma tu?
 
Back
Top Bottom